Thursday, October 27, 2011

MAITI YA GADDAFI- HII SI HAKI BABISA

Maiti Ya Gaddafi Yawekwa Kwenye Friza la Nyama

NewsImages/6013434.jpg
Gaddafi muda mfupi baada ya kukamatwa
Sunday, October 23, 2011 1:17 PM
Maiti ya aliyekuwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi imewekwa kwenye friza la nyama mjini Misrata na itaendelea kukaa humo kwa siku chache zijazo ili kila mtu aamini kuwa Gaddafi ameuliwa.
Mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi umehifadhiwa kwenye friza la depo la nyama mjini Misrata ambako waziri wa mafuta wa Libya, Ali Tarhouni amesema kuwa itaendelea kuwekwa humo kwa siku kadhaa ili watu wajue kuwa ni kweli Gaddafi ameuliwa.

"Nimewaambia wauweke mwili wa Gaddafi kwenye friza ili watu wajue ni kweli Gaddafi ameuliwa", alisema waziri huyo wa mafuta.

Gaddafi aliuliwa kwenye mji alikozaliwa wa Sirte baada ya kukamatwa akiwa hai alipojeruhiwa kutokana na mashambulizi ya majeshi ya NATO na baadae mashambulizi ya wanajeshi wa baraza la mpito la Libya, NTC.

Kwa kawaida maiti ya kiislamu hutakiwa kuzikwa ndani ya masaa 24 lakini hadi sasa haijulikani ni lini Gaddafi atazikwa kwakuwa kuna mvutano ndani ya NTC juu ya wapi Gaddafi azikwe.

"Hadi sasa hakuna uamuzi uliotolewa juu ya mazishi ya Gaddafi" alisema Mahmud Shamam alipokuwa akiongea na shirika la habari la AFP na kuongeza "Haijulikani kama kama maiti ya Gaddafi itaendelea kuhifadhiwa mjini Misrata au kama itasafirishwa sehemu nyingine".

Viongozi wa NTC hawajaafikiana juu ya mazishi ya Gaddafi lakini hawataki kuona kaburi la Gaddafi linatumika kama alama ya ukumbusho kwa wafuasi wa Gaddafi waliobaki.

Shirika la habari la BBC limeripoti kuwa kuna mipango ya kufanya mazishi ya Gaddafi yawe ya siri huku pia kukiwa na tetesi kuwa huenda Gaddafi akazikwa baharini kama mazishi ya aliyekuwa kiongozi wa Al-Qaeda, Osama bin Laden yalivyofanyika kwenye bahari ya Uarabuni.
  GONGA HAPA KWA PICHA ZA MAITI YA GADDAFI  


    
Mtumie Rafiki Yako

No comments:

Post a Comment