Friday, March 30, 2012

Matokeo ya kura Ubungo yalikuwa na kasoro adai msimamizi

Matokeo ya kura Ubungo yalikuwa na kasoro adai msimamizi  Send to a friend
Thursday, 29 March 2012 21:05
James Magai
ALIYEKUWA Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi katika Jimbo la Ubungo, katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 amekiri kuwa kulikuwa na upungufu katika matokeo ya jumla ya jimbo hilo na kwamba dosari hakustahili  kusaini wala kuyatangaza matokeo.

Msimamizi huyo msaidizi, Gaudence Kadiarara, pia  alikiri kuwa Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, aliingiza kompyuta zake ndogo katika chumba cha kuhesabia kura na kwamba walilalazimika kuachana na mfumo wa Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa kuwa ulikuwa unachelewesha matokeo.

Kadiara ambaye pia ni Ofisa Maendeleo na Ustawi wa Jamii katika Manispaa ya Kinondoni, alikuwa akitoa ushahidi katika kesi ya  kupinga matokeo ya uchaguzi  katika jimbo hilo.

Kesi hiyo ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi Mnyika,  imefunguliwa na aliyekuwa mgombea mwenzake kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, Hawa Ng’humbi.
Katika kesi hiyo inayosikilizwa Jaji Upendo Msuya, Ng’humbi anadai kuwapo kwa ukiukwaji mkubwa wa taratibu na sheria ya uchaguzi.

Katika ushahidi wake, Ng’humbi na mashahidi wake pia wanadai kuwepo kwa dosari katika matokeo kwa madai kuwa fomu ya matokeo ya jumla iliyopokewa na mahakama ina kura hewa 14,854, ambazo hazijulikanai zilikotoka.
Pia wanadai kuwa Mnyika alipeleka kompyuta zake katika chumba cha kujumlishia kura na kwamba aliingia na wafusi wake zaidi ya wanane katika chumba hicho, jambo ambalo ni  kinyume cha sharia.

Wanadai kuwa kwa pamoja, watu hao walimshinikiza aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Rajabu Kiravu, aruhusu kutumia kompyuta hizo katika kujumlishia kura, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Akihojiwa na wakili wa upande wa madai, Issa Maige jana, shahidhi alikiri kuwa takwimu zinazoonekana katika fomu o ya matokeo si sahihi na kwamba

kwa mujibu wa matokeo, kura halisi zilikuwa ni 119823, kura halali zilikuwa ni 117,639 huku kura zilizokataliwa (zilizoharibika) zikiwa ni 2184.

Alidai kuwa Ng’humbi alipata jumla ya kura 5,0544 na Mnyika kura 66,742 na wagombea wengine 14 walipata kura 15,207 kwa pamoja akiwamo mgombea wa CUF, Julius Mtatiro, aliyepata kura 12,964.
Kwa fomu hiyo jumla ya kura za Ng’humbi na za Mnyika tu ni 117,286 karibu sawa na kura halali bila kujumlisha za wagombea wengine.
Awali akiongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali kutoa ushahidi wake, shahidi huyo wa kwanza wa upande wa wadaiwa, alikiri kuwapo kwa upungufu katika fomu hiyo ya matokeo.

 “Tatizo hapa ni kwamba kura halisi ni pungufu ya kura walizopata wagombea wote, kwa hiyo hili ni kosa. Nikiziangalia kwa harakaharaka hizi kura halisi (zinazooneshwa kwenye fomu hizo) ni za vyama vya CCM na Chadema tu,” alidai shahidi huyo.
 Alidai kuwa katika kujumlisha, walishughulika zaidi na kura za wagombea wa CCM  na Chadema kwa kuwa ndivyo vyama ambavyo vilikuwa vikijirudiarudia kila mara katika kura.
Alipoulizwa na Jaji Msuya kuhusu kura za vyama vingine kutokujumlishwa, shahidi huyo alijibu, “ndilo kosa lililofanyika,” .

Akijibu swali la Wakili wa Serikali juu ya  kura za vyama vingine kutohesabiwa, alijibu kuwa ni tatizo la kibinadamu na kwamba kura zao zote zipo.

Shahidi huyo alilazimika kufanya mahesabu upya, ili kujibu swali la Jaji Msuya aliyetaka kujua idadi ya kura za wagombea wa vyama vyote.

Baada kufanya hivyo, alijibu kuwa kura halali zilipaswa kuwa 132,496, badala ya 117,639 zinazoonekana kwenye fomu  na kwamba kura halisi zilipaswa kuwa 134,680 badala ya  119,823.

Sehemu ya mahojiano baina ya shahidi huyo na Wakili Maige ilikuwa kama ifauatvyo:
Wakili Maige: Shahidi nani alijaza fomu hiyo (namba 24B ya matokeo ya jumla ya ubunge).

Shahidi: Ni msimamizi msaidizi mwenzangu Sioni.
Wakili: Mli-cross check accurancy ya recording mlizoziweka katika fomu hiyo?
Shahidi: Ndio
Wakili: Kwa hiyo dosari hizo mlizijua tangu mwanzo na ninyi ni sehemu ya dosari hizo?

Shahidi: Hatukuzifahamu kabla, tungezifahamu tungeweza kuzirekebisha.
Wakili: Kwa jinsi hiyo fomu ilivyo, msimamizi angebaini kuwa kuna kura hewa zaidi ya 14,000 katika 24B angesaini?
Shahidi: Asingesaini.

Wakili: Asingesaini kwa sababu matokeo yaliyorekodiwa si halali na sahihi, kweli si kweli?
Shahidi: Kimya

Jaji Msuya: Kwa hiyo asingesaini kwa sababu hayako sawa sawa?
Shahidi: Ndio mheshimiwa jaji.
Akizungumzia jukumu lake katika chumba cha kujumlishia kura, shahidi huyo alidai kuwa lilikuwa ni kusoma  matokeo kutoka kwenye fomu za matokeo ya vituoni na kumwezesha  karani kuyaingiza kwenye kompyuta na kujumlisha.

Akizungumzia madai ya Mnyika kupeleka kompyuta zake tano  kuhesabia kura, alikiri kuwa alipigiwa simu akiwa nje kuwa Mnyika alipeleka  kompyuta zake na kwamba hata hivyo alipofika ofisini hawakuzitumia.

Alidai kuwa kompyuta hizo zilitumiwa na Mnyika na kwamba wao walitumia kompyuta (laptop).
Shahidi huyo aliendelea kudai kuwa wakiwa katika chumba cha majumuisho Mnyika alimweleza msimamizi msaidizi wa Uchaguzi Lambaert Kyaro kuwa watumie kompyuta zake kwa katika kujumlisha kura kwa kuwa kompyuta za Tume ya Uchaguzi(NEC) zilikuwa zinachelewesha kiasi kwamba wangeweza utumia hata siku 15.


Shahidi huyo aliendelea kudai kuwa alimfuata Kiravu na kupinga matumizi ya kompyuta za Mnyika lakini wale wafausi wa Chadema waliendelea kumzongazonga wakimfuata kila mahali wakimshinikiza akubali kutumia kompyuta za Mnyika hadi Kiravu akakubali.

Wafuasi Chadema watawanywa kwa Mabomu Songea

Wafuasi Chadema watawanywa kwa Mabomu Songea  Send to a friend
Thursday, 29 March 2012 21:06
0digg
Boniface Meena, Songea
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma juzi jioni lilirushia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakiandamana kutokea katika mkutano wa hadhara wa kampeni za udiwani kuelekea katika ofisi za mkoa za chama hicho baada ya kumsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe.

Msafara wa wafuasi hao wa Chadema ambao walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za chama hicho walipita karibu na mkutano wa CCM uliokuwa ukihutubiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi ndipo polisi walikuwa katika eneo hilo waliwatawanya kwa kutumia mabomu ya machozi.

Hatua hiyo ya polisi kupiga mabomu ya kutoa machozi ilisababisha wafuasi hao kukimbia kila kona kutafuta mahali pa kujificha ili kujiokoa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma,  Michael Kamhanda alipoulizwa kuhusu tukio hilo alisema; "Sina taarifa."

Akizungumzia tukio hilo, Zitto alisema aliwashangaa polisi hao kuwatawanya wanachama hao kwa kuwapiga mabomu ya kutoa machozi na kuwashauri kuwa wasome alama za nyakati wanaposhughulikia masuala ya raia.

Alisema ni kawaida kwa wanachama wa Chadema mjini Songea kuandamana baada ya mkutano hadi katika ofisi za chama kuagana, hivyo polisi walipaswa kuelewa hilo na kutokuamua kutumia nguvu.

Awali, akihutubia katika mkutano huo wa Lizaboni, Songea katika kampeni wa uchaguzi mdogo wa udiwani unaotarajiwa kufanyika  Aprili mosi, mwaka huu aliwaambia wakazi wa Songea kuwa atahakikisha wafanyakazi wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) ambao wamekuwa na tabia ya kuiba mafuta ya jenereta za kuzalishia umeme wanachukuliwa hatua za kisheria haraka iwezekanavyo, ili kuondoa tatizo la umeme linaloukabili mji wa Songea na viunga vyake.

Zitto alisema akiwa Mwenyekiti Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), atashughulikia tatizo hilo kwa kufanya mambo mawili ambayo ni kuwahoji kwa nini umeme ukatike hovyo Songea na matumizi ya mafuta yanatumikaje ambayo yanalalamikiwa kuisha mara kwa mara.

“Hili halina mjadala wakija na kuwahoji kwa kuwa wanaripoti kwangu mtiti (mgogoro) wake mtauona. Nimeweza kumshughulikia mkurugenzi wa Tanesco, hivyo kwa Songea itakuwa ni kitu kidogo kwangu,” alisema Zitto.

Katika kuondoa tatizo la umeme katika mkoa wa Ruvuma, alisema ujenzi wa mitambo mikubwa ya kuzalisha umeme kwa makaa ya mawe inajengwa Mbinga yenye uwezo wakuzalisha megawati 120 na mji wa Songea utapata kilovoti 220 na kulifanya tatizo hilo kuwa ndoto na kwamba mkoa wa Ruvuma utaunganishwa na gridi ya taifa kutoka Makambako, mkoani Njombe.

Zitto alimsihi Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma (RPC), akitaka wasimamie haki na kuacha mpango wao unaodai kuwa mgombea udiwani wa kata ya Lizaboni kwa tiketi ya chama hicho ana tuhuma zinazomkabili tangu mwaka 1988.

“Chadema imeinasa barua waliyoandikiana wakuu hao wa Jeshi la Polisi. Tunataka kujua inakuwaje tuhuma hizo zifumbiwe macho tangu mwaka 1988 zije kuibuliwa sasa. Muda wote huo walikuwa wapi, wakati mgombea alikuwa kiongozi wa mtaa kwa vipindi viwili?,” alihoji Zitto.

Alisema katika barua hiyo, diwani huyo anaundiwa zengwe linaloonesha kuwa yeye alikuwa anachochea waendesha pikipiki waandamane na kuleta fujo katika kipindi cha mauaji yaliyotokea miezi michache iliyopita mjini hapa.

Zitto amelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina wa mauaji yaliyotokea na si kutishia raia na kwamba, ili kukomesha tabia hiyo ya polisi, ameahidi kupeleka barua hiyo bungeni.

Aliongeza kwamba jeshi la polisi lina mpango wa kuleta polisi wengine kutoka nje ya mkoa wa Ruvuma siku ya uchaguzi ili kuwadhibiti wananchi wa Lizaboni washindwe kupiga kura siku ya uchaguzi, kwakuwa kwa sasa polisi wa Songea wengi ni Chadema.

Akiwa Mbeya

Juzi, Zitto alisababisha kuvunjika kwa Soko la wilaya ya Rungwe baada ya kufanya maandamano makubwa kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara kumnadi mgombea udiwani wa kata hiyo  uliofanyika Kiwira Madukani.

Zitto alifanya maandamano hayo ambayo yalihudhuriwa na mmia ya wananchi wa Kiwira kuanzia saa 9:30 na wakati wakipita katika soko hilo, wafanyabiashara waliokuwa wakichuuza katika soko hilo waliacha biashara zao na kuhamia eneo la mkutano huku wakiimba wimbo wa Chadema wa 'Presha inapanda, presha inashuka'.

VIJANA WA CHADEMA WAMZINGIRA , AHOJIWA NA POLISI

Waziri matatani Arumeru  Send to a friend
Thursday, 29 March 2012 23:04
0digg
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye (kushoto) akimnadi mgombea wa ubunge wa chama hicho katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari (katikati) kwenye mkutano uliofanyika katika kijiji cha Ambureni jana. Picha na Edwin Mjwahuzi.
VIJANA WA CHADEMA WAMZINGIRA , AHOJIWA NA POLISI
Waandishi Wetu, Arumeru
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodlucky Ole Medeye juzi usiku aliingia matatani baada ya kutiwa msukosuko na vijana wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wakimtuhumu kujihusisha na utoaji rushwa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge zinazoendelea Jimbo la Arumeru Mashariki.

Tukio hilo, lilitokea kati ya saa 12:30 jioni na saa 1.20 usiku eneo la Kata ya Mbuguni wilayani Arumeru, pale Naibu Waziri huyo alipokurupushwa na vijana hao, kisha kukimbilia Shule ya Msingi Oldevesi, kabla ya kuokolewa na polisi.

Taarifa kwamba Medeye amekamatwa, zilisambaa kwa kasi hali iliyosababisha watu kadhaa kwenda Kituo cha Polisi Usa River kupata taarifa kamili za tukio hilo, lakini ilifahamika kuwa, Naibu waziri huyo hakufikishwa polisi baada ya kutolewa Mbuguni.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye akizungumza na Mwananchi kwa simu jana, alisema walipata taarifa kutoka kwa vijana hao juzi kwamba Naibu Waziri huyo alikuwa anafanya kampeni eneo la Shambarai.

Gazeti hili lilipomtafuta Naibu waziri huyo kupata ukweli wa tukio hilo,  alikiri kukumbwa na mkasa huo, lakini alikanusha madai kwamba alikuwa akigawa fedha kwa lengo la kukisaidia Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Hata hivyo, habari kutoka Mbuguni zilizolifikia Mwananchi, zilidai kuwa Medeye ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Magharibi, alikutwa na mkasa huo alipokuwa kwenye mazungumzo na mmoja wa wamiliki wa mashamba makubwa katika eneo hilo, mwenye asili ya kiasia (jina tunalihifadhi), pamoja na wanawake kadhaa ambao ni wakazi wa kata hiyo.

Baadhi ya vijana wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Chadema, walimzingira Medeye na kuanza kumhoji sababu za kuwepo eneo hilo  na kugawa fedha kwa lengo la kukisaidia CCM huku akitumia gari la Serikali, hali iliyozua tafrani na kusababisha Naibu Waziri huyo kutimua mbio hadi Shule ya Msingi Oldeves.

Wakati wakiendelea kujibizana, mmoja wa vijana hao alimpiga picha Naibu Waziri huyo pamoja na gari hilo lililokuwa na bendera ya taifa, na kwamba kitendo hicho kilimkera kiongozi huyo kiasi cha kutaka kuvunja kamera, hatua iliyochangia kuongeza kwa tafrani hiyo.

“Baada ya hali ya hewa kuchafuka, baadhi ya wakereketwa wa CCM walipiga simu Kituo cha Polisi Mbuguni, askari wakafika mara moja na kuondoka na Medeye hadi Kituo cha Polisi Mbuguni," alidai mmoja kati ya mashuhuda wa tukio hilo.

Ilikuwaje?

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema,  Zanzibar,  Hamid Mussa Yusuph, ambaye alikuwa eneo la tukio, alisema wakiwa katika kazi ya kutangaza mikutano ya chama chao juzi, waliona gari la waziri huyo na walipolisogelea, walimkuta akiwa jirani huku akizungumza na  mkulima huyo mwenye asili na kiasia na baadhi ya akina mama.

"Sisi tulimhoji anafanya nini jioni katika eneo hilo akiwa na gari la Serikali? Akatujibu ana shughuli zake, hapo yakatokea majibizano, ndipo alikimbia kwenda kujihifadhi Shule la Oldevesi," alisema Yusuph.

Alisema kutokana na idadi ya watu kuendelea kuongezeka katika eneo hilo, yeye (Yusuph) aliamua kupiga simu polisi, kuwaarifu na kwamba baada ya muda mfupi, askari walifika na baada ya kumhoji sababu za yeye kuwepo hapo, waliondoka naye.

Yusuph alisema baada ya hapo, waliamua kwenda kutoa taarifa polisi na kufungua faili la uchunguzi ambalo lilipewa namba MNG/RB/81/2012 na baadhi ya wanachama waliokuwepo, waliandika maelezo yao.

Hata hivyo jana Mkuu wa Operesheni wa Polisi katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki, Naibu Kamishna, Isaya Mngulu, alisema hakuna jalada lolote lililofunguliwa kuhusu tukio hilo na wala polisi hawajamshikilia Naibu Waziri huyo.

Baada ya Mngulu kutajiwa namba ya faili la keshi iliyofunguliwa Mbuguni, alisema: “Mimi sina hiyo taarifa bwana, labda kama ndio hivyo mtafute RCO (Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Arusha) akueleze zaidi”.

Aliongeza: "Ninachojua mimi hakuna kesi yoyote ya Naibu Waziri huyo na kama kuna faili limefunguliwa, atafutwe huyo Mkuu wa Upelelezi".

Medeye na RPC Arusha
Medeye kwa upande wake, alisema alikutana na vijana hao, akiwa katika shughuli zake za kiofisi jioni na alishangazwa na uvumi kuwa alikuwa akigawa fedha jambo ambalo ni uongo mkubwa.

"Hawa vijana wa Chadema ni waongo, mimi nilikuwa katika shughuli zangu za kiofisi, ndipo walipokuja nikashtukia wakinizingira na kuanza kunihoji maswali ambayo si ya msingi," alisema Medeye.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Andengenye alisema: "Naomba uandike ninayokueleza, baada ya kupata habari hizo, tuliwasiliana na Waziri ambaye alituambia kwamba yupo kwenye shughuli za Serikali nasi tukamshauri kuwa asitishe shughuli hizo kwa ajili ya muda kwani tayari ilikuwa ni jioni sana.”

Alisema baada ya maelekezo hayo, Naibu Waziri huyo aliondoka, hivyo habari zilizoenea kuwa aliandikishwa maelezo au kufunguliwa jalada, siyo sahihi.

Utekaji washamiri
Wakati huohuo, hali ya amani katika uchaguzi mdogo wa Jimbo  la Arumeru Mashariki sasa ni tata kutokana na kuibuka vitendo vya utekaji wafuasi wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo.

Chadema ndiyo wamelalamikia kutekwa kwa makada wake wawili, Omar Abdul ambaye hadi jana alikuwa hajulikani alipo wakati kada mwingine, Juma Ally (32) amelazwa hospitali baada ya kutekwa na kunyang’anywa gari, kisha kutupwa mtoni baada ya jaribio la kumuua kushindikana.

Kamanda Andengenye amethibitisha matukio yote mawili ambayo yamekuja kipindi ambacho kimegubikwa na vurugu katika mikutano ya kampeni za CCM na Chadema, huku vijana kadhaa wakiripotiwa kujeruhiwa kwa mapanga na wengine kukamatwa na polisi.

Katika tukio la kwanza, Juma ambaye ni mkazi wa Tengeru, juzi alitekwa na watu asiojulikana akiwa na gari lake, kisha kutaka kumuua.  Andengenye alisema tukio hilo lilitokea Machi 27 usiku, wakati watu wanane, walikodi gari la Juma katika eneo la Usar River na kutaka kupelekwa Makumira lakini kabla ya kufika mmoja wao, aliomba kushuka na ghafla watu hao, walianza kumshambulia dereva huyo na kumtupa kwenye korongo.

Alisema wakati watu hao, wakimshambulia, kijana huyo alianza kupiga kelele, ndipo walimvua nguo zote na kuchukua simu na fedha kisha kutoweka na gari hilo aina ya Toyota lenye namba za usajili, T563 BTM.

 Andengenye aliongeza kuwa kutokana na sauti aliyokua akitoa Juma, mpita njia mmoja aliisikia na kumulika tochi kwenye Korongo hilo ndipo alimwona na kuita watu wengine kusaidiana kumtoa kisha kumkimbiza Hospitali ya Wilaya ya Arumeru iliyopo Tengeru akiwa uchi huku amejeruhiwa vibaya.

Hadi jana Juma alikuwa bado amelazwa. Akizungumza kwa taabu na waandishi wa habari, alisema watu hao kabla ya kumteka na kumpora gari, walimuomba awapeleke eneo la Makumira.

Katika tukio lingine, Omar maarufu kama Omar Matelephone, ambaye amekuwa akivalia kanzu iliyoshonwa kwa rangi za bendera ya Chadema, kwa siku nne hadi jana, alikuwa hajulikani alipo ikiwa ni siku mbili tangu alipokwaruzana na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Malisa katika klabu ya ‘Triple A’ baada ya kiongozi huyo wa UVCCM, kumtaka avue mavazi yake ya Chadema.

Tangu Machi 25 Omar alipohudhuria mkutano wa Chadema katika kata ya Songoro, hajaonekana na simu zake zote hazipatikani, pia nyumbani kwake hayupo.

Rafiki wa Omar, Christopha Mbajo alisema jana kuwa yangu  walipoachana naye jioni ya Machi 25, hawajamuona hadi jana na simu zake zote hazipatikani.

“Hatujui yuko wapi ila tunakumbuka mara ya mwisho aligombana na Malisa na baadaye waliombana msamaha, kisha aliitwa na Ofisa Usalama wa Taifa Mkoa wa Arusha, Suleiman Mombo na kuhojiwa juu ya ugomvi huo,”alisema Mbajo.

Akizungumza na Mwananchi jana kwa simu, Malisa alikana kumfahamu Abdul na kueleza kuwa hajawahi kugombana naye katika ukumbi wa ‘Triple A’ uliopo jijini Arusha kama inavyodaiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Meneja Kampeni wa Chadema, Vincent Nyerere, alidai vitendo hivyo vinafanywa na kundi la vijana wa CCM walioletwa kutoka nje ya Arumeru na kwamba polisi wanapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kuwadhibiti

“Tuliwaambia kuna kundi la vijana linakuja na basi la Manko Express toka Musoma na kwamba wawazuie kwani ni vijana wa vurugu, tukawapa na majina yao lakini wameshindwa kuwadhibiti na sasa wanatishia maisha ya watu!”Alilalamika Nyerere.

ran yadaiwa kusaidia Sudan kwa silaha

ran yadaiwa kusaidia Sudan kwa silaha

 21 Machi, 2012 - Saa 12:54 GMT

Maafisa wa Sudan Kusini wamelaumu utawala wa Iran kwa kutoa makombora kwa jirani wake Jamuhuri ya Sudan.
Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini amesema ndege iliyodunguliwa katika jimbo la Kordofan Kusini ilipatikana na mabomu yaliyowekwa alama ya Iran.
Sudan Kusini pia imelaumu Sudan kwa kuendelea kuwasajili wapiganaji wa kijamii katika eneo la mpaka kama jaribio la kujitayarisha kwa mashambulizi.
Serikali ya Sudan imeomba jeshi la kikabila maarufu kama Popular Militia kama hatua ya kuzima maasi ya kundi moja lililoshirikiana na waasi wa SPLA ambao walipata uhuru wa Sudan Kusini Julai mwaka jana.

Waasi Mali watwaa mji wa Kidal


Waasi Mali watwaa mji wa Kidal

 30 Machi, 2012 - Saa 13:23 GMT
Waasi wa Tuareg
Waasi wa Tuareg nchini Mali wameutwaa mji wa Kidal kaskazini mwa Mali,wiki moja tu baada ya wanajeshi kuipindua serikali, wakisema kuwa jeshi linahitaji silaha za kupambana na waasi hao.
Msemaji wa waasi aliambia BBC kuwa wamethibiti mji huo, tamko lililothibitishwa na raia wa eneo hilolo
Kiongozi wa waasi waliopindua serikali, Amadou Sanogo ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kusaidia jeshi kupambana na waasi hao.
Shirika la nchi za kanda ya Magharibi mwa Afrika, ECOWAS, limelaani kitendo cha wanajeshi, huku nchi hizo zikitishia kuiwekea vikwazo Mali.
Viongozi wa nchi za magharibi mwa Afrika wamewapa wanajeshi waliopindua serikali ya Mali makataa ya saa 72 kuondoka madarakani au waadhibiwe kwa kuwekewa vikwazo vya kiuchumi.
Viongozi hao wametangaza kuwa watafunga mipaka yote ya Mali na kufunga akaunti ya nchi hiyo.
Hii ni baada ujumbe mzito wa viongozi wa ECOWAS kushindwa kutua katika uwanja wa ndege wa Bamako kutokana na maandamano makubwa ya kuunga mkono mapinduzi hayo.
Viongaoi wa ECOWAS,walikutana Ivory Coast, baada ya mpango wao kwenda kwa mazungumzo na viongozi wa wanjeshi waasi , Mali kutibuka.

Thursday, March 29, 2012

Skendo ya ngono yatikisa kanisa katoliki...


Skendo ya ngono yatikisa kanisa katoliki...

STORI NA MAKONGORO OGING"
Skendo ya ngono inaitikisa Kanisa  la Katoliki, Parokia  ya Mburahati  lililopo wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam  na kusababisha  mgawanyiko  mkubwa  kwa waumini.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wetu zimebaini kuwa skendo hiyo ya ngono inamhusisha Padri Paul Njoka na mhudumu wa nyumba za mapadri  ambaye pia ni muumini wa kanisa hilo aliyejulikana kwa jina moja la Mwasiti.
Taarifa zilizopatikana kanisani hapo zinadai kwamba padri huyo alimjaza mimba mhudumu huyo na hivi sasa amezaa naye mtoto.
Habari hizo zilienea kanisani hapo na kusababisha baadhi ya waumini kutaka suala hilo liwekwe wazi ili kiongozi huyo achukuliwe hatua zaidi, jambo  lililomfanya kasisi huyo  atafute jinsi ya kujihami.
Chanzo chetu cha habari  kinasema kwamba baadhi ya viongozi wa kanisa hilo walifikia hatua ya kutafuta jinsi ya kumficha mtoto  huyo baada ya kuzaliwa ili kupoteza ushahidi.
 Imeelezwa kwamba Februali 4, mwaka huu Padri Njoka akiwa na muumini  aliyejulikana kwa jina  la Maria Kaswela walichukua gari na kumsaka Mwasiti, walimpata na kumuingiza katika gari hilo.
Imedaiwa kwamba katika  mzunguko wao, Mwasiti hakujua ni kitu gani alichotakiwa kufanyiwa na mtoto wake bali yeye alijua ni matembezi ya kawaida  huku akifurahia ni jinsi gani  padri anavyompenda mtoto wake na kuamua kuzunguka naye jijini kwa siku hiyo.
Chanzo kilidai kwamba siku hiyo padri huyo na mzazi mwenzake walielekea  Sinza,Manzese kisha  Magomeni.
MTOTO ATEKWA
Walipofika Magomeni habari zinasema  walimtuma dukani mama wa mtoto (Mwasiti) na mtoto akawa amebebwa na Maria.
Chanzo kiliendelea kudai kwamba padri aliendesha gari na kuondoka eneo la Magomeni kwa kasi kuelekea kusikojulikana na Mwasiti alipotoka dukani na kwenda sehemu lilipoegeshwa gari hakuwaona na alipowapigia simu hawakupatikana.
TAARIFA YAFIKA POLISI
Hata hivyo, Mwasiti alipatwa na hofu kwani ilimchukua muda mrefu bila kuwaona,  kitendo kichomfanya aende Kituo cha Polisi, Wilaya ya Kipolisi ya Magomeni kutoa taarifa ya kutekwa kwa mtoto wake wa siku 28 tangu azaliwe.
Mwasiti alifunguliwa jalada lenye kumbukumbu MG/RB/2430/2012 ndipo polisi walipoanza kazi ya kuwatafuta padri na Maria  bila mafanikio.
Habari zinasema polisi walifanikiwa kumuona Padri Njoka akiwa kanisani siku ya Jumapili akiendesha ibada  ila ilishindikana kumkamata kwa sababu misa ilikuwa ikiendelea.
Kutokanana kitendo cha padri huyo kuendesha misa, askari hao waliacha taarifa kwa mlinzi wa kanisa hilo  kwamba baada ya kumaliza ibada afike Kituo cha Polisi  Magomeni akiwa na Maria.
Hata hivyo, hawakwenda siku hiyo badala yake walienda kesho yake Jumatatu ya Februali 6, mwaka huu.
“Mara walipofika kituoni waliwekwa chini ya ulinzi, walibanwa ili waonyeshe alipo mtoto ambapo walisema kwamba yupo  Kigamboni kwa ndugu wa padri huyo,” chanzo hicho kilisema.
Polisi waliwaamuru watoe namba ya simu ya watu walio na mtoto huyo ili wapigiwe, padri alitoa, ilipopigwa aliye na mtoto akaamriwa amlete kituoni hapo na akafanya hivyo saa 5.00 usiku padri akiwa chini ya ulinzi.
Hata hivyo, polisi walipomkabidhi Mwasiti mtoto wake alikataa kumpokea na kudai kwamba akapimwe afya yake kwanza kwa vile  hakujua alichofanyiwa huko na alikua katika mazingira gani.
Chanzo kiliendelea kusema kwamba hapo polisi Magomeni alikuwepo pia Paroko Timoth Nyasulu Maganga  ambaye  ni mkubwa wake wa kazi Padri Njoka.
Habari zinasema Padri Maganga alimbembeleza Mwasiti amchukue mtoto wake ambaye alikubali kisha alikwenda naye Kinondoni kwa dada wa mzazi huyo. Uchunguzi wetu umebaini kuwa kesi hiyo ipo chini ya mpelelezi mwenye namba WP697 Tiba.
WARAKA KWA PENGO
Kutokana na kitendo hicho,   baadhi ya waumini wa kanisa hilo waliamua kumuandikia barua Februali 8, mwaka huu Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Muadhama Askofu Polycarp Kadinali Pengo kuhusu udhalilishaji wa Kanisa Katoliki waliodai kufanywa na padri huyo kwa kumteka mtoto.
Katika barua hiyo (Nakala tunayo) waumini hao wameeleza jinsi wachunga kondoo walivyofikia  hatua ya kufanya mapenzi  na wafanyakazi, wahudumu wa nyumba ya mapadri na kuwapa mimba.
 Hata hivyo, katika barua hiyo waumini hao wamesikitishwa na kitendo hicho  na kudai kuwa gharama kubwa za fedha za kanisa zimetumika kushughulikia suala hilo.
“Tunakuomba ufanyie kazi jambo hili kwa haraka inawezekanavyo ili kuepusha  uvunjifu wa amani endapo viongozi  hao wachafu watabaki hapo parokiani,” ilisema sehemu ya barua hiyo.
Barua hiyo imeendelea kueleza kuwa mapenzi yanayofanyika kanisani hapo kati ya viongozi na waumini yamesababisha utoaji hovyo wa mimba hadi wengine kuzalishwa, kitendo ambacho kinalitia aibu Kanisa Katoliki.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela hakupatikana kuzungumzia tukio hilo lakini afisa mmoja wa cheo cha juu wa jeshi hilo alithibitisha kuwepo kwa madai hayo kuongeza kuwa upelelezi bado unaendelea.
Aidha, Kadinali Pengo hakuweza kupatikana kuzungumzia malalamiko hayo ya waumini wake.
Gazeti hili linaendelea kufuatilia sakata hilo kwa undani zaidi ili kujua ni hatua gani zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa.

Wabunge waibua ufisadi wa mabilioni D’Salaam

Wabunge waibua ufisadi wa mabilioni D’Salaam  Send to a friend
Wednesday, 28 March 2012 20:50
0digg
Mwenyekiti wa LAAC, Augustine Mrema
Patricia Kimelemeta na Ramadhan Semtawa
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeibua tuhuma za ufisadi wa Sh2.7 bilioni katika mradi wa ujenzi wa machinjio ya kisasa Gongo la Mboto, Dares Salaam uliopaswa kufanywa na Kampuni ya East Africa Meat (EAMC).Mradi huo ulipaswa kutekelezwa kati ya mwaka 2005/06 kwa ushirikiano wa jiji na Manispaa tatu za Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam jana kwenye kikao kati ya kamati yake na watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Mwenyekiti wa LAAC, Augustine Mrema alisema kampuni hiyo ya Malaysia ndiyo iliyoshinda zabuni ya ujenzi wa machinjio hayo.
Mrema alisema katika mradi huo, Halmashauri ya Jiji iliingia mkataba wa kughushi na EAMC, huku wakiwashawishi watendaji kushiriki kwenye ujenzi wa machinjio hayo yanayodaiwa kuwa ya kisasa.
Alisema kutokana na hali hiyo Halmashauri ya Kinondoni ilitoa Sh229milioni wakati ya Ilala ilitoa Sh364miloni, Temeke ilitoa Sh224milioni huku jiji likitoa Sh1.2bilioni.
Alisema kutokana na hali hiyo, fedha hizo zimepelekwa kwenye miradi huo ambao mpaka sasa haujatekelezeka jambo ambalo linaonyesha kuwa kuna baadhi ya wajanja ambao wamechukua fedha hizo.
“Tunajua kabisa kuwa kuna baadhi ya vigogo wameshiriki kuwarubuni watendaji wa halmashauri kwa ajili ya kutekeleza miradi hewa, hatutakubali na kila aliyeshiriki atachukuliwa hatua za kisheria,” alisema Mrema.
Alisema mbali na hilo, baadhi ya vigogo hao ndiyo walioshiriki kwenye kashfa ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), ambalo ripoti yake bado inasubiriwa ikabidhiwe serikalini kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Mrema alisema kutokana na hali hiyo, LAAC itawasilisha taarifa hizo kwa watendaji wakuu ili waweze kuangalia hatua stahiki za kurudishwa kwa fedha hizo katika halmashauri ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani wahusika walioshiriki kwenye utapeli huo.
“Haiwezekani hata kidogo watu wachache wanufaike na rasilimali za taifa kwa manufaa yao, jambo ambalo limesababisha kuingia mikataba feki ambayo wanajua kabisa kuwa haiwanufaishi wananchi. Lazima fedha hizi zirudi,” alisema.
Meya: Kampuni imefilisika
Hata hivyo, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk Didas Masaburi alisema kampuni hiyo imefilisika na kwamba hakuna mtu atakayeweza kulipa deni hilo. Kutokana na hali hiyo, alisema watakaa na halmashauri za manispaa ili kuangalia jinsi ya kutatua matatizo hayo.
“Kampuni yenyewe imefilisika, nani atalipa deni hilo? Hakuna kwa sababu hata jiji ni miongoni mwa watu waliotapeliwa japo tulikuwa tumeingia ubia lakini kilichofanyika ni kwamba mradi huo haujatekelezeka,” alisema Dk Masaburi.
Alisema machinjio hayo yalitakiwa kujengwa mwaka 2006, lakini mpaka sasa hayajengwa na wala hakuna eneo la ujenzi.
Meya Masaburi alisema halmashauri hizo zilitoa fedha hizo na kudaiwa kuwa zimetumika kwenye upembuzi yakinifu na kuongeza kwamba, ilipofika mwaka 2009, madiwani wa jiji na manispaa walitaka ufafanuzi kuhusu suala hilo na kuitaka jiji kujiondoa kwenye mkataba huo jambo ambalo lilisababisha halmashauri hizo kudai fedha zao ambazo mpaka sasa hazijalipwa.
Alisema wakati hayo yakiendelea, tayari kampuni hiyo ilikuwa imefilisika na hakuna mtu mwenye uwezo wa kuendelea na mkataba au kurudisha fedha.
“Meneja wa kampuni hiyo ambaye ni raia wa Zimbabwe aliyejulikana kwa jina la Benjamin Chipazi ni miongoni mwa watu waliotapeliwa, anadai mafao yake ya zaidi ya Dola za Marekani 150,000, lakini ameshindwa kulipwa kwa sababu hakuna mtu aliyerithi madeni hayo,” alisema.
Alisema kutokana na hali hiyo, jiji haliwezi kurithi madeni ya kampuni hiyo na kwamba kila mmoja anapaswa kutambua kuwa katika mkataba huo wametapeliwa.
Iddi Simba Mwenyekiti
Alipoulizwa jana, Mwenyekiti wa EACM, Iddi Simba alikiri kuwa kampuni hiyo na ilikuwa ijenge mradi huo.
Alisema EACM ilikuwa ni kampuni iliyoanzishwa kwa kuhusisha jiji na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam wakati huo alikuwa akiingia kwenye vikao akiwa mjumbe.
Alisema awali, jiji na manispaa zake tatu lilibuni mradi huo wa kujenga machinjio ya kisasa katika kiwanja chake cha Gongo la Mboto kilichokuwa na thamani ya Sh bilioni moja ambacho kilitumika kama sehemu ya mchango wa fedha katika hisa zake.
Alisema katika mkataba huo, Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni kila moja ilipaswa kutoa Dola 500 za Marekani ikiwa ni mchango kwa hisa zake hivyo kufanya tahamani ya mtaji kufikia Dola 2.5milioni.
“Lakini, kilichotokea ni kwamba, fedha hizo za manispaa hazikutolewa katika kipindi ambacho mradi ulipaswa kuanza. Hivyo, kampuni ikafilisika kwa sababu hata watu wengine waliotaka kuwekeza fedha zao walisita baada ya kuona manispaa hizo zinasuasua,” alisema.
Alisema kampuni iliyofanya upembuzi yakinifu ilikuwa ya mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (jina tunalihifadhi kwa kuwa hakupatikana kujibu madai hayo jana).
Simba alisema hakuna fedha ambayo imeliwa na EACM kwani hata kiwanja hicho ambacho ni mali ya halmashauri ya jiji, bado kiliachwa mikononi mwa mamlaka hiyo.
Kuhusu ni kiasi gani cha fedha ambacho manispaa hizo tatu zilitoa hadi kampuni hiyo ilipokuwa ikikaribia kufilisika, Simba alijibu, “Sijui. Wewe umenikurupusha tu hapa sina nyaraka zozote.”
Lakini alisisitiza kwamba EACM haikuwahi kuuza kiwanja hicho kwani bado kiliachwa mikononi mwa jiji hilo hadi kampuni ilipofilisika.

"What does a Pope do?" Fidel Castro asks Benedict

"What does a Pope do?" Fidel Castro asks Benedict

email
email

Havana (Cuba):  Pope Benedict and Cuban revolutionary leader Fidel Castro, both octogenarians, joked about their age in a brief meeting on Wednesday and then Castro popped the question: so what do you do?

The two world figures chatted for about 30 minutes at the Vatican embassy in Havana near the end of the pope's three-day visit to Cuba, where he called for greater freedom and a bigger role for the Catholic Church in the communist-led nation.

Vatican spokesman Father Federico Lombardi said Benedict, 84, and Castro, 85, had an "exchange of ideas" in a "very cordial" atmosphere.

Mr Castro led a 1959 revolution and transformed the Caribbean island into a communist state, ruling it for 49 years before stepping down due to poor health in 2008. Under his rule, Cuba for years called itself an atheist state, although relations with the Church have improved over the past two decades.

Mr Castro arrived for his meeting with the pope on Wednesday in a green Mercedes SUV amid heavy security that included armed guards in a phalanx of surrounding black Mercedes cars.

He was helped out by two assistants, who supported him as he walked slowly up the steps into the stately white building where Benedict spent Tuesday night and where Pope John Paul II stayed during his landmark 1998 visit.

"What does a pope do?" Mr Castro asked Benedict, who is just one year his junior. The pontiff told him of his ministry, his foreign trips and his service to the Church, saying he was happy to be in Cuba and with the welcome he received.

Dressed in a dark Reebok track suit and wearing a scarf despite the searing heat outside, Mr Castro told the pontiff he had watched his whole visit on television. Two of his children were also presented to the pope.

Mr Castro handed the reins of power to his younger brother, President Raul Castro, four years ago and he has since largely retired from government but he still writes columns and meets with visiting leaders.

He told the pontiff he was spending most of his time reading and reflecting on the state of the world.

His columns are posted on the internet and read aloud on state television, and cover his fears of impending Armageddon, the evils of consumerism and his criticisms of arch ideological foe, the United States.

CASTRO SEEKS FOOD FOR THOUGHT

Mr Castro questioned Benedict about changes in Church liturgy and asked the pope to send him a book to help him reflect. The pope said he would think of which one to send, but had not yet decided, Lombardi said.

The pair discussed the difficult world situation and the problems of mankind from a religious, scientific and cultural point of view.

And the Pope also spoke to Mr Castro about the problem of the absence of God in much of society today and the relationship between faith and reason.

As he was waiting for the Pope, Mr Castro said he had great admiration for Mother Teresa and for John Paul, whose visit 14 years ago marked a watershed in long-strained relations between the communist government and the Church.

Castro reinstated Christmas as a holiday ahead of John Paul's visit, and in talks on Tuesday with Raul Castro, the pope asked the government to consider also making Good Friday, the day Christians commemorate Christ's death, a national holiday.


Read more at: http://www.ndtv.com/article/world/what-does-a-pope-do-fidel-castro-asks-benedict-191352&cp

Wednesday, March 28, 2012

Watu milioni 15 wakabiliwa na njaa Sahel


Watu milioni 15 wakabiliwa na njaa Sahel

 29 Machi, 2012 - Saa 03:11 GMT
Mkurugenzi wa Opareshini anayeshughulikia maswala ya kibinadam amelitaja eneo hilo kuwa ni janga la kimataifa.
Maeneo ya Sahel yanayokumbwa na njaa
Bwana John Ging ametaka mipango madhubuti iandaliwe katika kukabiliana na janga hilo linalotishia maisha ya mamilioni ya watu.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa mamilioni ya watu katika eneo la Afrika la Sahel lililokumbwa na baa la njaa wanakabiliwa na upungufu wa chakula uliosababishwa na ukame na migogoro, na mipango ya kuwapatia msaada ni chini ya asilimia 40 ikitolewa kwa ajili ya kukabiliana na hali itakapofikia kilele chake.
Sahel ni eneo lenye nchi karibu kumi na mbili zikiwa maskini kuliko zote kusini mwa jangwa la Sahara.
John Ging amesema watu milioni 15 wameathiriwa na tatizo la ukoefu wa chakula.
Akizungumza baada ya kutembelea nchi za Niger, Burkina Faso na Mauritania,
amesema tayari huu ni mgogoro kwa upande wa ukubwa wa tatizo lenyewe na kiwango cha mateso ya binadamu na litakuwa baya zaidi, la ivyo mipango ya kukabiliana nalo inatengewa fedha za kutosha.
Ni suala la kufa au kupona kwa mamilioni ya watu walio katika janga hilo.
Bwana Ging amesema mwaka huu mamilioni wa watu katika eneo la Sahel siyo tu wamekosa mvua lkini madhara yake baada ya vita vya Libya, hofu kutoka mapigano ya Nigeria kati ya serikali na kikundi cha Boko Haram na hivi karibuni mapinduzi ya kijeshi nchini Mali.

MWANACHUO ALIEMTUKANA FABRICE MUAMBA KWA KUANGUKA UWANJANI AHUKUMIWA KWENDA JELA.

MWANACHUO ALIEMTUKANA FABRICE MUAMBA KWA KUANGUKA UWANJANI AHUKUMIWA KWENDA JELA.

2
.
Mwanachuo wa Uingereza Stacey Liam ambae aliandika kwenye twitter maneno ya kibaguzi na matusi kwa mchezaji Fabrice Muamba wa Bolton muda mfupi baada ya kuanguka uwanjani siku kumi zilizopita, amehukumiwa kwenda jela.
Stacey alipandishwa mahakamani wiki iliyopita na kukubali kosa baada ya kukamatwa na polisi ambao walipata taarifa za Liam kutoa maneno hayo ya kibaguzi kupitia kwa watu mbalimbali waliyoyaona kwenye twitter na kuchukizwa nayo.
The sun wamesema Adhabu ambayo alikua apewe ni miaka saba gerezani lakini jaji amesema mwanachuo huyo amehukumiwa kwenda jela kwa siku 56 (mwezi mmoja na siku kama 25) kwa kosa hilo.

Waziri amkana Mkapa Arumeru

Waziri amkana Mkapa Arumeru  Send to a friend
Tuesday, 27 March 2012 20:33
0digg
ASEMA HAKUNA TATIZO LA ARDHI, WARAKA WASAMBAZWA KUMPINGA SIOI
Waandishi Wetu, Arumeru
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodlucky Ole Medeye amewatetea walowezi wanaomiliki maeneo makubwa ya ardhi katika Jimbo la Arumeru Mashariki kwamba wanamiliki mashamba hayo kwa mujibu wa sheria.
Kauli ya Ole Medeye ambaye alikuwa akimnadi mgombea wa CCM, Sioi Sumari katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo inapingana na ile iliyotolewa na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa alipokuwa akizindua kampeni za CCM, Machi 12 mwaka huu mjini Usa River.
Kadhalika, kauli hiyo inapingana na kauli zote za makada wa CCM na vyama vya upinzani akiwamo mgombea wa CCM Sioi ambao wanakiri kuwapo kwa matatizo makubwa ya ardhi Arumeru, huku wakiahidi kuyashughulikia.
Mkapa akizungumzia matatizo ya ardhi siku ya uzinduzi huo, kwanza alikanusha kuwa na ubia na walowezi hao lakini akakiri kuwapo kwa matatizo hayo huku akiahidi kwamba atafikisha suala hilo kwa Rais Jakaya Kikwete ili alipatie utatuzi.
Mkapa alikiri kupokea taarifa za kuwapo kwa migogoro mikubwa ya ardhi inayosababishwa na baadhi ya wawekezaji kuhodhi maeneo makubwa na kusema kwamba kero hiyo iko katika hatua mbalimbali za utatuzi wake.

“Yapo matatizo kadha wa kadha, wapo wawekezaji ambao wamehodhi maeneo makubwa wakati hawayatumii, wapo ambao wamechukua maeneo na kubadilisha matumizi yake na wapo ambao wamekiuka sheria za uendeshaji wa maeneo waliyopewa,” alisema Mkapa.
Alisema suala hilo atalifikisha kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na kumshauri achukue hatua kwa kuwawajibisha watendaji wa serikali ambao wameshindwa kuwajibika na kuchukua hatua za kisheria kwa wawekezaji waliokiuka masharti.
Lakini jana, Ole Medeye alisema mashamba yote 13 yanayotajwa yanamilikiwa kihalali na kwamba ikiwa kuna tatizo lolote basi wizara yake itafuatilia ili kuchukua hatua.
“Masuala ya umiliki wa ardhi yanasimamiwa na sheria za nchi, kwa hiyo wawekezaji hawa wanaotajwa, wanamiliki maeneo yao kwa mujibu wa sheria. Sasa kama kuna maeneo hayajaendelezwa basi hilo ni suala la kuona jinsi ya kuchukua hatua,” alisema Medeye katika mkutano wa kumnadi Sioi uliofanyika katika Kijiji cha Sing’isi.
Medeye ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Magharibi alisema Serikali imekuwa ikichukua hatua madhubuti kutatua kero ya ardhi ndani ya wilaya hiyo na kwa sasa itayatwaa mashamba yote yanayomilikiwa na watu binafsi endapo hayataendelezwa ili yagawiwe kwa wananchi. Aliyataja mashamba ambayo hayajaendelezwa kuwa ni Valeska, Madira na Tanzania Plantation.
Alisema akiwa Naibu Waziri wa Ardhi tayari ametembelea mashamba yote na kwamba Serikali inajipanga jinsi ya kutatua migogoro iliyopo. Alisema endapo watamchagua mgombea wa CCM atashirikiana naye kwa kuwa atakuwa anamkubusha juu ya utekelezaji wa kero za ardhi.
Alisema hoja za wapinzani kwamba wanaweza kurejesha ardhi kwa wananchi si kweli kwani ili kufikia hatua hiyo lazima sheria zifuatwe.
Amvaa Dk Slaa
Ole Medeye alimshukia Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kwamba ameshindwa kutatua kero ya ardhi na maji katika Wilaya ya Karatu alikokuwa mbunge kwa miaka 10 hivyo asirukie hoja ya Arumeru Mashariki.
Alisema katika Wilaya ya Karatu inayoongozwa na Chadema, kuna mashamba 32 yanayomilikiwa na wawekezaji ambao kimeshindwa kuwanyang’anya.
Alisema Karatu ambako Chadema kinashika dola kwa kuongoza halmashauri, inaongoza kwa tuhuma za ufisadi kwa kuwa baadhi ya madiwani wa chama hicho waligawana eneo la shule mojawapo ya msingi na kisha kujenga vilabu vya pombe na nyumba za wageni karibu na shule hiyo.
Alisema mmoja wa madiwani wa Chadema alibaini ufisadi huo na kuandika barua wizarani kwake. Alisema alifunga safari kwenda Karatu ambako alishudia madudu hayo na kisha kuvifuta viwanja hivyo.
Waraka wasambazwa
Watu wasiojulikana jana walisambazwa waraka ambao unadaiwa kuandikwa na wabunge wa CCM ambao wanapiga vita ufisadi wakitaka mgombea wa CCM, Sioi Sumari asichaguliwe kwani atawaongezea nguvu mafisadi kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Waraka huo ambao jana ulikuwa ukisambazwa katika mitaa mbalimbali ya Usa River na kwenye mikutano ya kampeni ya Chadema na CCM, una kichwa cha habari kisemacho “Chama cha Mapinduzi na Kamati maalum dhidi ya ufisadi.”
Katika waraka huo ambao haujasainiwa na mtu yeyote unadaiwa kutumwa kwa wananchi wa Meru na wabunge wa CCM ambao picha zao zimeambatanishwa.
“Tunawaandikia waraka huu kwa kuwa tunaamini kabisa kwa kufanya hivyo tunamfurahisha Mungu na kuwanusuru na kiu ya damu ya baadhi ya viongozi wa nchi hii. Mafisadi hawa wameshindwa kabisa kuacha ufisadi na sasa wanatumia fedha walizowaibia Watanzania…” inasomeka sehemu ya barua hiyo.
Kadhalika waraka huo unamtaja mmoja wa makada wakongwe wa CCM (jina tunalihifadhi) kwamba ameamua kutunisha misuli yake na kuhakikisha Sioi anashinda ubunge Arumeru, lengo likiwa ni kuonyesha kwamba ana nguvu zaidi kwa kutumia fedha zake.
Chadema jana walikana kuufahamu waraka huo na kusema kuwa wenye uzoefu wa kuandika nyaraka za aina hiyo ni CCM.
Mkuu wa operesheni wa uchaguzi huo wa Chadema, John Mrema alisema: “Sisi hatuwezi kuandaa waraka kama huu, haya ni mambo ya CCM wenyewe.”
Meneja Kampeni wa CCM, Mwigulu Nchemba hakupatikana jana kuzungumzia waraka huo.

Chadema chadai kadi 668 Polisi
Chadema jana kimeitaka Polisi kurejesha kadi za kupigia kura za watu 668 ambazo zinashirikiliwa Kituo chake cha Usa River na Kituo Kikuu cha Arusha.
Mrema alisema wamepata taarifa kutoka polisi za kuwapo vitambulisho vya kupiga kura 206 katika Kituo cha Usa River ambavyo vimeachwa na watu waliokwenda kuwawekea dhamana watuhumiwa. Alisema katika Kituo Kikuu Arusha kuna kadi za vijana wa Meru 462 ambao wanafanyakazi za kubeba mizigo ya watalii katika Mlima Meru maarufu kama Wapagazi.
Mkuu wa Oparesheni ya Polisi katika uchaguzi wa Arumeru Mashariki, Isaya Mngulu alisema asingeweza kutoa maelezo yoyote kuhusu madai hayo akisema maofisa wa ngazi za juu wa polisi walikuwa kwenye kikao.
CCM wapigwa mawe
Jana, msafara wa CCM ulishambuliwa kwa mawe katika Kijiji cha Sing’is ulipokuwa umekwenda kwa ajili ya kumnadi mgombea wake, Sioi Sumari.
Katika tukio hilo, mmoja wa vijana wanaoshukiwa kuhusika na shambilio hilo alikamatwa na vijana wanaosadikiwa kuwa wa CCM na kupigwa hadi kupoteza fahamu hadi alipookolewa na polisi waliokuwa nyuma ya msafara huo.
Tukio hilo lilitokea saa 6.30 mchana jana wakati msafara huo wa CCM ulipofika eneo la Chama na ghafla walijitokeza vijana watatu mbele ya magari hayo kisha kuanza kuyashambulia kwa mawe. Vijana hao watatu walikuwa wamevaa beji zenye picha ya mgombea wa Chadema, Joshua Nassari.
Katika tukio jingine, kijana ambaye hakufahamika jina, juzi jioni alipigwa kwenye mkutano wa CCM katika Viwanja vya Ngaresero baada ya kuishangilia helkopta ya Chadema iliyopita kwenye eneo hilo wakati Sioi akihutubia.

Huko Seela Sing’isi, vijana watatu ambao walikuwa wakinyoosha vidole viwili ambayo ni alama ya Chadema, jana walikamatwa kwenye mkutano wa kumnadi Sioi. Vijana hao walikuwa wamesimama nyuma ya eneo la mkutano na walishikiliwa na polisi baada ya Ole Medeye kutamka kwamba wanaoiunga mkono CCM wanyooshe mikono juu na wao wakanyoosha alama ya vidole viwili.

Annan akutana na Medvedev kuhusu Syria

Annan akutana na Medvedev kuhusu Syria

 25 Machi, 2012 - Saa 15:03 GMT
Urusi imeonya kuwa ujumbe wa Kofi Annan, uliotumwa Syria na Umoja wa Mataifa na Jumuia ya Nchi za Kiarabu, unaweza kuwa fursa ya mwisho ya kuepuka vita.
Kofi Annan na Sergei Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Urusi, mjini Moscow
Onyo hilo limetolewa na Rais Dmitri Medvedev wa Urusi, alipokutana na Bwana Annan ambaye amewasili Moscow kujadili swala la Syria, na njia za kumaliza utumiaji nguvu nchini humo.
Anajaribu kuishawishi Urusi - mshirika muhimu wa Syria - ichukue msimamo mkali dhidi ya Rais Bashar al Assad.
Warusi wanasema haifai kuweka muda maalumu kwa Bwana Annan kumaliza kazi yake; na baada ya muda itabainika kama Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linahitaji kuchukua hatua zaidi kuhusu Syria.
Huku nyuma, "Jeshi Huru la Syria" la upinzani, limetangaza kuwa wapinzani watashirikiana katika mapigano yao dhidi ya serikali.
Katika ghasia za karibuni, baina ya askari wa usalama wa Syria na upinzani, wanaharakati wanasema watu kama 54 waliuwawa Jumamosi

Abdoulaye Wade akubali ameshindwa

Abdoulaye Wade akubali ameshindwa

 26 Machi, 2012 - Saa 03:20 GMT
Shirika la habari la serikali nchini Senegal limetangaza kuwa rais Abdoulaye Wade amekubali kushindwa na mpinzani wake Macky Sall katika dura ya pili ya uchaguzi wa Urais.
Macky Sall kiongozi mpya wa Senegal
Bwana Wade alimpigia simu mpizani wake Macky Sall, na kumuambia kuwa amekubali kushindwa.
Na maelfu ya wafuasi wa Macky Sall wamejitokeza katika barabara za mji wa Dakar wakisherehekea ushindi wa kiongozi wao.
Miongoni mwa waliokuwa wakisherehekea ni Bi Seynabou Seck
" Niimefurahi sana , Macky bado ni kijana na tena ni mtu mpole sana na ana heshima! Kwa hakika anastahili ushindi huu . Kila mtu alikuwa akimuombea ashinde”.
Mshindi huyo wa duru hiyo ya pili ya uchaguzi wa urais ameutaja ushindi wake kama muamko mpya kwa raia wa Senegal.
Macky Sall alikuwa akizungumza mara tu baada ya mpinzani wake Abdoulaye Wade mwenye umri wa 85 kukubali kuwa ameshindwa katika duru hiyo ya pili.
Wade alikuwa anataka kuchaguliwa tena kama raia wa Senegal kwa muhula mwengine wa tatu baada ya kubadilisha katiba ya nchi hiyo.
Mabadiliko hayo yalizua machafuko na vurugu kubwa nchini Senegal.
Machafuko hayo halishtua ulimwengu kwani tofauti na jirani zake Senegali imekuwa tulivu na hajawahi kuwa na mapinduzi ya kijeshi kama jirani zake.
Lakini upinzani ulipinga hatua ya kiongozi wao mkongwe na kwenda mahakamani. Hata hivyo mahakama iliidhinisha hatua ya Wade ya kubadili katiba ili aweze kusimama tena kama rais.
Na baada ya dura ya kwanza kukosa kuwa na mshindi wa moja kwa moja kwani hakuna aliyepata zaidi ya asilimia 50, ikiwa ni lazima kuwe na duru ya pili ambapo viongozi wote wa upinzani walimuunga mkoni Macky Sall.
Na sasa Macky Sall ambaye zamani alikuwa Waziri mkuu katika serikali ya Abdoulaye wade ameibuka mshindi.

Mapigano makali Sabha, Libya


Mapigano makali Sabha, Libya

 27 Machi, 2012 - Saa 16:29 GMT
Mapigano kati ya makundi hasimu ya wapiganaji nchini Libya yamesababisha vifo vya watu 20. Mapigano hayo yalifanyika eneo la Sabha kati ya wapiganaji wa kabila la Toubou baada ya mpiganaji mmoja kuawa katika mzozo wa umiliki wa gari.
Majeshi ya serikali yamefika eneo hilo kutuliza hali. Utawa wa mpito wa Libya unakumbwa na wakati mgumu kudhibiti nchi hiyo baada ya kumuondoa Kanali Muammar Gaddafi mwaka jana.
Ahmed al Hamrouni ambaye zamani alikuwa kamanda wa waasi amesema milio ya roketi imesikika katika barabara kuu huku moshi ukionekana kupaa juu ya uwanja wa ndege wa Sabha.
Serikali ya mpito imewashawishi wapiganaji waliosaidia kumng'oa madarakani kanali Gaddafi kusalimisha silaha na kujiunga na jeshi la taifa.
Mwakilishi wa utawala wa mpito amesema makabiliano yalianza pale wapiganaji wa kabila la Toubou walipojaribu kuiba gari la mpiganaji wa kundi la Sabha.
mapigano sabha
Msemaji huyo amesema kamati ya maridhiano imeundwa ili kumaliza mapigano.

Mali yasimamishwa uanachama

Mali yasimamishwa uanachama

 28 Machi, 2012 - Saa 01:48 GMT
Jumuiya ya Afrika Magharibi ECOWAS imesimamisha uanachama wa Mali kuafuatia hatua ya jeshi kuoindua serikali ya Rais Amadou Toumani Toure .
Wanajeshi wa Mali waonywa na ECOWAS
Viongozi wa Jumuiya hiyo walifikia uamuzi huo katika mkutano uliofanyika nchini Ivory Coast.
Sasa viongozi hao kutoka nchi sita wanachama wa ECOWAS wamepanga kusafiri hadi mjini Bamako Mali ili kukutana na baraza kuu la jeshi linalotawala nchi hiyo.
Akihutubia waandishi wa habari baada ya mkutano huo Rais wa Ivory Coast, alisema Amadou Toumani Toure bado yuko hai na yuko katika hali njema .
Kiongozi huyu wa Ivory aliongezea kuwa alizungumza na Toure saa chache kabla ya mkutano wao kuanza.
Na kwa wale waliohusika na kumwangusha madarakani rais wa Mali, ECOWAS imechukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kusitisha uanachama wao katika chombo hiki, kulaani mapinduzi hayo ya kijeshi na kutishia kuiwekea vikwazo nchi hiyo iwapo viongozi wapya wa kijeshi hawatarejesha utawala wa katiba.
Nae mwenyekiti mpya wa Tume ya ECOWAS, Kadre Desire Ouedraogo, ametoa wito wa kuachiliwa huru kwa wafungwa wa kisiasa na kumchagua Rais Blaise Compaore wa Burkina Faso kuwa msuluhishi wao.
"Mkutano huu unaidhinisha kuyapa uwezo majeshi ya akiba ya ECOWAS kujiandaa kwa kila tukio.
Endapo kutatokea kutoheshimu maamuzi ya CNRDR, mkutano unawaagiza wanachama wote kuweka mara moja vikwazo vya usafiri na kidiplomasia na fedha dhidi ya watawala hao wa kijeshi na marafiki zao,” Desire-Ouedraogo alitangaza "
Rais wa Ivory Coast, Alassane Ouattara anatarajiwa kuongoza ujumbe wa viongozi sita wa nchi za Afrika Magharibi kwenda Mali kukutana na viongozi wa kijeshi.
Rais Ouattara pia amesema viongozi hao wa kijeshi wamekwisha taarifiwa kuhusu msimamo wa ECOWAS.
Rais wa Ivory Coast amesema kwa wakati huu, mazungumzo yanahitajika zaidi katika kutatua mgogoro wa kikatiba nchini Mali, lakini amesema hawatasita kutumia njia nyingine zote mbadala iwapo hii itashindikana.
Kikundi cha viongozi wa kijeshi wa kanda hiyo pia nao wamepanga kwenda Bamako kuwashauri viongozi wa kijeshi wa nchi hiyo kukabidhi madaraka kwa utawala wa kiraia, lakini pia kuweka wazi namna ECOWAS itakavyosaidia kukabiliana na mashambulio ya waasi kaskazini mwa nchi ya Mali.

Tuesday, March 27, 2012

Sudan na Sudan kusini zapigana vikali.

Sudan na Sudan kusini zapigana vikali.

 26 Machi, 2012 - Saa 23:52 GMT
wapiganaji wakikabila wa Sudan Kusini
Mapigano mapya yamizuka kati ya majeshi ya Sudan na yale ya Sudan kusini .
Pande zote zinasema kuwa mapigano hayo yametokea katika maeneo kadhaa ya mipaka kati ya mataifa hayo mawili.
Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini amesema mapigano hayo ndio makubwa na mabaya zaidi kuwahi kutokea tangu nchi hiyo ijipatie uhuru wake toka Sudan.
Na kuchipuka kwa mapiganao hayo mapya kumemfanya Rais Salva Kiir kuonya kuwa vita vinanukia eneo hilo
Rais Kiir amesema," asubuhi hii anga yetu ilishambuliwa kwa mabomu ....Ni katika maeneo ya Unity.
"Kiongozi huyo wa Sudan kusini amesema ni vita ambavyo wanalazimishwa kuwa navyo. Na ni Sudan ndio inatafuta vita hivyo"
Nae msemaji wa jeshi la Sudan amenukuliwa akisema kuwa vita viko katika maeneo ya South Kordofan na kusini mwa jimbo la Unity.
July mwaka jana Sudan kusini ilijitenga rasmi na Sudan baada ya vita vya miaka mingi.
Licha ya kujitenga huko kumekuwa na malumbano ya kisiasa na mikwaruzano kati ya nchi hizo mbili kutokana na sababu kadhaa lakini kubwa zaidi ikiwa ni zogo la mafuta.
Radio ya kitaifa ya Sudan imetangaza kuwa Rais Omar el-Bashir amehairisha ziara yake ya kwenda Sudan Kusini.
Vita hivi pia vinakuja wakati mkutano ulikuwa umepangwa kufanyika wiki ijayo kati ya Bashir na mwenzake wa Sudan Kusini ,Salva Kiir ili kusuluhisha sintofahamu kati ya nchi hizo mbili jirani

Friday, March 23, 2012

Polisi Ufaransa wamemzuilia mshukiwa

Polisi Ufaransa wamemzuilia mshukiwa

 21 Machi, 2012 - Saa 13:59 GMT
Eeneo anakoishi mshukiwa wa mauaji Ufaransa
Majususi wa Ufaransa wamemkamata mtu wanayeamini kuwa mshukiwa wa mauaji ya watu wanne wakiwemo, watoto watatu wa kiyahudi na mwalimu wao.
Mshukiwa huyo pia anaaminika kuwaua wanajeshi watatu.
Kwa mujibu wa kituo cha televisheni BFM, wametoa tangazo kumtaja mshukiwa huyo wakisema kuwa amezuiliwa ndani ya jengo lenye nyumba nyingi ambalo walilizingira tangu ashubuhi ya leo.
Muhammed Merah, ana umri wa miaka ishirini na nne, raia wa Algeria
Wakati mmoja mshukiwa huyo alitupa nje bunduki moja ingawa waziri wa mambo ya ndani Claude Gueant, anasema mtu huyo angali amejihami vikali.
Bwana Merah alizungumza na polisi wanaomshawishi mtu huyo kujisalimisha lakini baadaye akaodnoka kwenye eneo hilo.
Watu wengine wanaoishi katika jengo hilo wamehamishwa.

Unbeaten super lightweight Vernon Paris boxes with a bullet an inch from his spine Kevin Iole

Unbeaten super lightweight Vernon Paris boxes with a bullet an inch from his spine

Vernon Paris (left) is considered one of boxing's rising stars and was signed by Don King in 2011.
Carlos Baeza/BoxinginLasVegas.com
Unbeaten boxer Vernon Paris carries two bullets with him everywhere, a sobering reminder of how quickly a bad decision can turn into a life-threatening moment. He has no choice because the bullets are lodged in his groin and back, the latter so close to his spinal cord doctors won’t remove it.
A third bullet hit him squarely in the back of the head that day in 2006. Paris hit the ground in the back of an old, abandoned house on Detroit’s west side. He was disoriented, but looked up at the sky and realized he was still alive.
His first thoughts weren’t of fear, or dread, about the consequences of being shot multiple times. Rather, the promising young boxer was angry he hadn’t listened to his father.
“The first thing that popped into my head was, ‘Pops just told me not to hang with these people,’ ” he said. “He had just told me, and then I let them get me. I let them get me. I was hit in the back of the head, and I thought I was done, and I said to myself, ‘I should have listened to Pops.’ ”

Paris, 24, has survived a tumultuous life to make it to a point where, on Saturday in Brooklyn, N.Y., on the NBC Sports Network, he’ll fight ex-champion Zab Judah in a 12-round bout for the No. 1 contender’s spot at super lightweight.
It’s been quite a career. Paris is 26-0 with 15 knockouts and three no contests, moving him to within a win over Judah from getting a shot at the International Boxing Federation 140-pound title.
Carlos Llinas, who signed him to a promotional contract on the boxer’s 18th birthday, is convinced Paris’ indomitable will to win will lead him to a title. Llinas calls Paris his “Miracle Man,” and said every time he hears Paris speak, he thinks of some crazy episode or another from his life.
It’s a movie, waiting to be told, though it’s up to Paris now to give it the happy ending.
“You know, Vernon is a talented guy and if he came from different circumstances and had that powerful promoter and the connected people around him taking care of him, he’d already have a championship and done who knows what in boxing,” Llinas said. “We’ve had some very big fights, fighting on national TV and winning, and now we’re fighting to be No. 1 in the world.
“But the lows this kid has had, man. The lows were like nothing I’ve ever seen, or could imagined. Forget about getting close to getting the title, I can’t believe that Vernon is still here and talking to you today. That’s as big of a miracle as anything.”

It was July 25, 2006, and Paris was 18 years old. He was an unbeaten boxer with dreams of glory that seemed about to die with him in the back of a crumbling home in one of the country’s most notorious neighborhoods.
[ Also: Floyd Mayweather Jr. quietly pays the bills for a baby with a serious heart defect ]
Paris had talent – lots of it – but there had always been questions about his dedication and commitment. He lived in one of the most crime-ridden areas in the country, where shootings are a way of life, and the police seemed powerless to stop it.
Llinas signed him amid a slew of skepticism.
“When I signed him, so many people came up to me and said, ‘Why would you do that? He’s going to be dead or in a jail cell in six months,’ ” Llinas said.

Wanajeshi watangaza mapinduzi Mali

Wanajeshi watangaza mapinduzi Mali

 22 Machi, 2012 - Saa 09:07 GMT
Wanajeshi waasi wametangaza katika televisheni ya taifa ya Mali kuwa wamechukua udhibiti wa nchi, saa kadha baada ya kuvamia kasri ya rais.
Wanajeshi walioasi wanasema kuna marufuku ya kutotoka nje katika nchi nzima na kwamba katiba haitatumika kwa sasa.
Bamako
Marufuku kutoka nje nchini Mali
Siku ya Jumatano wanajeshi hao walifyatuliana risasi na wanajeshi watiifu kwa serikali.
Wanasema serikali haijawapa silaha za kutosha kukabiliana na waasi wa jamii ya Tuareg.
Tayari walikuwa wamechukua udhibiti wa kituo cha taifa cha redio na televisheni na kusitisha matangazo.
Baada ya saa kadha ya kuonyesha picha za nyimbo za wanamuziki wa Mali, kundi la wanajeshi likaonekana kwenye televisheni mapema siku ya Alhamisi, wakitambulishwa kama "Kamati itakayorudisha Demokrasia na kutuliza hali katika nchi".
Msemaji wa waasi hao, aliyetajwa kwa jina la Luteni Amadou Konare, alisema sasa wamemaliza "utawala usio thabiti" wa Rais Amadou Toumani Toure.

Wednesday, March 21, 2012

Mitt Romney seeks to make Illinois victory into 2012 campaign turning point

Mitt Romney seeks to make Illinois victory into 2012 campaign turning point

Mitt Romney waves to a crowd in Schaumburg, Ill., Tuesday, March 20, 2012. (Steven Senne/AP)
Shortly after he wrapped up his victory remarks, Mitt Romney emailed out a fundraising appeal to his supporters with a telling subject line: "Time to close"
It reflects both the frontrunner's wishful thinking that Rick Santorum, Newt Gingrich, and Ron Paul would pack up and go home and the Romney campaign decision to become more assertive about declaring the former Massachusetts governor the presumptive GOP nominee.

Click image to see more photos

AP Photo/Steven Senne
"I think it is another sign that the Republican Party is uniting behind Mitt Romney's candidacy," senior Romney adviser Eric Fehrnstrom told CNN of his candidate's victory in Illinois. "At some point the reality is going to set in that Mitt is the all but certain nominee," he added.
Irrespective of how Santorum, Gingrich, and Paul plan to move through the primaries and caucuses on the calendar from now until June, the Romney campaign is shifting into victory mode. Romney no longer wants to be perceived as the weak frontrunner who cannot win the hearts and souls of the voters at the core of his own party--his campaign is pushing Romney as the experienced and prepared contender ready to defeat President Obama, particularly when it comes to righting the American economy.
If you watched Ann Romney and her frontrunning husband Mitt deliver their victory remarks in Schaumburg, Illinois on Tuesday night in front of a ballroom of supporters, you might be wondering where the extraordinarily wealthy and out-of-touch elite CEO had gone.
Of course, that is the funhouse mirror image of Romney that President Obama and his team have spent the better part of the last year trying to sear into the minds of the American voters.
Instead, you saw a doting wife who used "fix it" no fewer than three times in the span of minutes when describing what her husband would do to Washington and the economy if he were to win the White House.
Romney, meanwhile used his victory remarks to drive home the image of a deeply experienced businessman who learned the ins and outs of the American economy through successes and failures in the private sector.
"You can't learn that teaching constitutional law at the University of Chicago," Romney said standing 40 miles away from President Obama's former classroom.
Romney also sought to wrap his message of economic competence in Reaganesque "city on a hill" style imagery. Innovation and entrepreneurship are not just at the heart of a robust recovery, he said, but also at the core of the "American dream."
But Tuesday night's victorious, economic champion Mitt Romney is not the one presented in the bulk of the campaign coverage. And changing that may prove Romney's greatest challenge as he attempts move from the primaries to the general in 2012.
He has yet to prove his ability at driving a positive message that both illustrates his vision for the future while simultaneously becoming the larger public story of Mitt Romney.
It is, no doubt, challenging to close down a nomination race while your competitors are still running, but Romney and his team have a far greater challenge: upending a narrative built by his Democratic opponents that has solidified in the minds of voters.
For that reason more than any other, the Romney campaign needs to successfully convince all Republicans that it is indeed "time to close."
David Chalian is the DC Bureau chief for Yahoo News.
More popular Yahoo! News stories:
Mitt Romney wins Illinois primary
Obama celebrates extended St Patrick's Day, honors Irish Prime Minister
Paul Ryan: GOP presidential candidates will fully back proposed budget
Want more of our best political stories? Visit The Ticket or connect with us on Facebook, follow us on Twitter, or add us on Tumblr. Handy with a camera? Join our Election 2012 Flickr group to submit your photos of the campaign in action.