Sunday, November 18, 2012

Israel yalenga ofisi za Hamas Gaza


Israel yalenga ofisi za Hamas Gaza

 17 Novemba, 2012 - Saa 14:05 GMT
Jeshi la wanahewa la Israil limeshambulia kwa mabomu ofisi ya waziri mkuu kutoka chama cha Hamas pamoja na jengo la baraza la mawaziri kwenye ukanda wa Gaza, katika siku ya nne ya mashambulio.
Gaza  ikishambuliwa

Wapalestina 39, wakiwemo watoto kadha, wameuwawa tangu mashambulio hayo kuanza siku ya Jumatano.
Wapiganaji wa Gaza wameendelea kurusha makombora dhidi ya Israil, baada ya kulenga miji ya Tel Aviv na Jerusalem hapo jana.
Hamas imeomba madawa kutoka nchi za Kiarabu.
Israel inasema mashambulio yake yameleta uharibifu mkubwa katika vituo vilioko chini ya ardhi ambako makombora ndiko yanakorushwa.
Waziri wa mashauri ya Nchi za Nje wa Tunisia, ambaye alitembelea eneo la Gaza Jumamosi, alitoa wito kwa viongozi wa Kiarabu - wataokutana baadae mjini Cairo - kumaliza kile alichoita uhasama wa Israel.

Mkeo aweza "kunusa" uoga wako


Mkeo aweza "kunusa" uoga wako

 16 Novemba, 2012 - Saa 22:20 GMT
Je? Unafahamu kuwa Wanawake wanauwezo mkubwa zaidi wa kunusa.
Wenyewe hawajui lakini, mwamke anaweza kunusa hasira, naam ikiwe mumewe ana hasira hata akikaa kimya , mkewe atakuwa wakwanza kujua kwamba mmmh! leo kumeharibika.
Mwanamke pia anaweza kunusa uogoa wa mumewe.
Dr Gün Semin wa Utrecht University, Ujerumani anasema hii ni kutokana na jasho la mwanamume!
Utafiti unaonyesha kuwa jasho analotoka mwanamume linatuma ujumbe katika kiwili wili cha mwanamke na kumuambukiza hali unayosikia bila ya wewe kumuambia kitu.. Jasho lako linatuma ujumbe kwa mkeo au kwa mchumba wako.
Ukiwa wewe mwanamume umeshutshwa na kitu au umebabaika au umeogopa au ana hasira. Jasho lako litasema. Na System ya mama itapokea ujumbe!
Dr Gün Semin wa Ujerumani anasema mwanamume akikasiria anatoa jasho lenye kemikali aina fulani. Akiwa na uoga anatokwa na jasho aina tofauti.
Ndio maana mkeo au mchumba wako atakuuliza kuna nini lakini? Hata ukikataa mwili wake unamuashiria kwamba lazima kuna kitu. Sio ati wao ni wajanja sana lakini jasho lako limetoa chembechembe fulani kulinagani na hali yao na hivyo kutuma ujumbe wa siri kwa system ya mama.
Ni majaliwa ya wanawake hayo.
....
Kipepeo aweza kunusa mpenzi wake akiwa mbali
Vipepeo wanawake pia wanamajaliwa ya kuweza kunusa vitu.
Wanasayasi wanasema kipepeo ana uwezo wa kunusu kipepeo mchumba wake au anayemfaa hata akiwa maili 7 au nani hivi.
Kipepeo atanusa nakujua kiboko yangu anakuja japo yuko kilomita nyingi.
Nani mwenye uwezo mkubwa zaidi wa kunusa? Kwa wanyama ni Dubu, yaani bear, sio teddy bear.
Baharini ni papa. Papa anaweza kunusa hata damu amboyo bado ingali ndani ya samaki mwengine. Ni papa huyo.
..............
Wanasayansi wanasema kuwa wanawake ni viumbe wa ajabu!
Katika mahusiano ya kawaida, urafiki tu wa kimapenzi, boy friend na girl friend wanawake bila ya wao kujua huvutiwa na watu wakaidi, watukutu watu wenye miguvu kuvu, misuli misulu, watu wenye vimo virefu kwa kiingereza hao wabajulikana kama Alfa men.
wabasayansi wanasema watu wenye vurugu vurugu , watundu wanauwezo mkubwa wa kutongoza.
Pengine hii nikutokana na sababu ya kutoogopa kukataliwa.
........
Lakini katika ndoa wanawake bila ya wao hata kujijua huvutiwa na watu wadhaifu , watu waungwana, wastaarabu, wenye hekima watu wenye vimo vya wastani.
Wanawake wanapenda Alpha men kama wapenzi tu
Hata enzi za adamu na hawa mambo yalikuwa vivyo hivyo.
......
Watafiti wa maswala ya kijamii na mahusiano wanasema kuwa kwa akina dada wengi katika ndoa huvutiwa na watu wasio na misuli, wenye vimo vya wastani au hata wafupi - hawa kimombo wanajulikana kama Beta men- B-E-T-A, Beta, baada ya Alfa , kuna Beta katika alphabeti za kirumi.
Kwanini ieve hivyo.
Sayanmsi ya mahusiana inasema kuwa watu wasiokuwa nguvu, vimo vya kutisha au misulu eti, eti wanajali sana familkia zao na wake zao.
Maelezo ni kwamba
kwa kuwa hawaezi kushndana katika ulimwerngu wa mahaba kwa kutumia nguvu na kifua basi mwenyezi mungu amewapa sifa za kuwa wakarimu, wenye kutoa, kujali wapenzi wao , na kama njia ya kutinza ndo zao Mungu amewapa watu sampuli hiyo uwezo wa kuwa waaminifu. Wasipo kuwa hivyo kuna hofu ya kutorokwa!
Ni sayansi ya mahusiano!
.........
Jee unajua kuwa kufanya kazi usiku ni hatari kwa akina mama? Na inaweza kusababisha kifo?
Utafiti uliofanywa na madaktari nchini Uingereza umegundua kuwa wanawake wanaopendelea kufanya kazi usiku wanahatari ya kupatikana na sartani ya matiti- breast cancer.
Katika kichwa cha Kazi za usiku zinasababisha vifo 500 kila mwaka nchini Uingereza utafiti hunasema shift za usiku ni hatari kwa akina amma.
Dr Lesley Rushton, wa Imperial College Mjini London anasema Mawanamke akifanya kazi ya usiku kwa wastani ya siku tatu kwa wiki kwa miaka sita - anakaribisha kansa ya matiti.
Kufanya kazi usiku au kukosa usingizi kwa akina mama kunatatiza utengenezaji wa homoni ya ya MELATONI, hii ni chembechembe inayosaidia usingizi na hii inasadikiwa kuwa na uwezo wa zuia kansa.
................
Wanasayansi wana mambo!
Dawa ya kuzuia nyumba ndogo
Sasa kumegunduliwa dawa aina ya homoni inayoweza kuwazuia wanaume kwenda nje, au kuwa na uhusiano wa pembeni,
Dawa hii iliyovumbuliwa Ujerumani inaitwa FIDELITY HORMON. Dawa ya uaminifu! Au kampuni hiyo ya ujereumani imeipa dawa hiyo jina la CUDDLE DRUG! Dawa ya kukumbatiana.
Dr René Hurle­mann, of Bonn University nchini Ujerumani anasema mwanamume akipewa dawa hii ya kumeza huyeyuka na kuingia katika damu, hivyo mwanamke mrembo akipita karibu, basi mume analazimika kukaa umbali wa inchi sita . Mume bila kujua damu yake itakuwa haipatani na mwanamke mwengine mbali na mkewe.
Mwanamke huyo akiwa mrembo zaidi , ndio dawa inafanya kazi vizuri zaidi. Ni FIDELITY HORMON. Tembe za uaminifu.
.....
iPad inaweza kusababisha maradhi ya moyo
The iPad ni komputa ndogo ya mkoni hii inatengezwa na kampuni ya Apple Ipad yakanzwa ilinza kuuzwa tarehe 3 April mwaka 2010 NA iPada ya kisasa zaidi imetolewa tarehe 2 novemba mwaka huu wa 2012.
Ipada inaweza kupiga picha ya video, picha ya kawaida , kucheza muziki , kuzuru mtandao na mambo mewngi tu.
Lakini ujajua kwamba ukiwa na tabia ya kutumia Ipad usiku usiku huenda ukapatikana na matatizo ya moyo au msongo au kudorora kwa afya, yaani depression?
Utafiti pia unasema kuwa ukiwa na tabia ya kuangali televisheni hadi usiku mpevu kila mara basi unakaribisha maradhi ya moyo au depression.-kudorora kwa afya.
Profesa Samer Hattar anasema wa Marekani anasema utafiti umegundua kuwa televisheni na komputa ya iPad inatoa mwanga usistahili wakati mwili unahitajika kulala.
Hivyo kutumia iPad na televisheni usiku sana inaweza kusababisha maradhi ya moyo au mtu kukosa raha maishani au kutompenda starehe au mkuwa mtu pweke, kutumia iPad au televsiheni kila mara usiku sana kunasababisha upweke.
Hii bi BBC na Mimi ni Odhiambo Joseph

Jeshi la MONUSCO laingia kati Goma

Jeshi la MONUSCO laingia kati Goma

 17 Novemba, 2012 - Saa 16:46 GMT
Helikopta zenye silaha za Umoja wa Mataifa zimeshambulia maeneo ya wapiganaji mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, huku mapambano yanaendelea baina ya jeshi la Congo na kundi la wapiganaji wa M23.
Mpiganaji wa M23 kaskazini ya Goma

Mtangazaji Fred Mtoi afariki dunia


Mtangazaji Fred Mtoi afariki dunia

 17 Novemba, 2012 - Saa 16:25 GMT
BBC inasikitika kutangaza kifo cha mtangazaji mwenzetu Fred Mtoi ambaye alifariki Ijumaa usiku mjini London.
Fredd Mtoi
Fred alianza kazi ya utangazaji katika Radio Tanzania kabla ya kuja Ulaya kwa mafunzo.
Amekuwa akifanya kazi huku akiendelea na masomo ya shahada ya pili ya masters kwenye digital media katika chuo kikuu kimoja cha London.
Alishiriki katika vipindi muhimu na vilivyopata sifa hasa vya sanaa, utamaduni na jamii kutokana na kuwafahamu wakaazi wengi wa London hasa wenye asili ya Afrika Mashariki.
Alishiriki piya katika matangazo ya kawaida ya habari ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC.
Wenzake katika Idhaa ya Kiswahili ya BBC wanamkumbuka Fred kuwa mtu mwema, mpole, mchangamfu na anayepatana na wote, na ambaye alikuwa mtangazaji tulivu na akishikilia kazi lazima ahakikishe kuwa ameimaliza vema iwezekanavyo.
Matayarisho yanafanywa kusafirisha mwili wake hadi Tanzania.

M23 wakaribia Goma

M23 wakaribia Goma

 18 Novemba, 2012 - Saa 12:39 GMT
Wapiganaji wa mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo wanasema wako katika vitongoje vya Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.
Mwanajeshi wa serikali ya DRC nje ya Goma
Hayo yamethibitishwa na wakaazi wa Goma ambao wamesema kuwa jeshi la serikali na wapiganaji wa M23 wanapambana karibu na uwanja wa ndege.
Jumamosi, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilitaka kundi la wapiganaji la M23 kuacha kuelekea mji wa Goma, na nchi nyengine ziache kulisaidia kundi hilo.
Katibu Mkuu, Ban Ki-Moon, alimsihi Rais Kagame wa Rwanda atumie madaraka yake kuwazuwia wapiganaji hao.
Rwanda inakanusha kuwa inawasaidia wapiganaji hao.
Naibu Katibu Mkuu wa shughuli za kuweka amani za Umoja wa Mataifa, Herve Ladsous, aliulizwa Jumamosi kama M23 wanasaidiwa na nchi nyengine katika mapambano yanayoendelea.
Alisema: "Hatuwezi kuthibitisha au kukanusha kama Rwanda ilihusika hasa na mashambulio hayo ya M23.
Lakini naweza kusema kuna ripoti kuwa washambuliaji wa M23 wana silaha na zana za kutosha."

LUIS SUAREZ AENDELEZA MAKALI YAKE - AIONGOZA LIVER KUIPA THALATHA KWA MTUNGI WIGAN

NORWICH YAMPA MAN UNITED DOZI DOZI ILE WALIYOMPA ARSENAL

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
N1-0M www.fasthighlights.com *by fasthighlights-2013*

OLIVIER GIROUD KIWANGO, ARSENAL WAKIISAMBARATISHA SPURS KWA MIKWAJU MITANO KWA MBILI

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 5 hours ago
A5-2T www.fasthighlights.com *by fasthighlights-2013*

WEST BROM WAIPA SOMO CHELSEA - WAITANDIKA 2-1

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 10 hours ago
West Brom vs Chelsea 2:1 GOALS HIGHLIGHTS *by UCL2410*

LUIS SUAREZ AENDELEZA MAKALI YAKE - AIONGOZA LIVER KUIPA THALATHA KWA MTUNGI WIGAN

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 10 hours ago
Liverpool 3 -0 Wigan All Goals & Highlights (17... *by kofiswag*

MAN CITY YAMTANDIKA ASTON VILLA 5 BILA NA KUKAA KILELENI EPL

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 10 hours ago
Manchester City 5 0 Aston Villa hoofoot... *by hoofoot*

LIONEL MESSI AONGEZA MAWILI BAADA YA KUMPITA PELE - BARCA IKICHINJA 3-1

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 10 hours ago
FC.Barcelona 3 1 Real ZARAGOZA hoofoot... *by hoofoot*

REAL MADRID YAZIDI KUWACHIMBIA KABURI AKINA LLORENT - WAWAPIGA KIGANJA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 10 hours ago
Real Madrid 5-1 Athletic Bilbao *by goalsarena2012*

Jeshi la MONUSCO laingia kati Goma

BBCSwahili.com | Mwanzo - 19 hours ago
Helikopta za Umoja wa Mataifa zimetumwa kushambulia wapiganaji kaskazini ya Goma, mashariki mwa DRC

Mzozo kati Newcastle na Senegal

BBCSwahili.com | Mwanzo - 19 hours ago
Kuhusu mchezaji wake Papiss Cisse

Arsenal yaipepeta Tottenham 5-2

BBCSwahili.com | Mwanzo - 20 hours ago
Arsenal leo imeilaza Tottenham mabao 5-2 katika mechi ya iliyochezwa katika uwanja wa Emirates.

Mfungwa wa kisiasa afa gerezani Tunisia

BBCSwahili.com | Mwanzo - 20 hours ago
Mfungwa wa Tunisia aliyekematwa mwezi Septemba afariki baada ya kususia chakula

Sierra Leone yafanya uchaguzi mkuu

BBCSwahili.com | Mwanzo - 21 hours ago
Wananchi wengi wamejitokeza mapema kupiga kura kwenye uchaguzi wa rais na wabunge nchini Sierra Leone

Mtangazaji Fred Mtoi afariki dunia

BBCSwahili.com | Mwanzo - 22 hours ago
Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Fred Mtoi afariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi

Israel yalenga ofisi za Hamas Gaza

BBCSwahili.com | Mwanzo - 22 hours ago
Israel yaendelea kushambulia Gaza kwa ndege, ikilenga ofisi za serikali

MCHEZAJI WA UJERUMANI AAMKA KUTOKA KWENYE COMA BAADA YA MWEZI 1

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 1 day ago
Klabu ya Bundesliga Hoffenheim imesema kiungo wake Boris Vukcevic ameamka kutoka kwenye coma, mwezi mmoja baada ya kujeruhiwa na ajali ya gari. Vukcevic aliwekwa kwenye coma baada ya kufanyiwa upasuaji kufuatia ajali ya gari aliyopata tarehe 28 mwezi wa September, gari yake ilipongana na gari lingine kubwa. Hoffenheim inasema kwamba kiungo huyo mwenye miaka 22, raia wa Ujerumani alipata fahamu masaa yaliyopita na kuweza kuzungumza na ndugu zake, lakini klabu hiy imesema kwa muonekano wa jeraha lake kichwani alilopata kwenye ajali ni vigumu kutoa utabii wowote juu ya upataji nafuu... more »

KILIMANJARO MARATHONI 2013 YAZINDULIWA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 1 day ago
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Bi. Kushilla Thomas akishirikiana na Mkurugenzi Msaidizi wa Michezo wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Bi. Juliana Yassoda kukata utepe kuzindua rasmi mbio za Kilimanjaro Marathon 2013 zinazotarajiwa kufanyika Moshi mwezi Machi mwaka 2013. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. (Picha: Executive Solutions)

Mkeo aweza "kunusa" uoga wako

Kutumia iPad usiku usiku kunadhoofisha afya

Wash United kuungana na Taifa Stars kuweka mazingira na Usafi ‘salama’

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 1 day ago
*Mpira wa miguu unaweza kufanya nini kuhusu mazingira na usafi?* Zaidi ya watu bilioni 2.6 duniani wanaishi bila ya kuwa na vyoo. Barani Afrika, magonjwa ya kuhara yanayosabishwa na ukosefu wa vyoo na usafi ni hatari zaidi na ndio yanayosababisha vifo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, hii ni zaidi ya magonjwa kama Ukimwi, Malaria na surua ikifuatia. Takwimu kutoka mashirika ya UNICEF na WHO zinaonyesha kuwa nchini Tanzania zaidi ya asilimia 90 ya watanzania wanaishi katika mazingira machafu, na asilimia 12 hawana vyoo wala maji. Matokeo yake zaidi ya watoto 24,000 nc... more »

WACHEZAJI 20 WALIOITEKA ULAYA KWA KUZISAIDIA TIMU ZAO

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 1 day ago
Kabla ya kuwataja wachezaji bora 20 ambao wameiteka Ulaya, napenda kuthamini mchango wa wachezaji hawa katika timu zao Yaya Toure, Xavi, Mario Gotze, Wayne Rooney, na Hazard. Hawa wamekuwa kwenye viwango bora kabisa msimu huu huku wakiziwezesha timu zao katika kupata matokeo bora. *Frank Ribery (20) * Mfaransa huyu amekuwa akijitolea kila kitu kwa ajili ya klabu yake ya Bayern Munchen. Licha ya matatizo yake ya kugombana na winger mwenzake wa Bayern, Arjen Robben mara kwa mara, Ribbery amekuwa bora mara zote anapoingia ndani ya uwanja. Hivi karibuni Ribbery alikaririwa akisema ... more »

MSIKILIZE RAGE ALIPOONGEA NA WAANDISHI - KUWAFUNGIA WANACHAMA WA TAWI LA MPIRA PESA

Shadaka at Shaffih Dauda in Sports. - 1 day ago
VIDEO KWA HISANI YA ITV

Monday, November 5, 2012

Wachina walitumia kondom za utumbo


Wachina walitumia kondom za utumbo

 28 Septemba, 2012 - Saa 19:50 GMT

Nani asiyejua Kondom?
Kondom ya Utumbo wa Nguruwe
Nani asiyejua kazi ya Kondom?
Lakini unajua kifaa hicho ambacho siku hizo husambazwa bure kilianza lini na wapi?
Tarehe yenyewe haifahamiki lakini katika karne ya 15 yaani miaka mia 6 iliyopita kondom zilikuwepo na zilikuwqa zinatumika katika bara la Asia.
Miaka mia sita iliyopita Kondom nchini china zilikuwa nizatengenezwa kutumia utumbo au mbuzi au kondoo.
Matajiri walikuwa wakitumia Kondom zilizotengenezwa kwa karatasi ya hariri iliyopakwa mafuta.
Nako nchini Japan Kondom zilikuwa zikitengenezwa kwa magamba ya kobe au pembe za wanyama . Naama pembe ilikuwa ikivaliwa kama kondom..ni huko Japan, miaka mia 6 iliyopita.
Ni katiuka karne iliyopita , mwaka 1900 kondom zilizotengenezwa kwa utumbo wa mbuzi na kondoo hata utumbo wa ngombe zilianza kuenea duniani.
Enzi hizo ilikuwa inatumiwa kukinga magonjwa ya zinaa na kuzuia mimbia isiyotakikana.
.........
Ni kawaida kwa wanawake wengi wakati wa ujazito kuanza kutapika , kuwa ni kichefu chefu ,kuhisi kisunzi au kizunguzungu , kujisikia mnyonge, hasa wakati wa asubuhi. Wazungu wanasema ni Morning sickness.
Wataalam wanasema haina sababu moja. Lakini wanakubali kuwa husababishwa na ongezeko la homoni hasa ya Estrogen katika mwili wa mwanamkea ambayo inaweza kumuongezea , uwezo wa kusikia harufu hasa mbaya. Kuongezeka kwa maji aina ya gastroline.
Na unafahamu kuwa mwanamume.Baba mwenye nyumba pia anaweza kuwa na dalili hizo hizo za ujauzito yaani ?, kizunguzungu,kutapika , kichef chefu , tumbo kufura na kuwa na hasira kama mkewe?
Kwa wakati huu Mike Dowdall , bwana mwenye umri wa miaka 25 kutoka Manchester Uingereza amefura tumbo, anatapika tapika , asubuhi, husikia kisunzi au kizunguzungu na anapenda kula vitu vichachu kama maembe mabichi yalitiwa chumvi au pilipili.
Kwa wakati huu mpenzi wake Amanda Bennett ni mjamzito. Dahili za Mike zilipoanza bi Amanada alichukulia kwamba mpenzi wake ambaye wameishia naye miaka mitatu anamfanyia mzaha au stihizai Eti anamuiga vile anavyo tapika, na kupenda kula kula.
Lakini madaktari kutoka Manchster wanasema Bwana Mike ana ugonjwa wa mimba bandia. Wao wanaita Couvade syndrome
huu sio uchawi , bali ni ugonjwa unaoweza kuwapata wanaume. Tumbo kufura, kutapika tapika asubuhi, kuhisi kizunguzungu na kupenda kula maembe ya liotiwa chumvi au pilipili.
Mike amekuwa na uja uzito bandia kwa wiki 33 na kama vile tu akina mama walio na mimba , Mike ameongeza uzani au zaidi ya kila 3 na sasa anajihisi mchovu kila mara, kuumwa na mgongo na kwnda haja ndogo kila mara.
Madaktari hao wanasema ugonjwa huu unaweza kusababishwa na ile hali kuwa wasiwasi unaposubiri mkeo kujifungua, au pia kuwa karibu sana na mkeo.
Bi Amanda ambaye ana mimba ya wiki zaidi ya 34 sasa analazimika kumsugua mumewe mgongoni na kiunoni kila siku na kumkanda tumbo lake.
Habari hizo zimeshamiri katika gazeti la The Sun la uingereza.
......
Si hadithi bali ni kweli kwamba , mtu na mkewe wakiishi kwa zaidi ya miaka 25 huishia kufanana!
Asante msikilizaji wa BBC kutoka Tanzania kutukumbusha hao?
ukitaka kuthibitisha hilo hebu mwaangalie bibi na babu, ukiwa wewe ni mtum mzima hebu waangalie wazazi wako wote wawili?
Mwalimu Nyerere
Hebu tazama picha ya Hayati baba wa Taifa wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere na Mama Maria? Unaonaje?
Mama Maria Nyerere
Lakini kitu gani kinasababisha hali hii ya mtu na mkewe kufanana baada ya kukaa pamoja kwa miaka 25 au zaidi?
Waalam wanasema , ikiwa kuna upendo kati yenu, hii itachangia?
kwa vile kwa miaka 25 mume na mke hucheka pamoja , kulia pamoja,wakati wa hupata msiba uhuzunika pamoja , wakati wa matatizo na mihangaiko wanakabiliana nayo pamoja michoro hivi vinasaidia kugeuza shepu na sura au uso wa mtu hivyo mume na mkewe huishia kufanana.
vyakula pia inasaidia kuwafanya wafanane. kwa vile wamkaa pamoja kwa miaka , mume na mkewe hula vyakula aina moja na kukaa mazingia aina moja hii pia inasaidi kuwafanya wafanane.
Ni utafiti uliofanywa na Dr. Zajonc(ZI-onz) akishirikiana na Pamela Adelmann, Sheila Murphy na Paula Niedenthal na kucahpiswha katika jarida la kisayansi la , Motivation and Emotion.
..........
Jee unataka kujua utakapozeeka utafanana vipi?.
Kazi rahisi sana.
Wataalam wakiongozwa na Dr. Zajonc(ZI-onz) wanasema kama wewe nimwanamume hebu muangalie baba mkwe wako, na kama wewe ni mwanamke , muangalie kwa umakini mama mkwe. Urefu unaweza kuwa tofauti lakini sura, utakapozeeka utafanana kama wakwe zako.
.........
nani anataka dola milioni 64 bila kutoa jasho jingi?
nadhani kazi hii itakuwa nyepesi mno kwa jamaa wa Bongo Tanzania, au Mombasa, au Uganda mtuweza?.
Tajiri mmoja nchini Hong Kong ametoa zawadi ya dola milioni 64 za kimarekani kwa mtu yeyote atakaye faulu kumtongoza binti yake bi Gigi Chao na akubali kuolewa nae.
tatizo ni hili bi Chao ni msango, au lesbian mwanamkea nayependelea kufanya mapenzi ya jinsia moja.
tatizo jengine ni kuwa bi Chao mwenye umri wa miaka 33 tayari amefunga ndoa kisiri na mwanamke mwenzake hivi majuzi tu.
sasa basi, ukitaka dola hizo milioni 64 za kimarekani mtongoze, Bi chao , ufaulu kumuondoa katika ndoa hiyo na mwanamke mwenzake na uafaulu kumuoa.
kama unaweza basi niandike katika facebook, BBC swahili.com nikuunganisha na tajiri huyo wa Hong Kong
Jina langu ni Odhiambo Joseph tukutane katika Internet BBCSWAHILI.COM katika Kisa na Mkasa au ungana nami wiki ijayo Mungu akipenda.