Monday, December 12, 2011

Mabomu yalipuka kaskazini mwa Kenya

Mabomu yalipuka kaskazini mwa Kenya

 11 Disemba, 2011 - Saa 18:44 GMT
Mashambulio mawili ya mabomu yaliyofanywa kaskazini-mashariki mwa Kenya, karibu na mpaka wa Somalia, yameuwa askari mmoja wa Kenya na kuwajeruhi wengine kama 10.
Jeshi la Kenya
Miripuko hiyo iliyotokea karibu na miji ya Mandera na Wajir, yaliwalenga askari waliokuwa wakipiga duru na msafara wa jeshi.
Mashambulio kadha yamefanywa nchini Kenya, tangu ilipotuma wanajeshi wake huko Somalia, kuwasaka wapiganaji wa Kiislamu wa kikundi cha al-Shabaab miezi miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment