Monday, December 5, 2011

Laurent Gbagbo kufika mbele ya ICC

Laurent Gbagbo kufika mbele ya ICC

 5 Disemba, 2011 - Saa 03:28 GMT
Laurent Gbagbo kushtakiwa na uhalifu wa kivita
Rais aliyeondolewa madarakani nchini Ivory Coast Laurent Gbagbo anafikishwa mbele ya mahakama ya kimataifa ya Jinai ICC hii leo. Mwansiasa huyo anatarajiwa kufunguliwa mashtaka ya uhalifu wa kivita. Gbagbo alipelekewa nchini Uholanzi wiki jana.
Mahakama ya ICC imemtuhumu Gbagbo kwa makosa ya uhalifu wa kivita kufuatia machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa Ivory Coast mwaka jana alipopinga kuyakabidhi madaraka kwa mpinzani wake,Alassane Ouattara, ambaye sasa ndiye rais wa Ivory Coast.
Kiongozi huyo ambaye ndiye rais wa kwanza kufikishwa mbele ya ICC atasomewa makosa yake chini ya sheria za mkataka wa Roma uliounda mahakama hiyo. Baada ya kusomewa mashtaka yake itakuwa jukumu la majaji waandamizi kuamua siku ya kusikizwa kwa kesi dhidi ya Laurent Gbagbo.


Jeshi la Iran linasema ndege yenyewe haikuwa na rubani
Kanisa Katoliki lataka amani na utulivu kudumishwa wakati nchi ikisubiri matokeo ya ubunge na urais

No comments:

Post a Comment