Thursday, April 19, 2012

JOGOO


FILAMU YA KANUMBA KUFA YANASWA


Marehemu Steven Charles Kanumba ‘The Great’.
Shakoor Jongo na Imelda Mtema
KIFO cha Steven Charles Kanumba ‘The Great’ kinazidi kuibua mapya kila kukicha ambapo tayari imebainika kuwa filamu aliyotengeneza na kuigiza hivi karibuni, imebeba maudhui ya kifo chake kwa asilimia 99, Ijumaa limeinasa ishu kamili.
Filamu hiyo aliyoitengeneza marehemu Kanumba mwenyewe ambayo bado haijaingia sokoni, mwanzoni ilikuwa inaitwa Love of Price lakini baadaye Kanumba aliibadilisha jina na kuiita Love & Power.
Kwa mujibu wa mwandishi wa muswada (script) wa filamu hiyo, Ally Yakuti, mazingira ya kifo cha Kanumba kwenye muvi hiyo yanafanana na kilichomtokea usiku wa kuamkia April 7, mwaka huu nyumbani kwake maeneo ya Vatican City Hotel, Sinza jijini Dar.

 STORI ILIVYO
Stori ya filamu hiyo inaonyesha kuwa Edwin (Kanumba) alitokea kumpenda mwanamke lakini kwa kuwa yeye alikuwa maskini, ‘demu’ huyo aliyetumia jina la Christina (Irene Paul) kwenye filamu hiyo alimkataa akidai kuwa hana hadhi.
Alisema kuwa wakati Edwin (Kanumba) anaendelea kumfuatilia, akasikia kuwa mwanamke huyo anaumwa na kupona kwake lazima ipatikane figo ya mtu mwingine ili awekewe.
Stori inaendelea kutiririka kuwa Edwin (Kanumba) anajitolea kutoa figo yake moja.
Muvi hiyo inaonesha kuwa baada ya kupona, Christina (Irene Paul) anagundua kuwa mwanaume ambaye hamtaki kwa sababu ya umaskini wake, ndiyo aliyenusuru maisha yake kwa kumtolea figo.
Stori inaendelea kuonesha kuwa katika hali hiyo, mwanamke huyo anakuwa hana jinsi hivyo anakubali kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Edwin (Kanumba).

ASUKUMWA, AFA PAPOHAPO
Katika filamu hiyo kuna kipande kinaonesha kuwa baada ya wawili hao kuishi kwa muda mrefu katika hali ya umaskini, Christina (Irene Paul) anashindwa maisha hayo, anambwaga Edwin (Kanumba) na kuwa na mwanaume mwingine.
Muvi hiyo inaendelea kuonesha kwamba kwa kuwa Kanumba alimpenda mwanamke huyo, hakukubali aondoke na katika kumzuia, ndipo mwanamke huyo alipomsukuma na kujigonga ukutani kisha akadondoka na kufa papohapo.

DAKTARI HUYOHUYO
Katika hali ya kushangaza, stori ya muvi hiyo inaonesha kuwa daktari ambaye anaonekana akimpima Edwin (Kanumba) kwenye filamu hiyo anayejulikana kwa jina maarufu la Kidume ndiye huyohuyo aliyempima Kanumba alipodondoka na kufariki dunia kiukweli usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita.

ALIYEMPELEKA MOCHWARI
Msanii wa filamu za Kibongo, Idrisa Makupa ‘Kupa’ ambaye kwenye filamu hiyo anaonekana akishiriki kumpeleka Edwin (Kanumba) mochwari, ndiye huyohuyo aliyeshiriki zoezi kama hilo la kumpeleka Muhimbili huku akimfumba macho baada ya kufariki kiukweli.

IRENE PAUL ANASEMAJE?
Akizungumza na Ijumaa juu ya ishu hiyo, mwigizaji Irene Paul ambaye kwenye filamu hiyo alitumia jina la Christina akionekana akimsukuma Edwin (Kanumba) na kufariki, alisema kifo cha staa huyo kimekatisha ndoto zake kwani ndiye aliyemwingiza kwenye filamu hivyo aliposikia habari hiyo mbaya ya kufa, mbali na kuzimia amekuwa akihisi bado ni ndoto.
“Kweli kwenye ile filamu nilimfanyia Kanumba mambo yote ambayo yamekuja kuwa ya kweli,” alisema Irene Paul akiangua kilio.

MASWALI TETE
Baada ya kujiridhisha na matukio yote ya kwenye filamu na uhalisia wa kifo cha Kanumba ndipo yaliboibuka maswali tete kuwa, je, Kanumba alifahamu juu ya kifo chake kwani kila kitu kipo kwenye filamu hiyo? Au ni nini kilichokuwa kikimtuma kufanya matukio yaliyoashiria tukio hilo?
TUJIKUMBUSHE
Kanumba alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumamosi ya Aprili 7, mwaka huu nyumbani kwake na kuzikwa Aprili 10 katika makaburi ya Kinondoni, Dar.

Bashir,"Nitawakomboa raia wa S.Sudan"

Bashir,"Nitawakomboa raia wa S.Sudan"

 18 Aprili, 2012 - Saa 18:45 GMT
Wanajeshi wa Sudan Kusini
Rais wa Sudan Omar al Bashir The Sudanese president, Omar al Bashir, amesema anataka kuwakomboa raia wa Sudan Kusini kutoka kwa serikali yao kufuatia mapigano yanayoendelea kwenye mpaka kati ya nchi hizo mbili.
Rais Bashir alisema haya katika mkutano wa hadhara mjini Khartoum akisema mipaka kati ya nchi hizo mbili haiwezi tena kuheshimiwa.
Amesema wakati umefika kuamua ikiwa Sudan itasalia na Juba au Sudan Kusini kusalia na Khrtoum.
Aliitaja Sudan Kusini kama mdudu ambao unafaa kuangamizwa.
Mapigano kati ya nchi hizo mbili yamesambaa nje ya eneo la Heglig lenya visima vya mafuta na ambalo linadhibitiwa na Sudan Kusini.

Magufuli augua ghafla, alazwa

Magufuli augua ghafla, alazwa  Send to a friend
Wednesday, 18 April 2012 23:06
0digg
Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli
Waandishi wetu
WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli jana aliugua ghafla akiwa kwenye Viwanja vya Bunge, Dodoma na kupelekwa katika Hospitali ya Mkoa ambako alilazwa.Taarifa za Dk Magufuli kuugua ghafla mbali na kuthibitishwa na Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Dk Zainab Chaula pia zilitangazwa bungeni na Naibu Spika, Job Ndugai.
Akitoa maelezo hayo muda mfupi baada ya kuanza kwa Kikao cha Bunge, Ndugai alisema Waziri Magufuli akiwa katika maandalizi ya kwenda bungeni, alijisikia vibaya ghafla na alipokimbizwa hospitali ilibainika kuwa alikuwa akikabiliwa na tatizo la shinikizo la damu.
“Waheshimiwa wabunge, Mheshimiwa Magufuli aliugua ghafla leo (jana) asubuhi na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma lakini, tunaelezwa kuwa presha (shinikizo la damu) iliyokuwa inamsumbua sasa imeshuka na kinachoendelea kumsumbua sasa ni vichomi ambavyo bado vimembana,’’ alisema Ndugai na kuongeza:
“Madaktari wanaendelea kushughulikia afya yake ili iweze kuimarika sawasawa kwa hiyo msiwe na shaka juu ya afya yake.’’
Wandishi wa habari na hata baadhi ya wabunge hakuruhusiwa kumwona Dk Magufuli hospitalini hapo na muuguzi wa zamu alisema: “Haiwezekani kumuona. Yupo katika eneo ambalo haturuhusu watu kufika na kumuona lakini anaendelea vizuri.’
Dk Chaula alisema Dk Magufuli amelazwa katika chumba maalumu ili kuwawezesha madaktari kuangalia afya yake kwa karibu… “Siyo kwamba yuko mahututi, bali tumemuweka huko kwa makusudi ya kuwa karibu naye zaidi na utulivu mzuri katika chumba hicho.”
Baadhi ya viongozi akiwamo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah walifika hospitalini hapo kwa nyakati tofauti kumjua hali waziri huyo.
Wakati Naibu Spika Ndugai akiwa hakueleza Magufuli aliugua akiwa katika eneo lipi, taarifa kutoka kwa baadhi ya watumishi wa bunge, zilieleza kuwa alipatwa na tatizo hilo asubuhi akiwa viwanja vya bunge.
Hii ni mara ya pili wabunge kuugua ghafla katika Mkutano huo wa Saba wa Bunge baada ya Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Clara Mwatuka kuugua wiki iliyopita na kupelekwa kwenye hospitali hiyo ambako alilazwa kwa siku mbili.
Mtemvu apata ajali
Katika hatua nyingine, Ndugai aliwatangazia wabunge kuwa Mbunge wa Temeke (CCM), Abbas Mtemvu alipata ajali ya gari mkoani Morogoro na kupatiwa huduma ya kwanza kabla ya kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
“Napenda kuwatangazia kuwa mheshimiwa Mtemvu amepata ajali leo (jana) saa 12:15 asubuhi maeneo ya Morogoro baada ya gari lake kupinduka,” alisema Ndugai na kuongeza kuwa gari la Mtemvu lilikuwa likiendeshwa na Hussein Ally (30).
Kamanda wa Polisi Mkoani wa Morogoro, Adolphina Chialo alisema ajali hiyo ilitokea baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka eneo la Gairo, Barabara ya Morogoro- Dodoma saa 11:00 alfajiri wakati mbunge huyo akitokea bungeni mkoani Dodoma kuelekea Dar es Salaam.
Kamanda Chialo alisema gari hilo liliacha njia na kugonga ukuta wa nyumba iliyokuwa jirani na barabara hiyo. Hata hivyo, hakuna mtu aliyejeruhiwa katika nyumba hiyo mbali ya kusababisha uharibifu.
Alisema ajali hiyo ilisababishwa na utelezi kutokana mvua iliyokuwa ikinyesha na dereva huyo kufunga breki kwa nguvu na hivyo kusababisha gari hilo kuacha njia na kupinduka.
Katika hatua nyingine, raia wa Rwanda amefariki dunia papo hapo katika eneo la Dumila, Barabara ya Morogoro- Dodoma baada ya gari alilokuwa akiendesha kugonga kwa nyuma gari jingine.
Kamanda Chialo alisema ajali hiyo ilitokea jana saa 10:30 afajiri na kumtaja marehemu kuwa ni Bigabilo Golam (78) ambaye alikuwa akitokea Dar es Salaam akielekea Kigali, nchini Rwanda.

HABARI ZA VITUKO

 HABARI ZA VITUKO

 

MFUNGWA AVAA GAUNI KUTOROKA

Heels
Viatu virefu sio jambo la mchezo
Mfungwa mmoja wa kiume nchini Brazil aliyekuwa akijaribu kutoroka gerezani kwa kuvaa nguo za kike amekamatwa tena na kurejeshwa ndani.
Bwana huyo Ronaldo Silva alinyoa nywele zake za mikononi na miguuni na kutoka kupitia lango kuu la gereza akiwa amevaa gauni la bluu, wigi kicwhani na viatu virefu.
Hata hivyo bwana huyo ambaye amefungwa kwa makosa ya uuzaji dawa za kulevya, alishtukiwa na polisi mmoja aliyeona akitembea tofauti na wanawake wengine mitaani.
Polisi wamesema nguo hizo aliletewa gerezani na mke wake. Mbali na kuvalia gauni hilo na viatu virefu Ronaldo pia alikuwa amepaka rangi ya mdomo-- lipstik nyekundu iliyokolea.
Polisi walimkamata dakika thelathini tu baada ya kufanikiwa kutoroka gerezani kutokana na kushindwa kutembea vyema na high heels. Mkurugenzi wa gereza hilo Carlos Welber amesema mke wake amekiri kumletea mume wake nguo za kike, lakini amesema hakufahamu kwa nini mume huyo alizitaka.
Mfungwa huyo alikuwa ndio kwanza tu amehamishiwa katika gereza hilo, baada ya kufanya jaribio la kutoroka katika gereza alilofungiwa awali.

MNYONYESHAJI ASIYEJULIKANA

Milk
Mama kwa mshangao...
Mama mmoja nchini Marekani alipatwa na mshituko baada ya kukuta mtoto wake mchanga akinyonyeshwa ndani ya nyumba yake na mwanamke asiyemfahamu.
Kituo cha radio cha KJJQ cha South Dakota kimesema mama huyo alipatwa na mshangao huo saa kumi na moja alfajiri alipokuta kichanga chake cha miezi miwili kikinyonyeshwa na mwanamama asiyefahamika.
Mama huyo alipiga simu mara moja polisi kuripoti suala hilo.
Aidha mama huyo alimchukua mwanaye, lakini mwanamama aliyekuwa akimyonyesha aliendelea kubaki ndani ya nyumba hiyo, hadi polisi walipowasili na kumkamata.
Jitihada za waandishi wa habari kutafa kufahamu zaidi kilichotokea ziligonga mwamba baada ya polisi wa kituo cha Brookings kutopokea simu, umeripoti mtandao wa Huffington Post.
Hata hivyo taarifa zinasema mwanamke mwenye umri wa miaka ishirini na nne ameshtakiwa kwa kosa la kuingia katika nyumba isiyo yake kinyume cha sheria. Pia majina ya wakinamama hao na hata kichanga hayakuweza kupatikana mara moja.

MLEGEZO WAMPELEKA JELA

Sag
Mlegezo wampeleka jela siku tatu
Kijana mmoja mwenye umri wa miaka ishirni nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela kwa siku tatu kwa kuvaa suruali yake chini ya kiuno, yaani mlegezo.
Jaji katika mahakama mjini Alabama alitoa adhabu hiyo kwa kijana aliyekuwa amevaa suruali aina ya jeans kwa misingi ya kukiuka maadili ya mahakama.
Kijana huyo LaMarcus D Ramsey alikuwa amefikishwa katika mahakama ya Autagua kwa kosa la kufanya wizi, limeripoti gazeti la Montgomery Advertiser.
Taarifa zinasema wakati kesi yake ikisikilizwa jaji John Bush alionekana kutatizwa sana na jinsi kijana huyo alivyokuwa amevaa suruali yake, na mara moja alitoa ari kijana huyo kupelekwa jela kwa siku tatu kwa kosa la kuvaa suruali mlegezo, au sag.
"Unadhalilisha mahakama kwa kuonesha makalio yako" amesema jaji huyo. Hali kadhalika jaji huyo amesema mbali na kukaa jela kwa siku tatu, akitoka, kijana huyo ametakiwa kununua suruali inayomtosha, au anunue mkanda, ili nguo yake ya ndani na makalio yake visionekane.

MFUNGWA AMN'GATA AFISA MAGEREZA

Jela
Kasheshe gerezani
Mfungwa mmoja wa kike nchini Marekani anakabiliwa na mashtaka zaidi, baada ya kumngata afisa wa magereza, siku ya jumatatu hadi meno yake mawili kun'gooka.
Mfungwa huyo Erin Babich, alikuwa akitumikia kifungo katika gereza la Manatee, karibu kilomita hamsini kusini mwa Tampa, Florida. Mtandao wa Big Pond News umesema mtafaruku ulianza baada ya Bi Babich kugoma kusikiliza mari za gereza na kujaribu kumpiga afisa mmoja wa gereza.
Wakati akifanya fujo hizo, maafisa wengine wa magereza walijitokeza kusadia, na ndipo alipoamua kumgnata mmoja wao mkononi kwa nguvu mno kiasi kwamba meno yake mawili yalingooka.
Bi Babich sasa ameshtakiwa kwa kosa la kumshambulia afisa wa magereza. Afisa aliyengatwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya mji huo.

POLISI ASIYEJUA KUTUMIA BUNDUKI

Gun
Shabaha sifuri
Mkuu wa Polisi wa mji mmoja nchini Marekani amepigwa marufuku kubeba bunduki kwa sababu hawezi kulenga shabaha inavyotakiwa.
Mtandao wa Huff Post umesema mkuu huyo Thomas Bennett amepunguziwa majukumu yake ya upolisi baada ya kufeli mtihani wake wa kulenga shabaha hivi karibuni.
Hatua hiyo inamaanisha polisi huyo haruhusiwi kuwasha taa za kimulimuli za gari ya polisi (SIRENS) na pia hata kusimamisha magari ya raia kwa ajili ya ukaguzi wa kawaida wa barabarani.
Hata hivyo Polisi Bennett mwenyewe amedai kuwa bado nana uwezo wa kutekeleza majukumu yake kama kawaida. Afisa mtendaji wa mji huo wa North Carolina Gregg Whitehead amesema bwana Bennett ametakiwa kujiandaa kufanya majaribio mengine tena ya kulenga shabaha kama inayotakiwa kipolisi.
Na kwa taarifa yako......Kuna takriban nywele mia tano hamsini katika kila nyusi za binaadam.
Tukutane wiki ijayo..... panapo majaaliwa...

Ufisadi wa mabilioni kila kona

Ufisadi wa mabilioni kila kona  Send to a friend
Wednesday, 18 April 2012 23:10
0digg
Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo
NI KWENYE MAGARI YA SERIKALI,TANESCO,MALIASILI,MABILIONI YA JK,AFYA NA MISHAHARA HEWA
Daniel Mjema Dodoma na Fidelis Butahe
WABUNGE jana waliijia juu Serikali kwa matumizi mabaya ya fedha za umma na ufisadi ulijitokeza kwenye taasisi zake mbalimbali katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, mwaka jana.

Hasira za wabunge hao zilitokana na ripoti tatu za Kamati za Bunge; Mashirika ya Umma (POAC), Serikali za Mitaa (LAAC) na Hesabu za Serikali Kuu (PAC) kuonyesha upotevu wa mabilioni ya shilingi yaliyotumika katika nyanja mbalimbali ikiwemo mishahara hewa na mikataba mibovu.

Mbunge wa Longido (CCM), Michael Laizer alisema ni aibu kila mwaka kuwa na ripoti za wizi wa mali za umma lakini Serikali inakaa kimya.

Alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido, mmoja wa maofisa wake aliidhinisha Sh11 milioni kwa ajili ya matengenezo ya gari. “Labda Serikali imechoka sasa inafanya makusudi fedha za wananchi zinaliwa lakini yenyewe inakaa kimya. Serikali itujibu hizi fedha zinazopitishwa kila mwaka zinakwenda wapi?” alihoji Laizer

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Magdalena Sakaya alisema Serikali inapaswa kuona aibu kwa kutekeleza pendekezo moja tu kati ya 12 yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Alihoji suala la mishahara hewa kuendelea kujitokeza huku Serikali ikikaa kimya na kila mwaka CAG anatoa ripoti yake… “Kuna vitabu vya halmashauri za wilaya ambavyo CAG hakuvikagua kwa kuwa havikuonekana vilipo, sasa hapo tunakwenda wapi? Kuna Sh8 bilioni hazikufika katika halmashauri husika zimekwenda wapi? Wabunge tunatakiwa kuhoji na kupewa majibu sahihi.”

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari alisema sasa Tanzania imekuwa kama Saccos kwa kuwa fedha za umma zinatafunwa bila utaratibu huku vielelezo vikitoweka kusikojulikana.

“Wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, mawaziri walijaa bungeni ila sasa tunajadili hatima ya Watanzania hawaonekani. Wabunge tuwe kitu kimoja tuibane Serikali itueleze hizi fedha zimekwenda wapi?” alisema Nassari.

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya alisema chama tawala kisipokuwa makini katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kitahukumiwa na vijana.

“Serikali ndiyo chanzo cha fedha kutafunwa… inakuwaje Naibu Waziri wa Maji anasimama na kuahidi mambo mengi wakati anajua wazi kuwa fedha za kutekeleza miradi hazipo?” alihoji.

Alisema mwaka 2015, utakuwa mgumu kwa CCM kwa kuwa wakati huo vijana watakuwa asilimia 85 na wanaweza kukinyima kura kutokana na Serikali yake kushindwa kusimamia masuala ya msingi ya maendeleo.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee aliwataka wabunge kuacha kulalamika kwa kuwa wao ndiyo wenye rungu la kuishikisha adabu Serikali: “Tukilalamika wananchi waliotuchagua nao watatushangaa kwa kuwa wametutuma kuwawakilisha na si kulalamika.”

Alisema umefikia wakati wa wabunge kuweka itikadi za vyama vyao pembeni na kuwashughulikia mawaziri wa wizara husika ambazo zinaonekana kuwa tatizo.

Mbunge wa Mwibara (CCM), Alphaxard Lugola alimlipua Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo akisema alihusika katika uuzaji wa mali ya Serikali katika Kiwanja namba 10 Barabara ya Nyerere na kwamba anaingilia utendaji wa mashirika ya Serikali.

Alisema kuwa kiwanja hicho awali, ilikuwa kiuzwe kwa Shirika la Tanzania Motors chini ya Kampuni ya Mashirika Hodhi ya Umma (CHC) kwa Sh1.3 bilioni lakini baadaye Mkurugenzi Mkuu wa CHC alipewa barua kusitisha uuzwaji wa jengo hilo na kumtaka kuitisha mazungumzo upya na Morad Sadik, ambaye alikuwa akitaka kununua eneo hilo awali.

“Inakuwaje wizara inaingia utendaji wa taasisi au kampuni zilizopo chini yake?” alihoji.

Awali, baada ya Kipindi cha Maswali na Majibu, Wenyeviti wa Kamati hizo za Bunge; Zitto Kabwe (POAC), John Cheyo (PAC) na Augustine Mrema (LAAC), waliwasilisha ripoti za kamati zao zinazoonyesha kukithiri kwa vitendo vya ufisadi serikalini na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kamati ya PAC
Cheyo alisema kamati yake imebaini kuwapo kwa matumizi ambayo hayakupitishwa na Bunge na kutaja Maonyesho ya Sabasaba, Nanenane na Utumishi kama sehemu ambako fedha hizo zilitumika.

Alisema mwaka 2009/2010 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ilitumia fedha za matumizi ya jumla ya Sh1.10 bilioni kwa ajili ya Maonyesho ya Nanenane ambazo hazikuwamo kwenye bajeti iliyopitishwa na Bunge.

Alisema hata matumizi ya Sh21.63 bilioni zilizotumika kuendesha Mfuko wa Kukwamua Wananchi kiuchumi maarufu kama ‘mabilioni ya JK’ hazikuwapo katika bajeti iliyopitishwa na Bunge. Alipendekeza kuwa ili kuondoa hali hiyo, mfuko huo unatakiwa kuwa na mtu au taasisi ya kuusimamia badala ya kuachwa bila usimamizi.

Alisema kuwepo kwa udanganyifu na ukwepaji kodi kumeisababishia Serikali hasara ya Sh15.4 bilioni na Dola 2.6 milioni za Marekani.

Alisema Wizara ya Maliasili na Utalii na ilipoteza Sh874,853,564 baada ya kufanya uamuzi wa upendeleo wa kutoa kiwango cha chini cha mrabaha kwa mazao ya misitu.
 
Kuhusu magari ya Serikali, Cheyo alisema kumekuwa na matumizi yasiyo ya lazima katika uendeshaji na ukarabati wa magari hayo. Hadi Juni 30, 2010 Serikali ilikuwa inamiliki magari yenye thamani ya Sh5 trilioni.

Alisema mwendelezo wa ununuzi wa magari unaofanywa na Serikali unaongeza gharama za uendeshaji na kusisitiza kwamba matumizi hayo si ya lazima kwa Serikali yenye uchumi mdogo uliozidiwa na madeni.

Kuhusu ukaguzi wa magari uliofanywa na wakala chini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), PAC imependekeza kuwajibishwa kwa ofisa masuuli wa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kuisababishia Serikali hasara ya Dola 18,343,540 za Marekani ambazo ni karibu Sh30 bilioni na kusisitiza: “Sh30 bilioni zilitumika kufanyia ukaguzi wa magari ambao haukuwepo.”

Alisema pia wamegundua kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kukodi majengo ya wizara na kusisitiza kuwa moja inaweza kulipa kodi ya Sh485 milioni.

Alisema kuna watumishi hewa takriban 3,000 na kwamba Serikali haifahamu lolote kuhusu hali hiyo… “Kuna Sh1.8 bilioni ambazo hutumiwa na Serikali kwa ajili ya kulipa watumishi hewa. Pia imebainika kuwa Serikali haijui thamani ya majengo yake yaliyopo ndani na nje ya nchi.”

POAC

Zitto kwa upande wake, alielezea maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi ya fedha ambayo yanahusisha ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake.

Alitola mfano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambalo kwa mwaka mmoja wa fedha linafanya ununuzi wenye thamani ya kati ya Sh300 bilioni hadi Sh600 bilioni.

Alisema kwa mwaka wa fedha 2009/2010, Tanesco  ililitumia Sh1.8 bilioni ukilinganisha na Sh65 milioni zilizokuwa zimepangwa katika bajeti ya ukarabati wa gati mojawapo katika Kituo cha Bwawa la Mtera.

“Ongezeko hilo la gharama za ununuzi kwa ajili ya ukarabati, ni kiasi kikubwa na Kamati haikuridhika na majibu ya menejimenti hivyo kuagiza uchunguzi wa ndani ili kubaini uhalisia wa ununuzi huo,”alisema na kuongeza:

“Tumependekeza Tanesco ianze kutumia vyanzo vyake vya umeme na iache kununua umeme hasa wa kampuni ya IPTL kwani inatumia Sh62.4 kununua umeme katika kampuni hii kwa mwaka.”
 
Alisema Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa (MUCE) kilishindwa kuthibitisha kwa wakaguzi wa hesabu uwepo wa vifaa vya maabara vilivyonunuliwa ambavyo vina thamani ya Sh267 millioni.

Katika ripoti hiyo, Zitto alisema imebainika pia mkataba kati ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), na Kampuni ya Startimes unatakiwa kupitiwa upya ili uinufaishe TBC.

Pia aliugusia matumizi mabaya ya fedha katika Bodi ya Pamba ambako alisema kuwa kiasi cha Sh2 bilioni zilizotolewa na Serikali hazijulikani zilipo na wala hazikuwafikia wakulima wa zao hilo.

LAAC

Kwa upande wake, Mrema aliitaka Serikali ivunje mtandao wa wezi wa mali za umma na kuhoji inakuwaje inawakumbatia mafisadi?
Alihoji majalada ya watuhumiwa wa ufisadi kukaa zaidi ya miaka 10 katika Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) na ile ya Makosa ya Jinai (DCI) wakati kesi za uchaguzi zimewekewa kikomo.

Alisema ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2010, inaonyesha kuwa Sh583.2 milioni zililipwa kama mishahara hewa kiasi ambacho alisema kingetosha kujenga madarasa 194.

Mrema alisema katika ripoti hiyo, imebainika kwamba Sh8 bilioni zilitumika katika ununuzi usiokuwa na nyaraka na ama wenye nyaraka pungufu hali inayoashiria kuwapo kwa wizi.

Aliwataja watumishi wa Halmashauri ya Kishapu akisema ni vinara wa ubadhirifu wa Sh6 bilioni na kudai kuwa walishirikiana na baadhi ya watumishi wa Benki ya NMB Tawi la Manonga, Shinyanga kuiba fedha hizo za umma.

Aliwataja watumishi hao kuwa ni Mweka Hazina, Muhdin Mohamed, Mtunza Fedha wa Halmashauri hiyo, Walugu Mussa, Boniface Nkumiming na Mhandisi wa Halmashauri, Leonard Mashamba.

Alisema fedha hizo zilitafunwa kwa kutumia nyaraka feki, uhamisho wa fedha bila idhini na kuzitumia kinyume cha malengo, uhamisho wa fedha ambao haukufika kwenye akaunti husika na malipo kwa walipaji wasiofahamika.

Mrema aliilaumu Serikali kwa kuwahamisha kutoka halmashauri moja kwenda nyingine na Serikali Kuu, watumishi wanaotuhumiwa kwa ufisadi badala ya kuwachukulia hatua za kisheria.

Kamati hiyo imependekeza Bunge likubali kuitaka Serikali kutoa maelezo ya kuridhisha ni kwa nini ubadhirifu huo umeachwa ukishamiri kwa miaka mitatu mfululizo bila wahusika waliotajwa na CAG kuchukuliwa hatua.

“Shida iliyopo hapa ni Serikali kuonekana inawakumbatia wahusika kwa kisingizio cha uchunguzi unaendelea… nini kinachochunguzwa badala ya kupeleka watu mahakamani na kumuita CAG kama shahidi?”

HABARI MBALIMBALI

  HABARI MBALIMBALI

 

Uchaguzi G. Bissau kuchelewa

Watawala wa kijeshi wamesema uchaguzi wa urais utafanyika baada ya miaka miwili

Breivik alipanga kulipua mabomu matatu

Ameseme alipanga kushambulia makao makuu ya serikali, ofisi za chama cha Labour na kasri la familia ya kifalme.

Mafundi wa Force India watoroka

Washambuliwa Bahrain

Mpango wa amani Syria waporomoka

BBCSwahili.com | Mwanzo - 2 hours ago
Mpango huo anashurutisha majeshi ya serikali kuondoka kwenye maeneo ya makaazi

Kanda ya ubakaji yazua ghadhabu A. Kusini

BBCSwahili.com | Mwanzo - 2 hours ago
Watu nchini humo wameelezea hisia kali baada ya kusambazwa kwa kanda ya video ikionyesha msichana akibakwa

MANCHESTER UNITED WAENDELEA KUONGOZA KWA UTAJIRI DUNIANI KWA MWAKA WA 8 MFULULIZO - YAZIFUNIKA REAL NA BARCA.

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
* * *Manchester United wametajwa tena kama timu ya soka tajiri zaidi duniani - wakitajwa kuwana thamani ya £1.39billion.* * * *Mabingwa hao wa Uingereza wamekaa kileleni mwa listi ya jarida la kimarekani la Forbes kwa miaka 8 mfululizo kufuatia mwaka mwingine wa mafanikio chini ya Sir Alex Ferguson.* * * *Majirani zao Manchester City wenyewe pamoja na matanuzi yote ya Fedha hawajaweza hata kuingia Top 10 - wakishika nafasi ya 13.* * * *Timu nyingine ya kiingereza iliyofuata nyayo za United ni Arsenal waliopo nafasi ya nne, wakifuatiwa na Chelsea katika nafasi ya saba, Liverpool w... more »

BARCELONA YAENDELEZA UTEJA KWA CHELSEA - DROGBA AWADUNGA KAMOJA TU

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 6 hours ago
Chelsea 1-0 Barcelona *by goalsarena2012-3*

BAADA YA RUFAA YAO KUTUPWA - YANGA WATAFAKARI CHA KUFANYA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 6 hours ago
*SIKU moja baada ya kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutupilia mbali rufaa ya timu ya Yanga kupinga kupokwa pointi tatu na mabao matatu, uongozi wa klabu hiyo umesema bado unatafakari cha kufanya. * *Kamati ya nidhamu chini Mwenyekiti wake kamishna mstaafu wa Polisi Alfred Tibaigana iliyokutana juzi ilitupilia mbali rufani hiyo ya Yanga iliyowasilishwa na Yanga ikilalamikia kamati ya kamati ya Ligi kuipoka pointi hizo na mabao matatu baada ya kumchezesha beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ambaye alikuwa akitumikia adhabu ya kukosa mechi tatu. * *Ofisa habari wa Y... more »

MATUKIO YA PICHA UWANJA WA KAITABA YANGA NA KAGERA SUGAR

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 7 hours ago
anaitwa sajid shabiki wa kagera sugar. Abdulraz Majid mtangazaji kasibante fm radio Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Fabian Masawe ndiye alikua mgeni rasmi pembeni ni Athmani Chama katibu wa chama cha soka mkoa Mwamedi Hussen msemaji wa kagera sadik galiatano kushoto, enock na kulia ni mc baraka wa bukobawadau.

Kapteni ana mimba

BBCSwahili.com | Mwanzo - 10 hours ago
Bi Faye White atajufungua Oktoba

Chelsea 1 Barcelona 0

BBCSwahili.com | Mwanzo - 16 hours ago
Yakaribia fainali ya klabu bingwa

Bashir,"Nitawakomboa raia wa S.Sudan"

BBCSwahili.com | Mwanzo - 19 hours ago
Rais Bashir anasema atawakomboa raia wa Sudan Kusini kutoka kwa utawala wake. Anaongeza kwamba hakuna tena mipaka ya nchi hizo

Kombe la Olimpiki lauzwa

BBCSwahili.com | Mwanzo - 19 hours ago
Kombe la fedha limeuzwa katika mnada kwa takriban dolla laki tisa

SIMBA YAZIDI KUCHANUA MAKUCHA NA KUTAMBA KILELENI - YANGA YAPIGWA TENA HUKO KAGERA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 21 hours ago
*Simba imendelea kujiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania baada ya kuichapa JKT Ruvu kwa mabao 3-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa. * * Kwa matokeo hayo, Simba imejiweka katika nafasi nzuri ya kunyakua ubingwa huo baada ya kujikita zaidi kileleni mwa ligi hiyo kwa kufikisha pointi 56 ikiwazidi, pointi 13 mabingwa watetezi, Yanga. Simba ilianza kwa kasi mchezo na kufanikiwa kupata bao la kwanza katika dakika ya kwanza ya mchezo lililofungwa na Uhuru Selemani kwa kichwa baada ya kuunganisha kona iliyopigwa na Emnuel Okwi.* * Simba wal... more »

Nyaraka za ukoloni zatolewa Uingereza

BBCSwahili.com | Mwanzo - 22 hours ago
Nyaraka zinaonyesha harakati za Mau Mau nchini Kenya

LEO NI MIAKA 5 TANGU MESSI ALIPOMLIPA MARADONA.

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 23 hours ago
miaka mitano iliyopita siku kama ya leo Leo Messi alifunga moja kati ya mabao yake bora katika maisha yake ya kucheza soka.ilikua ni kwenye mchezo wa nusu fainali ya kombe ya mfalme ugenini dhidi ya Getafe. Maradona vs England kwenye robo fainali ya kombe la dunia mnamo mwaka 1986.

REAL MADRID NDIO ILIYOPIGA MASHUTI MENGI YALIYOLENGA GOLI KWENYE LA LIGA NA CHAMPIONS LEAGUE.

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 23 hours ago
*Kikosi cha Jose Mourinho kimepiga mashuti mengi langoni mwa wapinzani kuliko timu yoyote katika la liga na Champions league, wana wastani wa 8.1 na 8.5 kwa mechi katika kila michuano hiyo. Real wamepiga mashuti 270 yaliyo lenga langoni mwa wapinzani katika mechi 33 msimu huu katika La Liga, kuliko Barcelona, Atletico Madrid na Sevilla. Mechi ambazo walipiga mashuti mengi yaliyolenga lango msimu ni dhidi ya Zaragoza (17), ikifuatiwa na mechi dhidi ya Granada walipiga mashuti 12.* *SHOTS ON GOAL IN LA LIGA* *TEAM* *TOTAL SHOTS* *PER MATCH* *Real Madrid* *270* *8.1* Barcelona 25... more »

OFFICIAL: RUFAA YA YANGA YAPIGWA CHINI !

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 23 hours ago
Cannavaro KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Aprili 17 mwaka huu) imetupa rufani ya Yanga iliyowasilishwa mbele yake kupinga uamuzi wa kupokwa pointi tatu kwa kumchezesha mchezaji asiyestahili. Aprili 2 mwaka huu Kamati ya Ligi ya TFF iliipa Coastal Union ushindi wa pointi tatu na mabao matatu baada ya Yanga kumchezesha beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya timu hizo iliyofanyika Machi 31 mwaka huu wakati akiwa na adhabu ya kukosa mechi tatu. Yanga katika rufani hiyo iliwasilisha sababu nan... more »

Nyaraka za Ukoloni kutolewa

Mwaka uliopita serikali ya Uingereza iliwasilisha hoja mahakamani kupinga kutolewa kwa nyaraka hizo za siri.

Wednesday, April 4, 2012

ANC yamfungia Malema kuwaongoza vijana


ANC yamfungia Malema kuwaongoza vijana

 4 Aprili, 2012 - Saa 18:21 GMT
Chama tawala nchini Afrika kusini, kimemtimua rais wa tawi la chama hicho la vijana,Julius Malema kutoka wadhifa wake katika chama hicho mara moja.
Kamati ya nidhamu ya chama hicho, pia imempiga marufuku Malema kuhudhuria mikutano ya chama hicho baada ya Malema kusema utawala wa rais Jacob Zuma, ni wa kidikteta.
Bwana Malema alitimuliwa kutoka ANC tangu mwezi Februari mwaka huu, lakini hadi leo aliendelea kushikilia wadhifa wa rais wa mrengo wa vijana na kuruhusiwa kuhudhuria mikutano, akisubiri kusikizwa kwa kesi yake ya rufaa baadaye mwezi huu.

Al-Qaeeda yanyemelea vijana Uingereza

Al-Qaeeda yanyemelea vijana Uingereza

 4 Aprili, 2012 - Saa 09:36 GMT
Wanamgambo wa Taleban
Vijana waingereza wenye asili ya kiafrika, huenda wakawekwa kasumba na Al-qaeeda wakati kundi hilo likitafuta kukita mizizi barani Afrika.
Taarifa hii imetolewa na kundi la wataalamu wa maswala ya dunia wanaosema kuwa Al-qaeeda inatafuta kuweza kujikwamua kutokana na vita dhidi ya kundi hilo.
Kulingana na wataalamu, hali kama hiyo inaweza kusabisha changamoto kubwa kwa Uingereza pamoja na mashirika mengine ya kijasusi katika chi za magharibi.
wanaonya kuwa vijana walio katika tishio la kushinikizwa zaidi kimawazo kwa kufunzwa siasa kali ni wenye asili ya kisomali pamoja na wengine kutoka nchi za Afrika mashariki na Magharibi.
Serikali ya Uingereza imesema kuwa inakabiliana na tisho la ugaidi ndani ya nchi hiyo
Katika miaka kumi na tano iliyopita vijana kutoka Pakistan, wale wenye asili ya kiafrika, na hata wahindi wanaoishi nchini humo, wameweza kushinikizwa na kufunzwa siasa kali kulingana na ripoti iliyochapishwa na taasisi ya Royal United Service
 4 Aprili, 2012 - Saa 09:36 GMT
Wanamgambo wa Taleban
Vijana waingereza wenye asili ya kiafrika, huenda wakawekwa kasumba na Al-qaeeda wakati kundi hilo likitafuta kukita mizizi barani Afrika.
Taarifa hii imetolewa na kundi la wataalamu wa maswala ya dunia wanaosema kuwa Al-qaeeda inatafuta kuweza kujikwamua kutokana na vita dhidi ya kundi hilo.
Kulingana na wataalamu, hali kama hiyo inaweza kusabisha changamoto kubwa kwa Uingereza pamoja na mashirika mengine ya kijasusi katika chi za magharibi.
wanaonya kuwa vijana walio katika tishio la kushinikizwa zaidi kimawazo kwa kufunzwa siasa kali ni wenye asili ya kisomali pamoja na wengine kutoka nchi za Afrika mashariki na Magharibi.
Serikali ya Uingereza imesema kuwa inakabiliana na tisho la ugaidi ndani ya nchi hiyo
Katika miaka kumi na tano iliyopita vijana kutoka Pakistan, wale wenye asili ya kiafrika, na hata wahindi wanaoishi nchini humo, wameweza kushinikizwa na kufunzwa siasa kali kulingana na ripoti iliyochapishwa na taasisi ya Royal United Service

Rais wa Mali kushtakiwa kwa uhaini

Rais wa Mali kushtakiwa kwa uhaini

 4 Aprili, 2012 - Saa 09:21 GMT
Majeshi yaliyopindua serikali Mali
Watawala wa kijeshi wanapanga kumfungulia mashtaka ya uhaini rais waliyempindua. Kiongozi wa Mapinduzi Kapten Amadou Sanogo amesema pamoja na mashtaka mengine, Amadou Toumani Toure anakabiliwa na ubadhirifu wa fedha za umma.
Haya yanajiri wakati watawala wa kijeshi wametangaza kuanza kongamano la kitaifa kujadili mustakabali wa Mali. Nchi hiyo ambayo haina bandari imewekewa vikwazo vya kiuchumi na jamii ya kimataifa.
Wanajeshi wa daraja ya chini waliipindua serikali kutokana na kile walisema mikakati duni ya kukabiliana na waasi kaskazini mwa nchi. Tangu mapinduzi hayo , nao waasi wameendelea kuyateka maeneo mengi kaskazini mwa Mali ukiwemo mji wa Timbuktu ambao una hifadhi maalum za kitamaduni.
Waasi hao wamegawanyika makundi mawili ambapo lile la MNLA linapigania kuwepo taifa huru la Azawad. Kundi nyingine Ansar Dine lenye uhusiano na mtandao wa Al-Qaeda linataka kusalia Mali lakini chini ya sheria ya Kiisilamu.
Rais Amadou Toumani Toure alitarajiwa kuondoka madarakani baada ya kumaliza muhula wake wa pili baadaye mwezi huu.Wakati huo huo Waasi hao wa Kaskazini wameendelea kusonga hatua mbele kusini mwa Mali.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kutoa taarifa kuhusu mzozo wa Mali baadaye Jumatano wiki hii.
 4 Aprili, 2012 - Saa 09:21 GMT
Majeshi yaliyopindua serikali Mali
Watawala wa kijeshi wanapanga kumfungulia mashtaka ya uhaini rais waliyempindua. Kiongozi wa Mapinduzi Kapten Amadou Sanogo amesema pamoja na mashtaka mengine, Amadou Toumani Toure anakabiliwa na ubadhirifu wa fedha za umma.
Haya yanajiri wakati watawala wa kijeshi wametangaza kuanza kongamano la kitaifa kujadili mustakabali wa Mali. Nchi hiyo ambayo haina bandari imewekewa vikwazo vya kiuchumi na jamii ya kimataifa.
Wanajeshi wa daraja ya chini waliipindua serikali kutokana na kile walisema mikakati duni ya kukabiliana na waasi kaskazini mwa nchi. Tangu mapinduzi hayo , nao waasi wameendelea kuyateka maeneo mengi kaskazini mwa Mali ukiwemo mji wa Timbuktu ambao una hifadhi maalum za kitamaduni.
Waasi hao wamegawanyika makundi mawili ambapo lile la MNLA linapigania kuwepo taifa huru la Azawad. Kundi nyingine Ansar Dine lenye uhusiano na mtandao wa Al-Qaeda linataka kusalia Mali lakini chini ya sheria ya Kiisilamu.
Rais Amadou Toumani Toure alitarajiwa kuondoka madarakani baada ya kumaliza muhula wake wa pili baadaye mwezi huu.Wakati huo huo Waasi hao wa Kaskazini wameendelea kusonga hatua mbele kusini mwa Mali.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kutoa taarifa kuhusu mzozo wa Mali baadaye Jumatano wiki hii.

Mengi yaibuka ushindi wa Chadema Arumeru

Mengi yaibuka ushindi wa Chadema Arumeru  Send to a friend
Tuesday, 03 April 2012 21:46
0digg
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiwahutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Leganga, juzi ambapo Mbunge Mteule wa Jimbo la Arumeru Mashariki (Chadema), Jushua Nassari alifanya mkutano huo kuwashukuru kwa kumteua. Picha na Edwin Mjwahuzi
SIOI SUMARI ALITOSWA NA VIGOGO WA CCM MKOA, WILAYA, WAFUASI 61 WA CHADEMA WATIWA MBARONI, WADAIWA KUVUNJA KIOO GARI LA KAMANDA WA POLISI
Waandishi wetu, Arumeru, Dar
MAMBO mengi zaidi yamezidi kuibuka kuhusu uchaguzi wa Arumeru Mashariki uliomalizika juzi, baada ya taarifa kusema kuwa aliyekuwa mgombea CCM, Sioi Sumari alitelekezwa na viongozi wa chama hicho Wilaya ya Arumeru na Mkoa wa Arusha wanaodaiwa hakuwa chaguo lao wakati wa kura za maoni.

Wakati Sioi akidaiwa kutelekezwa, shamrashamra za Chadema kusherehekea ushindi wa mgombea wao, Joshua Nassari juzi ziliingia dosari baada ya wafuasi wake 61 kutiwa mbaroni kwa tuhuma za kufanya vurugu na kuvunja kioo cha gari la Mkuu wa Operesheji wa jeshi hilo, Isaya Mngulu.

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina gazetini, mmoja wa wajumbe wa timu ya kampeni za Sioi anayetoka wilayani Arumeru alisema mfano dhahiri wa kutengwa kwa mgombea huyo ni siku ya kupigakura ambako hakuna kiongozi yeyote aliyehangaika kuzunguka vituoni kukagua.

Alisema hali ilikuwa mbaya zaidi ilipofika wakati wa kukusanya masanduku ya kura na matokeo kutoka vituoni kabla majumuisho yaliyofanyika katika ofisi ya mji mdogo wa USA-River, ambako hakukuwa na kiongozi yeyote aliyejitokeza kusimamia wala kushuhudia majumuisho hayo.

“Huwezi kuamini kuwa hakukuwa na kiongozi wala mwakilishi yeyote wa CCM kwenye chumba cha majumuisho ya kura hadi ilipofika Saa 7:00 usiku, ndipo mgombea mwenyewe alipoamua kwenda kushuhudia na kusimamia kura zake,” alisema mjumbe huyo ambaye ni kiongozi wa ngazi ya mkoa.

Mwandishi wa habari hizi aliyekesha kwenye kituo hicho cha majumuisho alimshuhudia Sioi akifika eneo hilo akiwa ameongozana na Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa vijana wa CCM (UVCCM), Benno Malisa pamoja na makada wengine watatu ambao hata hivyo, waliondoka baada ya dakika 40 na kumwacha mgombea huyo peke yake.

Sioi aliyekuwa akiwania kurithi kiti cha ubunge kilichokuwa kikishikiliwa na marehemu baba yake, Jeremia Sumari, alibaki ukumbini hapo akiwa ameketi viti vya nyuma hadi alipoondoka ukumbini Saa 10:30 alfajiri, huku mwenzake, Joshua Nassari wa Chadema waliyekuwa wakichuana vikali akiwa ameketi mbele akiwa amezungukwa na kundi kubwa la viongozi wa kitaifa na mawakala wake.

Nje ya ukumbi wa majumuisho, pia walikuwepo viongozi kadhaa wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe waliokuwa wameweka kambi hapo na kukesha hadi matokeo yalipotangazwa kesho yake Saa 12:30 asubuhi.

Mbali ya Mbowe, baadhi ya viongozi wengine wa Chadema walikuwapo ni Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Mbunge wa Mbozi Mashariki, David Silinde na Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), John Heche.

Licha ya kususwa na kutelekezwa kwenye mchakato wa majumuisho ya kura, inadaiwa kuwa Sioi pia hakupewa fedha za kutosha na chama chake kwa ajili ya kampeni kwani hadi zinamalizika, CCM ilikuwa imetoa milioni 60 pekee tofauti na ilivyofanya kwa wagombea wengine kwenye chaguzi ndogo ambako chama hicho hubeba gharama zote.

“Mpaka usiku wa kuamkia Ijumaa, chama kilikuwa kimetoa milioni 60 pekee kwa kampeni nzima, fedha ambazo hazikutosha hata kulipa mawakala 327 na wale wa akiba ambao kila mmoja tulipanga alipwe Sh30,000. Yaani kama vile chama kilijitenga na kampeni za Sioi,” alisema na kulalamika kiongozi mwingine aliyeongoza kampeni za mgombea huyo.

Kiongozi huyo ambaye kama mwenzake alizungumza kwa sharti la kutotajwa akiogopa ‘kushughulikiwa’ alisema  gharama za kampeni za mgombea huyo wa CCM zilikuwa zaidi Sh200 milioni ambazo zilitokana na michango binafsi za wanafamilia na marafiki.

Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda alipoulizwa kuhusu madai hayo, alikataa kusema lolote akisisitiza kwamba hayo ni mambo ya ndani ya chama yanayostahili kuzungumzwa na kujadiliwa ndani ya vikao.

“Hao waliokuletea taarifa hizo siyo tu kwamba wanakwenda kinyume cha katiba na kanuni za CCM, bali pia wanatoa siri za ndani nje ya chama. Sisi tunatarajia kukutana kufanya tathmini ya uchaguzi huo na yale yanayostahili kuwekwa hadharani tutawaeleza na yanayofaa kufanyiwa kazi ndani ya chama pia tutafanya hivyo kwa maslahi na maendeleo ya chama chetu,” alisema Chatanda.

Sioi akubali yaishe
Kwa upande wake, Sioi jana alitangaza kuyakubali matokeo hayo na kuahidi kumpa ushirikiano wa dhati mbunge mteule atakapomhitaji.

Sumari alishindwa kwenye uchaguzi wa ubunge baada ya kupata kura 26,757 ambazo ni sawa na asilimia 44.56 huku Nassari akipata kura 33,972 sawa na asilimia 54.91.

Sioi ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kukipongeza Chadema kwa kuibuka kidedea katika uchaguzi huo huku akikitaka kihakikishe kinatimiza ahadi kilizozitoa kwa wakazi wa jimbo hilo.

Sioi alisema kwamba amekubaliana na matokeo yaliyotangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo,Trasias Kagenzi juzi alfajiri. Alisema ameridhishwa na matokeo hayo na kamwe hatarajii kwenda mahakanani kuyapinga.

Sioi aliwaomba wakazi wa Arumeru Mashariki kumpa ushirikiano wa kutosha mbunge mteule wa jimbo hilo huku akisisitiza ya kwamba hata yeye yuko tayari kufanya hivyo.

Pia alimtaka Nassari kutimiza ahadi zote alizokuwa akizitoa kwa wakazi wa jimbo hio wakati wa kampeni hasa za maji, elimu na miundombinu.

Shamrashamra
Wakati hali ndani ya CCM ikiwa hivyo, vijana 53 wa Chadema walikamatwa na kuachiwa huru baadaye na polisi juzi usiku wakati wakisherehekea ushindi wa Nassari.

Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri wa Chadema, John Mrema alisema vijana hao, wameachiwa kwa dhamana kutokana na maombi ya mbunge huyo mteule kwa polisi.

“Kama ambavyo mbunge aliahidi kuwa asingeweza kuendelea na sherehe za ushindi bila vijana walioshikwa, tunafuraha kuwaeleza kuwa vijana 53 wameachiwa bado vijana saba ndiyo tunawashughulikia,” alisema Mrema.

Vijana hao, walikamatwa na polisi katika operesheni kubwa iliyofanyika juzi usiku ikihusisha matumizi ya mabomu baada ya vijana hao kuandamana bila utaratibu na pia kudaiwa kuvunja vioo vya magari.

Polisi limeeleza kuwa vijana hao walikamatwa kwa kosa la kuvunja vioo vya magari likiwemo la Mngulu aliyekuwa mkuu wa operesheni wa polisi katika uchaguzi huo.

Tendwa asifu

Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania, John Tendwa amesifia ukomavu wa kisiasa uliojitokeza katika chaguzi ndogo za ubunge na udiwani zilizofanyika Aprili Mosi, mwaka huu jlicha ya kujitokeza kwa upungufu mwingi.

“Ukomavu wa kidemokrasia umejitokeza japo mapungufu ni mengi sana yaliyojitokeza pamoja na kuwapo kwa tume ambayo ilijaribu lakini hawakusitisha, sikuweza kuingilia maamuzi yale, kama kutoleana maneno machafu na kejeli  ni jambo ambalo linaweza kuleta madhara makubwa, uvumilivu wa kisiasa unahitajika,’’ alisema Tendwa.

Alikipongeza CCM kwa kuonyesha ukomavu wake wa kisiasa na Chadema kwa kushinda jimbo hilo na kuvitaka kwa vyama vyote vya siasa nchini kutekeleza kanuni na taratibu zote wakati wa uchaguzi ili kuboresha demokrasia ya nchi.

Maafisa wa michezo wauawa Somalia

Maafisa wa michezo wauawa Somalia

 4 Aprili, 2012 - Saa 18:45 GMT
jumba la tamthilia Somalia
Wajumbe wa Kamati ya Olimpiki ya Somalia na viongozi wa chama cha kandanda cha Somalia ni miongoni mwa watu saba waliouwawa katika shambulio la bomu mjini Mogadishu.
Waziri Mkuu Abdiweli Mohamed Ali pia alikuwepo wakati wa mlipuko huo katika jumba la maonyesho ya tamthilia lililofunguliwa upya hivi karibuni lakini aliiambia BBC kwamba hakudhurika.
Wanaharakati wa kundi la al-Shabab wanasema ndio waliotekeleza shambulio hilo.
Jeshi la kuweka amani la Muungano wa Afrika nchini Somalia limelaani shambulio hilo kua ni kitendo "kinachokirihisha" na kusema hakitavuruga juhudi za amani.
Rais wa Kamati ya Olimpiki ya Somalia , Aden Yabarow Wiish, na mkuu wa shirikisho la kandanda nchini Somalia , Said Mohamed Nur, nao pia waliuwawa. Walikua ni miongoni mwa kikundi cha wageni mashuhuri waliokusanyika kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa kituo cha televisheni ya taifa ya Somalia.
Rais wa shirikisho la kandanda la kimataifa FIFA ,Sepp Blatter, alisema ameshtushwa sana kwa vifo vya maafisa hao wa michezo.
Waandishi habari watatu wa kituo cha televisheni cha Somalia nao pia walijeruhiwa kwa mujibu wa rubaa zilizoiarifu idhaa ya Kisomali ya BBC.
Jumba hilo la tamthilia lilifungwa katika miaka ya mwanzo ya 1990 wakati Somalia ilipotumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe na lilifunguliwa upya mwezi mmoja tu uliopita wakati wa awamu mpya ya matumaini ya kurejea amani.
Waziri mkuu Abdiweli alisema mwanamke aliyejitoa mhanga ndie aliyefanya shambulio hilo.
Akilaani kundi la al-Shabab, alisema ni kawaida yao "kuwaua watu wasio na hatia ".
Salah Jimale,aliyeshuhudia shambulio hilo ameliambia shirika la habari la Associated Press " Mlipuko huo ulitokea wakati wapiga muziki walikua wakiimba huku wakishangiliwa na watazamaji.
"Moshi mweusi ulitanda kila mahali. Watu walipiga mayowe na wanajeshi ghafla wakaanza kufyatua risasi katika lango la kuingia ndani."
Waandishi wa habari waliokuwepo hapo wanasema watu kadhaa walijeruhiwa na wanaelezea kuona viatu na simu za mkononi vilivyojaa damu,na viti kulipuliwa vipande vipande na mlipuko huo.
Katika taarifa yake kundi la al-Shabab limesema ndilo liliohusika na shambulio hilo lakini limezungumzia bomu lililotegwa badala ya mshambuliaji wa kujitoa mhanga.
Msemaji wa Al-Shabab Sheikh Abdiasis Abu Musab ameliambia shirika la habari la Reuters "sisi ndio tuliopanga mlipuko katika jumba la tamthilia. Tuliwalenga mawaziri na wabunge makafiri na ndio miongoni mwa maafa ya leo."
Wanaharakati hao walitimliwa kutoka Mogadishu na wanajeshi wa Muungano wa Afrika mnamo mwaka jana.
Tangu wakati huo kumekuwepo na kipindi cha utulivu kiasi ambapo shughuli za michezo zilianza upya,mikahawa kufunguliwa pamoja na jumla la taifa la tamthilia.
Lakini al-Shabab imeendelea kushambulia mji mkuu kwa mabomu na makombora. .
Wakati huo huo,mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika mzozo wa Somalia, Augustine Mahiga ameelezea kukerwa kwake na shambulio hilo katika Jumba la Tamthilia la Kitaifa.

HABARI MBALIMBALI

Matayrisho ya Olimpiki mbioni

BBCSwahili.com | Mwanzo - 10 minutes ago
Kila kitu tayari kwa ufunguzi rasmi

Barca yatinga nusu fainali.

BBCSwahili.com | Mwanzo - 41 minutes ago
Lionel Messi alifunga penalti mbili katika kipindi cha kwanza na kusaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya AC Milan

"Chelsea bado jogoo" - Di Matteo

BBCSwahili.com | Mwanzo - 41 minutes ago
Kaimu kocha wa Chelsea, Roberto Di Matteo anaamini klabu hiyo bado ina sifa katika nyanja ya kimataifa

REAL MADRID VS APOEL: MOURINHO HAJAWAHI KUFUNGWA ROBO FAINALI YA CHAMPIONS LEAGUE

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
*MOURINHO IN UCL QUARTERFINALS* *Season* *Team* *Opponent* *Scores* 2003/04 Porto O. Lyonnais Porto 2-0 O. Lyonnais; O. Lyonnais 2-2 Porto 2004/05 Chelsea Bayern Munchen Chelsea 4-2 Bayern Munchen; Bayern Munchen 3-2 Chelsea 2006/07 Chelsea Valencia Chelsea 1-1 Valencia; Valencia 1-2 Chelsea 2009/10 Inter Milan CSKA Moscow Inter Milan 1-0 CSKA; CSKA 0-1 Inter Milan *2010/11* *Real Madrid* *Tottenham* *Real Madrid 4-0 Tottenham; Tottenham 0-1 Real Madrid*

GARETH BALE - NILIKATAA KUJIUNGA NA MANCHESTER UNITED NIKAENDA SPURS

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
*Gareth Bale amefichua siri kwamba alikataa kujiunga na Manchester United kabla ya kuchagua kwenda Spurs. Winga huyo wa kimataifa wa Wales alipewa ofa ya kuhamia Old Trafford na Boss United Sir Alex Ferguson alipokuwa na miaka 17 akiichezea Southampton. Lakini kinda hilo alichagua kwenda Tottenham baada ya kuhakikishiwa nafasi katika kikosi cha kwanza, hivyo akaamua kumtosa Fergie. Bale, 22, alisema: "Man United walikuwa wakinitaka lakini mimi nilikuwa nataka nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza. Hivyo niliona mahala pa ukweli ambapo ningepata nafasi hiyo ni Spurs. "Kocha w... more »

MECHI ZOTE AMBAZO MESSI AMEFUNGA KATIKA CHAMPIONS LEAGUE - BARCELONA HAIJAFUNGWA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
*Leo Messi alifunga goli lake la 51 katika ligi ya mabingwa wa ulaya jana jumanne. Mpaka sasa amefunga magoli 14 katika msimu huu wa ligi ya mabingwa. Muargentina huyo sasa yupo nyuma ya goli moja tu kuweza kuwa mchezaji aliyefunga magoli mengi katika msimu mmoja wa Champions league. Messi sasa anashika nafasi ya tatu katika listi ya wafungaji bora wa muda wote wa champions league, akiwa mbele ya Thierry Henry, na nyuma ya Raul aliyefunga magoli 71 na Van Nisterlrooy aliyefunga 56. MESSI AKIFUNGA BARCA HAWAFUNGWI Messi amefunga katika mechi 32 katika champions league, kati ya mechi... more »

PHOTOS: SIMBA ILIPOWASILI MJINI SETIF - ALGERIA - YAFIKIA HOTEL YA ZINEDINE ZIDANE

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
*Kocha wa Simba Milovan akiwa na daktari wa simba.* *Hotel waliyofikia Simba hapa Setif inayoitwa jina la mwanasoka bora wa dunia wa zamani Zinedine Zidane ambaye ana asili ya Algeria* *Victor Costa Jumba akiwa na mmoja ya viongozi wa msafara huo* *Bwana Salum Machaku akiwa anashangaa shngaa watoto wa kiarabu.* *Emmanuel Okwi na Uhuru Suleiman* *Ally Mustapha Barthez akiwa na Amiri Maftaa na Felix Sunzu leo walipowasili mjini Setif -Algeria*

SIMBA WASTUKIA HUJUMA YA ES SETIF - WAYAKATAA MAJI WALIYOPEWA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
*Aden Rage akikagua maji hayo kabla ya kuyakataa. Maji hayo yaliletwa na viongozi wa klabu ya ES Set*if. *Rage akisisitiza kutoyataka maji yaliyoletwa na ES Setif kwa kuhofia hujuma dhidi ya waarabu hao.* *Mtanzania ambaye ni daktari Elihuruma alikuwepo kutoa sapoti kwa Simba huko nchini ya Algeria.* *Viongozi wa klabu ya ES Setif wakijadiliana baada ya viongozi wa Simba kugoma kuchukua maji yao waliyoleta.*

Shambulio la kujitoa mhanga Afghanistan

BBCSwahili.com | Mwanzo - 7 hours ago
Mshambuliaji wa kujitoa mhanga amejilipua na kusababisha vifo vya takriban watu kumi mjini Maymana, mji mkuu wa jimbo la Faryab

MSHINDI MPYA WA PROMOSHENI YA Tick Tock APATIKANA!

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 8 hours ago
Mkuu wa Kibiashara Zanzibar Mohammed Mussa akimkabidhi Mshindi wa Milioni 1 wa promosheni mpya ya Zantel iitwayo Tick Tock Suleiman Vuia zawadi yake. Tick Tock ni promosheni mpya kutoka Zantel ambapo mteja akiongeza salio la TSH 1000 na kuendelea anaweza kujishindia milioni 1 pamoja na simu za Nokia zinazotolewa kila saa.

MAMA TUNU PINDA APOKEA MICHANGO YA TWIGA STARS.

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 8 hours ago
*MKE WA WAZIRI MKUU Mama Tunu Pinda leo amepokea michango kutoka kwa wadau mbalimbali jijini Dar es Salaam ikiwa ni mwitikio wa ombi lake kwa Watanzania kuwaomba waichangie timu ya Taifa ya Netiboli (Taifa Queens) ili iweze kushiriki Mashindano ya Kombe la Afrika mwezi ujao.* * * *Mama Tunu Pinda amepokea simu ya mtandao wa Zantel namba 0779-000-808 ambayo imeunganishwa na huduma ya EZY-PESA. Simu hiyo ambayo imekabidhiwa kwa uongozi wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) inawawezesha Watanzania kutuma pesa kwenye namba hii kutoka mitandao yote ya simu. * *Meneja Mawasiliano w... more »

MKANGANYIKO KATIKA LIGI KUU YA MKOA WA TANGA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 8 hours ago
*Jumla ya timu 14 ambazo zinatakiwa kushiriki ligi ya mkoa ambayo ilipangwa katika makundi matatu Timu zilizogawanywa katika makundi matatu na kundi lililokuwa na matatizo lilikuwa na timu ya Small Prison, African Sports , Segera FC , Air Shooting na Lushoto Shooting. Timu ya Segera FC ndio ilionekana ni dhaifu katika kundi hilo ambapo mchezo wake wa kwanza ilifungwa mabao 2 kwa 1, mchezo wa pili walicheza dhidi ya Air Shooting wakafungwa mabao 4 kwa 1 na katika mchezo wa tatu dhidi ya Small Prisons ikafungwa mabao 5 kwa 1. Mchezo uliokuja kuleta kasheshe ni baina ya African Sports ... more »

Maafisa wa michezo wauawa Somalia

BBCSwahili.com | Mwanzo - 8 hours ago
Wajumbe wa Kamati ya Olimpiki ya Somalia na viongozi wa chama cha kandanda cha Somalia ni miongoni mwa watu saba waliouwawa

Maelf waandamana Mauritania

BBCSwahili.com | Mwanzo - 9 hours ago
Wafanya maandamano katika mji mkuu Nouakchott,wakimtaka Rais Mohamed Ould Abdelaziz kuondoka madarakani.

Rais wa Mali kushtakiwa kwa uhaini

BBCSwahili.com | Mwanzo - 9 hours ago
Watawala wa kijeshi wanapanga kumfungulia mashtaka ya uhaini rais waliyempindua, Amadou Toumani Toure

Al-Qaeeda yanyemelea vijana Uingereza

BBCSwahili.com | Mwanzo - 9 hours ago
Vijana waingereza wenye asili ya kiafrika, huenda wakawekwa kasumba na Al-qaeeda wakati kundi hilo likitafuta kukita mizizi Afrika

KOCHA WA ES SETIF - SIMBA WASUBIRI KIPIGO CHA AJABU.

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 17 hours ago
*Kocha wa ES Setif, Alain Geiger ametambia kurejea uwanjani kwa wachezaji wake watatu ambao walikosekana wakati timu hiyo ilipofungwa mabao 2-0 na Simba Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Simba iliifunga ES Setif katika mchezo wa kwanza raundi ya kwanza Machi 25 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika michuano ya Kombe la Shirikisho. * * Wachezaji hao ni Abdelmoumen Djabou, Bengoreine Gourmi na Delhoum, ambao pia aliwatumia kwenye mchezo baada ya kuifunga CRB Ain Oussera kwa mabao 3-1, kwenye robo fainali ya mchezo wa Kombe la Algeria na kutinga nusu fainali mwishoni mwa wik... more »

HATIMAYE SAMUEL ETO'O AFUTA KESI YA MADAI DHIDI YA BARCELONA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 17 hours ago
* Straika wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto'o ameamua kufuta kesi yake ya madai ya mabilioni ya shilingi dhidi ya klabu yake ya zamani, Barcelona. Eto'o alikuwa akiida klabu hiyo wakati akihama kwenda Inter Milan ya Italia. Katika madai yake, Eto'o alitaka kulipwa kiasi cha Dola za Kimarekani 3.9milioni kama sehemu ya makubaliano alipohama na kwenda kujiunga na Inter katika msimu wa mwaka 2009. "Barcelona ingependa kutoa taarifa ya kumshukuru Samuel Eto'o kwa dhamira yake ya kumaliza suala lililokuwa mbele yetu," ilisema taarifa ya klabu hiyo jana jioni. "Yeye (Samuel) alikuw... more »

Tuesday, April 3, 2012

Syria ina hadi Aprili 10 kuweka amani


Syria ina hadi Aprili 10 kuweka amani

 2 Aprili, 2012 - Saa 18:49 GMT
Mapigano yameendelea mjini Homs
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa nchi za kiarabu Koffi Annan amelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuweka Aprili 10 kama siku ya mwisho kwa Syria kutekeleza mpango wake wa amani.
Kwenye kikao cha faragha kwa Baraza hilo, Bw Annan alisema sharti mapigano yasitishwe katika saa 48 baada ya siku hiyo.
Balozi wa Syria katika Umoja wa Mataifa amethibitisha kwamba serikali yake imeridhia kutekeleza mpango huo kabla ya siku ya mwisho.Aidha balozi huyo Bashar Al Jaafari amesema sharti upinzani pia umalize mashambulizi yote.
Mapigano yameendelea nchini Syria licha ya ahadi ya Rais Bashar al Assad kuitikia mpango wa amani uliopendekezwa na Koffi Annan wiki moja iliyopita.Wakati huo huo Mkuu wa Shirika la Msalaba Mwekundu ,Jakob Kellenberger anafanya ziara nchini Syria kutaka wapewe idhini ya kuwahudumia wafungwa na kusambaza misaada ya dharura.
Taarifa ya shirika hilo imesema Bw Kellenberger atajaribu kuomba kusitishwa mapigano kwa saa mbili kila siku ili kuwaondoa majeruhi na kutoa misaada ya kibinadamu.