Saturday, March 10, 2012

Madaktari warudi kazini Tanzania

Madaktari warudi kazini Tanzania

 10 Machi, 2012 - Saa 16:57 GMT
Chama cha Madaktari nchini Tanzania kimetangaza kuwa wanachama wake wanarudi makazini, baada ya kikao cha jana, ambapo viongozi wa madaktari waliokuwa wamegoma walikutana na Rais Jakaya Kikwete ikulu, mjini Dar-es-laam.
Rais Jakaya Kikwete amekutana na madaktari waliogoma
Madaktari hao wanasema Rais ameonyesha nia ya dhati katika kutatua mgomo huo pamoja na madai yao mengine , lakini hawana imani na maafisa wakuu katika wizara ya afya nchini humo.
Dr Ulimboka Steven ni Mwenyekiti wa kamati ya Jumuia ya madaktari hao waliokuwa wakigoma na alitoa sababu za kumaliza mgomo:
"Baada ya kujadili kwa kina mapendekezo ya mheshimiwa rais kuhusiana na njia za kutatua mgogoro huu, madaktari kwa umoja wao wametoa heshima kubwa kwa mheshimiwa rais, na kwamba kuanzia muda huu baada ya kikao, wanarejea kazini.
Lakini kitu kikubwa tunapenda tukiweke wazi ni kuwa waziri wa afya na naibu wake bado ni tatizo kwa madktari.
Hatuna imani nao na hatuko tayari kufanya nao kazi.
Na madaktari wamemvua waziri uanachama wa chama cha madaktari wa Tanzania na siyo mwenzetu tena.

No comments:

Post a Comment