Sunday, January 15, 2012

Ndege mbili zashambulia Jilib, Somalia


Ndege mbili zashambulia Jilib, Somalia

 15 Januari, 2012 - Saa 18:24 GMT
Ndege mbili zimeshambulia mji wa Jilib, kusini mwa Somalia - eneo linalodhibitiwa na wapiganaji wa Kiislamu, la al-Shabaab.
Wanajeshi wa Somalia
Wazee wa mji huo wameiambia BBC, kwamba watoto 6 waliuwawa katika shambulio hilo.
Kuna taarifa zisemazo kuwa wapiganaji wa al-Shabaab ni kati ya watu waliokufa.
Msemaji wa jeshi la Kenya, ameiambia BBC, kwamba alikuwa anajaribu kuthibitisha ikiwa ndege za Kenya zilishiriki katika mashambulio hayo.

No comments:

Post a Comment