Sunday, January 29, 2012

POAC team probes 500m/- misuse at varsity college

POAC team probes 500m/- misuse at varsity college

26th January 2012
Print
Comments
Parastatal Organisations Accounts Committee (POAC), committee`s Chairperson, Zitto Kabwe
Parastatal Organisations Accounts Committee (POAC) has formed a subcommittee to investigate reports of misuse of more than 500m/- at Mkwawa University College of Education (MUCE).
The committee’s Chairperson, Zitto Kabwe said the funds were linked to the Higher Education Students Loans Board (HESLB), adding that the committee has decided not to approve the university’s accounts for the 2009/2010 fiscal year.
The Kigoma-North lawmaker said the Controller and Auditor General’s (CAG) report for the financial year 2009/2010 showed that more than 260m/- was used to purchase various types of chemicals for laboratory tests while 60m/- from the Loans Board was allocated to fake students at the university.
“We have noted that the prices for the chemicals were doubled…this proves that Mkwawa University is among institutions that doesn’t follow procurement procedures,” Kabwe said.
On the students’ loans scam, he said the committee observed that there were two payment vouchers with forged names of 31 students. He said the names had the same registration and index numbers but with a slight difference in their surnames.
Kabwe said the sub-committee will be led by Mwibara Member of Parliament Kangi Lugola (CCM), naming Kwamtipura legislator, Ali Khamis (CCM) and Special Seats MP Zainabu Kawawa (CCM) as members. He has given them a week to complete investigations into the matter.
He said the sub-committee will collaborate with the CAG’s office, adding that if it is proven that the funds were embezzled, the committee would suggest that the sub-committee conduct similar investigations in other universities.
The committee also found payments which did not have supporting documents, citing salaries being issued without receipts while it is known that all government payments must be supported with receipts.
For his part, the University Principal Prof Philemon Mushi backed the committee’s decision to make further investigations into the university expenditure.


He promised to offer full cooperation to the sub-committee in order to facilitate investigation. 

Meanwhile, the Local Authority Accounts Committee (LAAC) refused to approve the financial report for Pangani district, Tanga region for the fiscal year 2009/2010.
The committee Chairman, Augustino Mrema said they didn’t approve the report because the District Executive Director Neneka Rashid did not submit the report to the CAG’s office on time.
“He was supposed to submit the account books to the CAG five days before they were brought to the committee. We cannot approve them since they have been submitted to us directly,” he noted.
According to Mrema 15 percent of the DED’s January salary will be deducted as penalty.
SOURCE: THE GUARDIAN

Wasunni Iraq waacha kususia bunge

Wasunni Iraq waacha kususia bunge

 29 Januari, 2012 - Saa 17:13 GMT
Chama kikuu cha Wasunni nchini Iraq kinasema kitaacha kususia bunge, ili kusaidia kupunguza msukosuko wa kisiasa, ambao watu wengi wakiona unaweza kurejesha vita vya kidini.
Bunge la Iraq
Chama cha Iraqiya kilisema hatua yao ni kuonesha nia njema kabla ya mazungumzo baina ya vyama vya siasa vya Wasunni, Washia na Wakurdi.
Lakini chama hicho kimesema kwa sasa, kitaendelea kususia baraza la mawaziri.
Msukosuko ulizuka mwezi uliopita baada ya waziri mkuu, Nouri al-Maliki, ambaye ni Shia, kutoa amri kuwa kiongozi mmoja wa Iraqiya akamatwe.
Wanasiasa wa Kisunni walimuelezea Bwana Maliki kuwa dikteta.
Mashambulio kadha ya mabomu dhidi ya maeneo ya Washia yalizidisha wasiwasi.

Viongozi wa AU wakutana


Viongozi wa AU wakutana

 29 Januari, 2012 - Saa 16:26 GMT

Mkutano wa viongozi wa Umoja wa Afrika umeanza mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Makao Makuu mepya ya AU, mjini Addis Ababa
Kumetolewa wito kuwa nchi mbili za Sudan zimalize mizozo yao kuhusu mafuta, ambayo wadadisi wanasema, inatishia kuzusha tena vita kamili.
Na katika hotuba yake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, ametoa wito kwa viongozi wa Sudan kufikia makubaliano.
Huu ndio mkutano wa mwanzo wa kilele wa AU tangu maandamano ya nchi za Kiarabu kuanza, na kumetolewa onyo kwamba ikiwa uongozi haikutengenea, basi mtibuko huo unaweza kutapakaa hadi kusini.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, alisema matukio yameonesha kuwa ukandamizaji siyo suluhu.
Alisema wanaume na wanawake walioandamana mitaani walitia moyo, na waliwakumbusha viongozi kwamba lazima wawasikilize.
Mkutano huu unaofanywa kwenye jengo jipya la AU, lilojengwa kwa msaada wa Uchina, unatokea wakati kuna wasiwasi mkubwa kuhusu mvutano baina ya Sudan Kaskazini na Kusini.
Baadhi ya wadadisi wanaonya kuwa vita kamili vinaweza kuanza tena baina ya majirani hao wawili.

Friday, January 20, 2012

Dk Slaa: Kwa nini sikumsalimia JK

Dk Slaa: Kwa nini sikumsalimia JK                           
 Send to a friend
Thursday, 19 January 2012 20:42
0digg
Fredy Azzah
KATIBU Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa  amesema kuwa, hakuweza kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete kutokana na Jiografia ya eneo la makaburini lilivyopangwa na watu wa usalama wa taifa pamoja na kamati ya mazishi kutomruhusu kufanya hivyo.

Hata hivyo Dk Slaa alisisitiza kuwa, kwa upande wake, kwenye msiba siyo sehemu ya kwenda kwa ajili ya kusalimiana na watu ama kurekebisha mambo yaliyoharibika bali ni sehemu ya kumwombea marehemu.

 “Siyo hulka ya Dk Slaa kutumia misiba kama sehemu ya kusalimiana, wala kutengeza mambo yaliyoharibika, mimi huwa naenda kwenye msiba kwa lengo moja tu la kumwombea marehemu, huwa simtazami hata mtu aliyekaa pembeni yangu,” alisema Dk Slaa alipozungumza kwa njia ya simu  jana.

Alifafanua kuwa, katika eneo la makaburi kulikuwa na mabanda matano ambayo yalipangwa kwa ajili ya Askofu, Rais, Viongozi wa vyama vya siasa, mwili wa marehemu  na familia na banda jingine lilikuwa la watu wengine waliohudhuria mazishi hayo.
“Sasa kutoka alipokuwa amekaa Rais mpaka kwenye banda nilipokuwa mimi, kulikuwa na umbali wa karibu  mita 20, sasa mlitaka nikimbie kumsalimia Rais nivunje protokali kisha nikamatwe na usalama wa taifa,” alisema Dk Slaa. Alisema alikuwa mtu wa kwanza kufika makaburini kwa lengo la kuangalia jinsi kaburi la mbunge wa chama chake lilivyochimbwa kisha akaonyeshwa sehemu ya kukaa na watu wa usalama wa taifa.

 Alisema kuwa, hata katika wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Regia Mtema, katika ukumbi wa Karejee, kulikuwa na utaratibu kama huo ambapo ilitengwa sehemu ya kukaa Makamu wa Rais, Spika wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani na Makamu wake na yeye Dk Slaa akawekewa sehemu yake kama Katibu wa Chama alichokuwa akikitumika marehemu.

 “Mimi sipendi kuweka siasa kwenye mambo kama ya msiba, Dk Slaa siyo kichaa siyo kichaa aanze kukimbia kumsalimia Rais. Katika sehemu kama ile Rais huwa anakuja baada ya watu wote wakiwa wameshakaa, yeye ndiye hupita na kuanza kusalimia watu na hamjaona hata sehemu moja aliponyoosha mkono kunisalimia nikamkwepa,” alisema Dk Slaa:

 “Msiba siyo mahali pa kutengeza urafiki, au kutengeza mambo yaliyo haribika, pale ni ibada tu na kumuombea marehemu siyo sehemu ya kufanya siasa” alisisitiza Dk Slaa. Jana baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa, Dk Slaa alishindwa kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete katika mazishi ya Regia Mtema yaliyofanyika kijijini kwao Ipangalala Morogoro juzi.Regia alifariki dunia Januari 14 kwa ajali ya gari iliyotokea katika eneo la Ruvu mkoani Pwani.  

Mbunge mwingine afariki - TANZANIA

Mbunge mwingine afariki  Send to a friend
Thursday, 19 January 2012 20:51
0digg
Mbunge wa Arumeru Mashariki (CCM),Jeremiah Solomon Sumari
NI JEREMIAH SUMARI WA CCM KUAGWA KESHO KARIMJEE
Fredy Azzah na Patricia Kimelemeta
SIMANZI nyingine imelikumba Bunge la Tanzania, kufuatia kifo cha Mbunge wa Arumeru Mashariki (CCM), Jeremiah Solomon Sumari (60),aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa muda mrefu akipatiwa matibabu.

Kifo cha Sumari kimetokea siku moja tu, tangu kufanyika kwa mazishi ya Mbunge wa Viti Maalum (Chadema),  Regia Mtema aliyefariki dunia kwa ajali ya gari, Jumamosi iliyopita katika eneo la Ruvu mkoani Pwani.

Sumari alianza kuugua kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, hali ambayo ilimfanya aende kampeni katika mazingira magumu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mtoto wa kwanza wa marehemu, Sioi Sumari alisema baba yake alipatwa na mauti katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alipokuwa amelazwa.

“Baba amefariki saa 8.30 usiku katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu,” alisema Sioi.
Alifafanua kuwa, marehemu anatarajiwa kuzikwa Jumatatu ijayo kijijini kwake katika jimbo la Arumeru Mashariki.
Mtoto  huyo wa marehemu alisema baba yake utaagwa kesho (Jumamosi ) jijini Dar es Salaam, kabla ya kusafirishwa kwenda Arusha.

Ofisi ya Bunge Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alisema ofisi ya Bunge imepokea kwa masikitiko msiba huo kwani umetokea muda mfupi tangu waliporejea kutoka kwenye maziko ya Mtema.Hata hivyo, alisema  kutokana na hali hiyo shughuli za Bunge zitaendelea kama zilivyopangwa na kwamba, zitasimamishwa siku ya kuaga mwili wa marehemu.

“Leo (jana) na kesho tutaendelea na shughuli za bunge kama kawaida, lakini siku ya kuaga tutasitisha shughuli ili kutoa fursa kwa wabunge kushiriki kwenye mazishi ya marehemu Sumari,” alisema Dk Kashililah.   Alisema  kwa sasa wanafanya taratibu za mazishi ya marehemu kwa kushirikiana na familia yake.

Alifafanua kwamba kutokana na hali hiyo, bunge limepata pigo kubwa baada ya kuondokewa na wabunge wawili katika kipindi kimoja, jambo ambalo limesababisha wabunge kushikwa na butwaa.Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema Kamati ya Uongozi ya Bunge itakutana leo kujadili namna ya kuratibu mazishi ya mbunge huyo.

Alisema  kuna uwezekano mbunge huyo akaagwa katika ukumbi wa Karimjee, kama ilivyofanyika kwa mbunge wa Chadema Regia Mtema.

“Tunasikitika sana kwa kuwapoteza wabunge wawili ndani ya muda mfupi,” alisema Ndugai.

Kikwete amlilia
Kwa upande wake, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge, Anne  Makinda  kutokana na kifo cha Sumari.

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Rais Kikwete ikisema; “Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha Mheshimiwa Jeremia Solomon Sumari….”
“Alikuwa kiongozi aliyewatumikia vema wananchi wa Jimbo lake la Uchaguzi la Arumeru Mashariki na Taifa kwa ujumla katika wadhifa wake wa Waziri kwa umahiri na uhodari mkubwa.”

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Kikwete alisema kutokana na kifo cha Sumari, wananchi wa Arumeru Mashariki wamepoteza kiongozi wa kutegemewa. “Kwa moyo dhati, natuma salamu za rambirambi na pole kwa familia ya marehemu Jeremia Sumari kwa kumpoteza kiongozi na mhimili madhubuti wa familia,” taarifa hiyo ilimnukuu Rais Kikwete.   Alifafanua akisema; “Ninawahakikishia kwamba nipo pamoja nanyi katika kuomboleza msiba huu mkubwa na namuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema aipumzishe roho ya marehemu Jeremia Solomon Sumari mahali pema peponi, Amina.”

 Lowassa amlilia
Mbunge wa Monduli,  Edward Lowassa alisema taifa limepata pigo kubwa kwa kuondokewa na Sumari.
 “Alikuwa mchapakazi sana.., hii imesababisha kuteuliwa kuwa Naibu Waziri katika serikali ya awamu ya nne, kutokana na umahiri wake,” alisema Lowassa.
Lowassa aliongeza kwamba, kutokana na hali hiyo, wananchi wa Arumeru Mashariki wamekosa mwakilishi wa kutetea maslahi yao bungeni.

 Historia yake
Sumari  alizaliwa Machi 2 mwaka 1943, katika kijiji cha Akeri wilayani Arumeru mkoani arusha.
Alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Meru Magharibi kati ya mwaka  1950 na 1957. Kati ya mwaka  1958- 1964 alisoma katika shule ya sekondari ya Old Moshi, mkoani Kilimanjaro na baadaye aliendelea na elimu ya juu nchini Uingereza.

Taarifa zinaonyesha kuwa, Sumari alipata elimu ya masoko kwa ngazi ya cheti ACCA, CIS, (Certificatein Marketing and Lincesed Broker lr), nchini Uingereza na baadaye kupata CPA nchini.
Kwa upande wa utumishi wake, mwaka 1996 mpaka 2004 alikuwa Mkurugenzi wa Bodi ya Boko la Disa Dar es Salaam (DSE).
Kisiasa , kuanzia mwaka 2005 mpaka mauti yalipomkuta alikuwa Mbunge wa jimbo hilo la Arumeru Mashariki kwa tiketi ya CCM.

Januari 4 mwaka 2006, aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana na mwaka 2008 mpaka 2010 alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchum

Ufisadi wa mabilioni tena Nishati na Madini

Ufisadi wa mabilioni tena Nishati na Madini  Send to a friend
Thursday, 19 January 2012 20:47
0digg
Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe
Leon Bahati
SERIKALI kupitia Wizara ya Nishati na Madini imeingia tena katika kashfa ya ufisadi wa matumizi mabaya ya rasilimali za umma, baada ya kubainika kuuza kinyemela sehemu yenye utajiri mkubwa wa makaa ya mawe Kiwira kwa kampuni ya Tan-Power Resources (TPR).

Uamuzi huo unaelezwa na wachunguzi wa mambo kuwa utaathiri mradi wa kuzalisha umeme wa makaa ya mawe kwa kusababisha bei ya nishati itakayozalishwa eneo hilo kuwa ghali na italisababishia serikali hasara ya dola za Marekani 600 milioni sawa na Sh960 bilioni.

Tuhuma hizo za ufisadi, ziliibuka kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na kuifanya iwaite maofisa wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini kujieleza mbele yao, jana.

Sehemu inayodaiwa kuuzwa ilitajwa kuwa ni mlima Kabulo, ambayo aliielezea kuwa ina utajiri mkubwa zaidi wa makaa ya mawe kuliko eneo jingine la Kiwira.

Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe alithibitisha kamati yake kuwaweka 'kitimoto' maofisa waandamizi wa wizara hiyo.

"Tumewaita ili watupe maelezo ya kina kuhusu suala hilo," alisema Zitto akilalamika; "Hili ni tatizo la kuchezea raslimali za nchi,"

Zitto ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni alisema tukio hilo limekuja wakati ambao serikali imetakiwa kumiliki hisa zote za mradi huo ili kuhakikisha anapatikana mbia anayeweza kuendesha mradi huo kwa faida.

Alisema mradi huo ambao ulikuwa unamililikiwa kwa pamoja kati ya serikali na kampuni ya Tan-Power Resourses, ulitakiwa kusimamishwa pia wafanyakazi walipwe haki zao.

Lakini mpaka sasa, alisema wafanyakazi hawajalipwa ingawa mradi huo umesimama jambo ambalo linaendelea kuisababishia hasara serikali.

Akizungumzia athari za kuuzwa kwa eneo lenye utajiri mkubwa wa makaa ya mawe, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka alisema mradi wa umeme unaotarajia kuanzishwa, gharama yake itakuwa kubwa kutokana na malighafi kuzalishwa na kampuni nyingine.

Ole Sendeka alisema Serikali ilikopa Benki ya Dunia dola za Marekani 600 milioni sawa na Sh960 bilioni kwa ajili ya kuendeleza mradi huo lakini kwa kuuzwa sehemu ya Kiwira, serikali itapata hasara kwa kulipa fedha hizo na riba yake kwa mradi ambao unamilikiwa na kampuni binafsi.

Hadi jana jioni Mwananchi lilipoondoka katika ofisi za Bunge, watendaji wa Wizara walikuwa bado hawajawasilisha maelezo yao mbele ya kamati hiyo.

Historia ya Kiwira
Kiwira ni moja ya miradi ambayo Serikali imeiweka katika orodha ya kuzalisha umeme ili kuliokoa taifa kwenye uhaba mkubwa wanishati ya umeme.

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliwahi kuliambia bunge kuwa Serikali imeamua kubeba mzigo wa mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira ili kuhakikisha kuwa unaleta tija kwa Taifa.

Kampuni ya TPR inadaiwa kumilikiwa na  familia ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Waziri wa zamani Nishati na Madini, Daniel Yona.

Ngeleja alikuwa ameliambia bunge kuwa baada ya uamuzi huo, serikali imeanza mchakato wa kupata uratatibu muafaka wa kuendesha mradi huo kama ilivyokusudiwa kwa kuangalia fursa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuingia mkataba wa uendeshaji na kampuni itakayopewa mamlaka ya kujenga na kuuendesha.

“Chini ya mkataba wa uendeshaji, mkandarasi atapewa jukumu la kujenga uwezo wa mashirika ya Stamico (Shirika la Madini) na Tanesco ili kuyawezesha kumiliki na kusimamia mradi huo,” alisema.

Kwa mujibu wa Ngeleja, hatua ya awali ya mpango wa serikali kuanza kuundesha mradi huo zilikuwa zimeanza kwa kuhakikisha kuwa wafanyakazi waliopo wanalipwa haki zao zote na kuwawekea mazingira mazuri ya kuendelea na kazi.

“Serikali pia imezungumza na serikali rafiki ya China iliyoanzisha na kuendesha mradi huo ili kupata mkopo wa kuufufua na kuhakikisha mradi wa kuzalisha umeme wa MW 200 unakamilika mapema iwezekanavyo,” alisema

Akizungumzia suala la Rais Mstaafu Mkapa ambaye aliomba kumiliki hisa 200,000, kupitia kampuni yake ya ANBEN Limited, Ngeleja alisema kuwa kiongozi huyo wa zamani alinyang’anywa hisa hizo Januari 10 mwaka 2005 baada ya kushindwa kuzilipia.

 “Mheshimiwa Spika, tarehe 10 Januari, 2005, (Siku 13 tangu kuanzishwa kwa TPR), ANBEN Limited iliondolewa kuwa miongoni mwa wamiliki wa hisa kwa vile haikuweza kulipia hisa ilizokuwa imechukua wakati wa usajili wa TPR.

Hivyo wamiliki wa TPR waliobaki walikuwa ni DevConsult International Ltd, Universal Technologies Ltd, Choice Industries Ltd na Fosnik Enterprises Ltd zote zikiwa na hisa 200,000,” alisema Ngeleja.

Wakati huo huo, Zitto alisema jana waliwahoji maofisa waandamizi wa Wizara ya Uchukuzi kwa kile kilichodaiwa ni Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kuingia kwenye mikataba inayoliingizia taifa hasara.

Zitto hakutaja mambo yaliyofanywa na ATCL na kuisababishia hasara serikali lakini taarifa zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa linatakiwa kuilipa kampuni ya kigeni dola za Marekani 36 milioni.

Fedha hizo zinadaiwa kuwa zilitolewa kwa ajili ya kukodisha ndege ambayo hata hivyo haikuwahi kufanya kazi nchini.

Eritrea ilihusika na mauaji

Eritrea ilihusika na mauaji

 19 Januari, 2012 - Saa 04:45 GMT
Watalii waliotekwa nyara
Watalii waliotekwa nyara
Ethiopia imelaumu taifa jirani la Eritrea kwa kuwaua na kuwateka nyara watalii kutoka Ulaya katika eneo la mpaka kati ya mataifa hayo mawili.
Watalii watano waliuawa na Wajerumani wawili na Waethiopia wawili katika shambulio hilo la Jumatatu.
Serikali ya Ethiopia imesema hiyo si mara ya kwanza kwa Eiritrea kutekeleza visa vya ugaidi dhidi ya watalii wanaotembelea Ethiopia.
Lakini Eritrea imekanusha kuhusika na tukio hilo. Mwakilishi wake katika Muungano wa Afrika, Girma Asmeron, ametaja madai hayo kama "uongo mtupu."
Mataifa hayo mawili yalipigana katika mzozo wa mpaka kati ya mwaka 1998 na mwaka 2000.

Ikulu ya White House yarushiwa bomu


Ikulu ya White House yarushiwa bomu

 18 Januari, 2012 - Saa 03:42 GMT

 

Watu wamehamishwa kwa muda kutoka kwa Ikulu ya White Hosue nchini Marekani baada ya bomu ya kutoa moshi kurushwa ndani ya ua la jengo hilo.
Ripoti zinasema kuwa jengo hilo ambalo ni ofisi ya rais Barrack Obama, ilifungwa kwa muda huku maafisa wa idara ya uchunguzi nchini humo CIA, wakifanya uchunguzi kufuatia uvumbuzi wa kifaa killichoonekana kuwa bomu la kutoa moshi.
Msemaji wa idara hiyo ya ujasusi George Ogilvie, amesema kuwa kifaa hicho kilirushwa kupitia ua la jengo hilo wakati waandamanji wapatao 1500 walikuwa wakiandamana nje ya Ikulu hiyo ya rais.

Thursday, January 19, 2012

Ripoti ajali ya meli yatolewa Zanzibar


Ripoti ajali ya meli yatolewa Zanzibar

 20 Januari, 2012 - Saa 04:50 GMT
Zanzibar, Tanzania
Serikali ya Zanzibar leo imetoa ripoti ya uchunguzi wa kuzama kwa meli ya MV Spice Islander hapo Septemba 10, 2011 eneo la Nungwi, Kaskazini mwa kisiwa cha Unguja.
Aliyetoa ripoti hiyo kwa niaba ya serikali alikuwa katibu kiongozi, Abdulahamid Yahya Mzee baada ya kupokelewa na Rais wa Zanzibar Dr Ali Muhammed Shein Novemba 30 mwaka jana kutoka kwa Jaji Abdulhakim Ameir aliyeongoza jopo la watu 10.

Yahya akielezea sababu zilizogunduliwa na tume kuwa chanzo cha kuzama kwake ni kujaza abiria kupita kiasi, mizigo kuwekwa vibaya, matatizo ya kiufundi yaliofanya kiwango cha upakizi kisijulikane, kuingia maji na uzembe wa nahodha kutoomba msaada.

Pia imetoa hesabu ambayo sasa itakuwa rasmi ya watu waliopotea na waliozama ambapo inasimama kuwa 1370.

Tume imesema abiria waliopakiwa katika meli hiyo walikuwa 2,470 wakati uwezo wake ulikuwa ni watu 620 ikiwa ni karibu kidogo ya mara nne zaidi ya uwezo wake.

Tume imesema ubovu wa meli hiyo ulijulikana tokea mwezi Julai, miezi miwili kabla ya kuzama kwake kutokana na ukaguzi uliofanywa na taasisi ya usalama wa bahari Sumatra, lakini bado meli hiyo ilipewa leseni.
Maiti za watu waliofariki kwenye ajali ya MV Spice Islander


Taarifa imesema kuna mnyororo mrefu sana wa watu waliokuwa na dhamana lakini walishindwa kufanya wajibu wao kuanzia maafisa wa meli hiyo, maafisa wa bandari na pia maafisa kama vile wa polisi na taasisi ya kukusanya mapato TRA, ambao wanatuhumiwa kupokea fedha na kupenyeza abiria.

Tume hiyo imependekeza watu kadhaa washtakiwe na imetaja makosa iliyoona yanawahusu na polisi waliwatia mbaroni watu kadhaa sku ya Jumatano katika kutekeleza hilo.
Watu muhimu watakaoshtakiwa ni pamoja na Abdula Muhammed mrajis wa meli, Haji Vuai Ussi mkurugenzi wa usafiri wa baharini, Juma Seif mkaguzi wa meli na wamiliki watano wa kampuni za Visiwani Shipping na Al Gubra Marine Services.

Pia nahodha Abdullah Kinyaiite anatakiwa kushtakiwa lakini serikali alikiri katibu kiongozi hajulikani alipo na tume haikusema yuhai au la.

Jana polisi ilitia kishindo mji wa Zanzibar kwa kamata kamata ya watuhumiwa hao, lakini haikujulikana iwapo leo walipelekwa mahakamani au la au ni lini taratibu zitakamilika na kusomewa mashtaka yao.

Mwandishi wetu wa Zanzibar Ally Saleh amesema ripoti hiyo pia inataja orodha ya watu ambao wameonekana wanafaa kuchukuliwa hatua za kinidhamu na mmoja wao ni mkurugenzi wa shirika la bandari Mustafa Aboud Jumbe ambaye kama wengine wataondoshwa sehemu zao za kazi mara moja.
Waliojiokoa kwenye ajali Zanzibar

Kwa bahati meli hiyo ilikuwa imewekewa bima isipokuwa bima hiyo haitahusu mizigo kwa sababu eneo hilo halikuwa limekingwa, lakini bima hiyo itasaidia kulipa jamaa za watu waliofariki dunia na tume imependekeza angalau kiwango cha shs 10,000,000 kwa kila mtu aliyefariki dunia kwa maana ya pia waliopotea.

Pia serikali imesema itazigawa kwa waathirika na jamaa waliofiwa fedha zote zilizokusanywa ikiwa ni michango mara taratibu zitapokamilika lakini kazi hiyo sasa ni rahisi kwa vile orodha kamili na iliyohakikiwa imeshapatikana.

Serikali imesema ripoti hiyo itachapishwa kwa uwazi na ukamilifu na kuweza kusomwa na kila mtu ikiwa na pamoja na kwenye mtandao.

Watu 6 wauawa mjini Mogadishu.


Watu 6 wauawa mjini Mogadishu.

 20 Januari, 2012 - Saa 04:46 GMT
Mlipuko wa bomu mjini Mogadishu
Mlipuko wa bomu mjini Mogadishu
Mlipuko wa Bomu umetokea ndani ya kambi iliyofurika katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu, muda mfupi baada ya kundi la maafisa wa Umoja wa Mataifa kuondoka mahali hapo.
Takriban watu sita wamefariki na inahofiwa idadi hiyo ikaongezeka kwani watu wengi zaidi wamejeruhiwa.
Mlipuko huo ulitokea muda mfupi baada ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa na waandishi wa Habari wa kimataifa kuzuru eneo hilo.
Mwandishi wa BBC Odhiambo Joseph alikuwa miongoni mwa waandishi wa habari kwenye msafara wa Umoja wa Mataifa, uliokuwa ukikagua oparesheni za utoaji misaada na akashuhudia mlipuko huo.
Shirika la kimataifa la kutoa misaada la Medicine Sans Frontiers limesema kuwa limefunga vituo vyake viwili vya matibabu katika mji mkuu wa nchi hiyo Mogadisu, kufuatia kuuawa kwa wafanyakaza wake wawili.
Wawili hao waliuawa mwezi uliopita na mmoja wao alikuwa raia wa Ubelgiji na mwingine kutoka Indonesia
kufuatia uamuzi huo shughuli za shirika hilo mjini Mogadishu zimepunguzwa kwa asilimia 50.
Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo, Christopher Stokes amesema ni vigumu kusitisha huduma muhimu katika eneo ambalo huduma hizo zilihitajika ili kuokoa maisha ya raia.
Kufuatia mauaji hayo imekuwa vigumu kwa shirika hilo kuendelea kuhudumu katika wilaya hiyo ambayo mauaji hayo yalitokea.

Madaktari, Serikali ngoma nzito

Madaktari, Serikali ngoma nzito  Send to a friend
Wednesday, 18 January 2012 21:02
0digg
Geofrey Nyang'oro
MGOGORO baina ya Serikali na madaktari umeingia sura mpya baada ya wanataaluma hao kutoa madai mapya ikiwa ni pamoja na kuongezewa posho, huku Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Lucy Nkya akiwapiga chenga kuhudhuria mkutano wao uliofanyika Dar es Salaam jana.
Juzi, Dk Nkya alitoa tamko la Serikali kuhusu mgogoro huku akitupilia mbali madai ya wataalamu wa tiba ya magonjwa ya binadamu na kutetea uamuzi wa kuwahamisha na kuwapangia vituo vipya vya kazi baadhi yao kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk Namala Mkopi alisema moja ya sababu za mkutano wa jana ilikuwa ni kujibu kauli hiyo Serikali iliyotolewa na dhidi ya madai yao.

Alisema tamko hilo la Wizara ya Afya lilikuwa la kisiasa zaidi kuliko uhalisia. Alisema madai ya madaktari ni kupatiwa nyumba za kuishi, kuongezewa posho za muda wa ziada za kazi ambazo sasa ni Sh10,000 na mishahara.

Akizungumza katika mkutano huo, mjumbe wa MAT, Dk Hamis Kigwangala alisema: “...Tunataka posho Sh200,000 na mshahara kima cha chini Sh 3.5 milioni.”

Kuhusu mshahara alisema wanayo haki ya kulipwa kiasi hicho cha fedha kwa kuwa Serikali ina fedha, ndiyo maana imewaongezea wabunge posho za vikao. “Tunastahili kulipwa... fedha ipo. Kwani wanazolipwa wabunge zinatoka wapi?.”
Alisema umefika wakati taaluma ya udaktari iheshimiwe na kuthaminiwa kwani ni kazi ya wito huku akipendekeza kufutwa kwa utaratibu wa kutoa vibali kwa vigogo kwenda kutibiwa nje, akisema ndicho kinachowatia kiburi hadi kuwapuuza madaktari.

“Anayesaini mgonjwa aende nje ni daktari na wakati mwingine hata kama mgonjwa anayeomba kwenda nje angeweza kutibiwa nchini. Utaratibu huo ni mbovu tugome kutoa vibali ili tuanze kuthaminiwa,” alisema.

Kwa upande wake, Dk Zaituni Sanya alisema kumekuwa na vitendo vya kupuuzwa kwa madaktari: “Sasa umefika wakati wa Serikali kuwathamini wana taaluma, tumechoka kunyanyaswa.”

Kabla ya kuanza mkutano wa jana, madaktari hao walituma ujumbe wa madaktari watatu wakiongozwa na Makamu wa Rais MAT, Dk Primus kwenda kumtaka Dk Nkya afike ili azungumze nao ana kwa ana kuhusu matatizo yao bila mafanikio.
“Mheshimiwa tumemwona na tumezungumza naye kwamba mmetutuma kumwita aje, amekubali lakini anaomba apewe muda wa saa moja ili ajiandae,” alisema Dk Saidia mara baada ya kurejea mkutanoni akitokea Wizara ya Afya.

Hata hivyo, baada ya saa moja kupita bila ya Naibu Waziri huyo kutokea, Dk Saidia aliwaambia wajumbe zaidi ya 200 waliohudhuria mkutano huo kwamba alipokea simu kutoka kwa kiongozi huyo akisema kwamba asingeweza kufika jana kama alivyokuwa ameahidi na badala yake akaomba wakutane leo.



Katika madai yake ya msingi, MAT inataka kurejeshwa kwa madaktari wote waliokuwa wakifanya mazoezi ya vitendo MNH na kupitiwa upya uamuzi wa kuwahamisha madaktari bingwa 61, kutoka hospitali hiyo ya taifa.
Madaktari 194 waliokuwa wakifanya mazoezi ya vitendo Muhimbili waliondolewa na kupelekwa katika vituo mbalimbali baada ya kuibuka kwa mgogoro wa malipo.

Msimamo wa Serikali

Katika tamko lake, Serikali ilisema tathmini iliyofanywa na wizara ilibaini kuwa idadi ya madaktari waliokuwa katika mafunzo kwenye hospitali ya Muhimbili ni kubwa kuliko uwezo wake akisema wingi wao ungeathiri mafunzo ya taaluma yao.

Pia ilisema uongozi wa hospitali hiyo ulilazimika kuwaandikia barua ya kuwarejesha wizarani, kutokana na kitendo chao cha kugoma huku ikisisitiza kwamba hawakufukuzwa kazi, bali walirejeshwa wizarani ili kupangiwa vituo vingine vya kazi kumalizia muda wao wa mazoezi kwa vitendo, baada ya kuvunja mkataba na uongozi wa hospitali hiyo.

“Kwa kuzingatia hatua zilichokuliwa na wizara na jinsi wahusika walivyotekeleza maagizo ya Serikali, hadi sasa ni dhahiri kuwa tamko la MAT kuhusu kunyanyaswa kwa madaktari walioko mazoezini halina msingi wowote,” alisema Dk Nkya alipokuwa akitoa tamko hilo juzi.

Dk Slaa ampiga chenga JK msibani

Dk Slaa ampiga chenga JK msibani  Send to a friend
Wednesday, 18 January 2012 21:08
0digg
Askari wa Bunge wakiuingiza kaburini mwili wa aliyekuwa mbunge wa viti maalum (Chadema) Regia Mtema wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Ipangalala Ifakara mkoani Morogoro jana.Picha na Juma Mtanda
AKWEPA KUKAA JUKWAA KUU, WENGI WAMZIKA REGIA
Juma Mtanda na Shakila Nyerere, Ifakara
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willbrod Slaa, jana alimkwepa tena Rais Jakaya Kikwete safari hii ikiwa katika mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya chama hicho, Regia Mtema yaliyofanyika katika Kijiji cha Lipangalala.Tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2010, ambao Dk Slaa alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 2,271,941 sawa na asilimia  26.34 akiwa nyuma ya Rais Kikwete aliyepata kura 5,276,827 sawa na asilimia 61.17, Dk Slaa hakuwahi kukutana na mkuu huyo wa nchi ana kwa ana.

Katika hafla ya kutangazwa matokeo ya urais iliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam, Dk Slaa hakuhudhuria tofauti na ilivyokuwa kwa waliokuwa wagombea wenzake wote.

Jana, Dk Slaa tofauti na viongozi wenzake wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, hakutaka kujiweka katika mazingira ambayo yangemkutanisha na Rais Kikwete katika mazishi hayo.
Nyumba kulikofanyika shughuli za awali za mazishi, waandalizi waliandaa majukwaa mawili, moja maalum kwa ajili ya wabunge huku jingine likiwa ni maalumu kwa ajili ya viongozi wakuu ambalo alikaa Mbowe, Spika wa Bunge, Anne Makinda, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe.

Mbali ya kukaa viongozi hao, kulikuwa na nafasi ambayo ilikuwa imetengwa maalumu kwa ajili ya Rais. Mbali ya nafasi hiyo, pia kulikuwa na kiti ambacho ilitegemewa kwamba Dk Slaa angekalia.
Hata hivyo, Katibu Mkuu huyo wa Chadema alikikwepa na kwenda kujichanganya katika jukwaa la wabunge na kiti hicho kubaki bila ya kuwa na mtu.

Hata hivyo, Rais Kikwete hakuweza kufika nyumbani hadi mwili wa marehemu Regia ulipopelekwa katika Viwanya vya Viungani ambako uliagwa na mamia ya waombolezaji.

Uwanjani hapo nako kulikuwa na majukwaa mawili. Kama ilivyokuwa nyumbani, jukwaa moja lilikuwa la wabunge na jingine la viongozi wa ngazi za juu lakini bado, Dk Slaa alilikwepa jukwaa hilo ambalo Rais alitarajiwa kuwa angefikia. Rais hakuweza kufika Viungani pia.

Rais Jakaya Kikwete akiweka udongo kwenye kaburi la aliyekuwa mbunge wa viti maalum (Chadema) Regia Mtema wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Ipangalala Ifakara mkoani Morogoro jana.Picha na Juma Mtanda
Baadaye wakiwa eneo la mazishi, Rais Kikwete alifika na kushiriki tukio hilo na kisha kusalimiana na wabunge mbalimbali na viongozi waliokuwa wamefika akiwemo Mbowe, Mbunge wa Rombo Joseph Selasini, Zitto na viongozi wengine lakini Dk Slaa hakuonekana.

Ilitegemewa kuwa tukio hilo la msiba lingewaleta wanasiasa hao lakini hadi Rais Kikwete alipoondoka hakuna mahali ambako walisalimiana.
Mbali ya tukio hilo, hata katika hafla mbalimbali ambazo viongozi wa Chadema wamekuwa wakialikwa ikiwemo Ikulu, Dk Slaa hakuwahi kuhudhuria.

Novemba mwaka jana viongozi wa Chadema wakiongozwa na Mbowe, walifanya mazungumzo na Rais Kikwete, Ikulu ya Dar es Salaam kujadili suala la Katiba Mpya, lakini Dk Slaa hakuhudhuria.


Chadema wahaha
Wakati viongozi wa Chadema wakihaha kumaliza mgogoro ndani ya chama hicho wilayani Kilombero, Pacha wa marehemu Regia, Remigia Mtema amesema ndugu yake Regia alikuwa akipeleka malalamiko kwa Dk Slaa mara kadhaa kuomba asuluhishe bila mafanikio.

Hata hivyo, Remigia alisema marehemu Regia alikuwa amepanga kuonana tena na Dk Slaa katika siku za hivi karibuni kumweleza kinachoendelea.

Akizungumzia suala hilo, Dk Slaa alisema alishaanza kushughulikia mgogoro huo lakini msiba huo ndiyo uliomkwamisha.

“Ni kweli nimekuwa nikielezwa tatizo hilo na tayari nilishaanza kulifanyika kazi ila sasa siwezi kusema suala hilo limefikia wapi kwani wote tuko kwenye mazishi,” alisema.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa wabunge wa Chadema waliotangulia kufika katika msiba huo, Mchungaji Peter Msigwa, Ezekia Wenje na Lucy Owenya, walikutana na uongozi wa kata wa Chadema ili kumaliza mgogoro huo.

Katibu mwenezi wa Chadema kata ya Ifakara, Antony Kamonalelo alisema viongozi hao walikaa na wanachama hao na kuwataka wapunguze munkari ili kumruhusu Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Kilombero, Salum Ngozi na Mbunge wa Viti Maalumu, Susan Kiwanga kuhudhuria mazishi.

Hata hivyo, inadaiwa kwamba wanachama hao waliukubalia uongozi huo kumruhusu Susan peke yake kuhudhuria mazishi hayo.

Juzi, wanachama hao walimtimua msibani Ngozi kiasi cha kuwalazimu polisi waliokuwa eneo hilo kuingilia kati kwa kumchukua mwenyekiti huyo na kumpeleka katika Kituo cha Polisi Wilaya.

Hiyo ilikuwa mara ya pili kwa Ngozi kutimuliwa katika msiba huo. Mara ya kwanza ilikuwa siku moja iliyotangulia ambayo ilimlazimu Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Francis Miti kuingilia kati.

Ngozi amekuwa akidai kwamba anafanyiwa fujo na kikundi cha watu aliowaita wahuni na kwamba amefungua kesi ya kufanyiwa vurugu katika Kituo cha Polisi Wilaya ya Kilombero na kwamba baada ya kumalizika kwa mazishi atasimamia suala hilo ili haki itendeke.