Monday, December 5, 2011

FIFA Yasusiwa kwa ufisadi

FIFA Yasusiwa kwa ufisadi

 2 Disemba, 2011 - Saa 08:48 GMT
Sepp Blatter
Rais wa shirikisho la soka duniani Sepp Blatter
Shirika la kupambana na rushwa ambalo limekuwa likilishauri shirikisho la soka duniani FIFA baada ya shirikisho hilo kugubikwa na kashfa za rushwa na ufisadi, limevunja ushirikiano nalo.
Shirika hilo la Transparency International limesema halikufurahishwa na FIFA kupuuza mapendekezo yake ya msingi kwa shirikisho hilo.
Transparency International liliondoa msaada wake wa ushauri baada ya kuhoji mfumo huru wa uchunguzi katika kashfa zinazoikabili FIFA.
FIFA imekataa kuzungumzia suala la kuvunjika kwa uhusiano baina yake na Transparency International.

No comments:

Post a Comment