Saturday, December 31, 2011

Hitimisho bila utafiti ni uvivu wa kufikiri II- MAKALA

Hitimisho bila utafiti ni uvivu wa kufikiri II

Maadui hawaitakii mema CHADEMA
Kama tulivyoahidi, wiki hii tunaendelea na sehemu ya mwisho ya makala ya Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa, akimjibu mmoja wa wachangiaji hoja na waibuaji mijadala katika gazeti hili, Mayage s. Mayage.
Mayage angelifanya utafiti angeligundua hoja ya Katiba mpya ilikuwa ndani ya Ilani ya CHADEMA. CCM imeibeba baada ya kushinda uchaguzi kama walishinda na siyo ‘kuiba kura’ (Katiba hairuhusu kuhoji matokeo hivyo hatuna pa kutolea ushahidi wetu). Sisi hatuna shida na hilo.
Tunasisitiza kama wamechukua hoja ambayo hawakuwa nayo waitekeleze vizuri kama ilivyobuniwa na walioibuni. CHADEMA ndiyo iliyoibuni, na kusema...ndani ya siku 100 mchakato wa Katiba mpya utaanza” Hakuna chama kingine chochote kilichosema hivyo kwenye ilani yake.
Ni dhahiri Mayage haelewi, kuwa ‘Mchakato ukiwa mbovu, tunda lake yaani Katiba itakayopatikana itakuwa mbovu’. Wengine tuna uzoefu si wa kusoma tu magazetini bali kushiriki mchakato wa Tume ya Rais ya Jaji Kisanga. Ni hovyo. Ndiyo maana tangu siku ya kwanza nimepinga Tume ya Rais badala ya Tume ya Wananchi itakayoundwa na mkutano wa Katiba.
Mayage haelewi kuwa uchaguzi unaendeshwa kwa Katiba na kuwa haki haitapatikana kama Katiba itaendelea kubeba Chama cha Mapinduzi (CCM).
Ni ndoto kufikiria uchaguzi huru na haki 2015 kama Katiba Mpya haitapatikana. Matukio yote ya wananchi kupigwa mabomu, kuzuiliwa mikutano ya upinzani mara kwa mara, kubadilishwa kwa matokeo ya uchaguzi yote haya ni matokeo ya Katiba mbovu.
Mayage hajui kuwa migogoro mingi kwenye ardhi ni matokeo ya Katiba mbovu! Hajui kuwa robo tatu ya bajeti ya taifa leo inatumika kwenye uendeshaji wa Serikali badala ya mipango ya maendeleo kutokana na Katiba mbovu? Mayage siyo tu hajafanya utafiti, lakini pia si makini katika kujenga hoja zake. Anajipinga mwenyewe mara aseme chama gani kimesimamia hoja zake, mara aseme CHADEMA kinapoteza muda kujadili hoja zenye manufaa kwa Watanzania. Tumuamini kwa lipi katika hali hii?
Mayage sisi tuliisha kumaliza utafiti na udadisi kuhusu Katiba.  Huhitaji kwenda mbali, nenda Ghana na Kenya. Tunayo michakato iliyotumika kupata Katiba na tunazo pia nakala za Katiba zao.
Nani kapotea kati yako wewe ambaye huna hata mfano mmoja na CHADEMA inayofahamu tangu awali nini kinahitajika kupata Katiba mpya!
Tuache ulimbukeni tunapozungumzia maslahi ya taifa. Mayage anaenda mbali kiasi cha kufananisha CHADEMA na “bundi katika msafara wa ndege dhaifu”! Kama yeye alijisikia kutukanwa je, na CHADEMA ambaye si mtu mmoja inajisikiaje na upotoshwaji na matusi ya kiasi hiki?
Ukisoma kwa umakini, kwake Mayage CHADEMA ni “chama cha ovyo” ndiyo maana anawashawishi Watanzania kuanzisha chama mbadala wa CCM.
Mayage amelundika vyama vyote 17 vya upinzani katika kapu moja. Ni kweli kuwa hafahamu CHADEMA ni chama pekee cha upinzani kinachoongoza halmashauri zaidi ya saba? Hajui kuwa CHADEMA imeshindwa kwa idadi ndogo sana katika halmashauri nyingine nane?
Mayage ameshindwa kutambua kuwa CHADEMA ni chama kinachokua kimkakati na vigezo ni vingi chukua idadi ya madiwani ambayo katika uchaguzi wa 2010 imeongeza kwa asilimia zaidi ya 400, mafanikio ambayo hakuna hata chama chochote cha upinzani kimefikia?
Mayage hajui kuwa katika vyama 17 viko ambavyo tangu vianzishwe havijawahi kupata kiongozi hata serikali moja ya mitaa angalau mwenyekiti wa kitongoji, wakati CHADEMA ina maelfu ya viongozi hao?, Mayage ameamua kuzipuuza makusudi kwa malengo anayojua na pia kwa ‘uvivu wa kutokufanya utafiti’ angalau kupiga simu tu kwa wahusika. Madhara yake ni kuwaambia watanzania “..tulivyonavyo sasa (vyama vya siasa/NGO’s). Hivi haoni hata aibu kulinganisha chama kinachoongoza halmashauri zikiwemo Jiji la Mwanza na NGO ambayo malengo yao si kuchukua dola?
Haya siyo matusi tu kwa Watanzania bali kwake mwenyewe aliyejifanya mtaalamu akashindwa kufikisha ujumbe ambao pengine hata mtoto wa shule ya msingi angeliweza kuufikisha vizuri zaidi.
Wanachama,wapenzi na Watanzania wapenda mabadiliko ambao walikuwa hawajagundua dhamira ya Mayage kuanzia makala ya kwanza ni vema wakarudi kusoma makala zake za mwanzo na kuzichambua kwa kina ili kuepuka upotosha uliojificha kwa hoja za kuuma na kupuliza.
Dk. Slaa nisingeliweza kwa namna yoyote kufumbia macho upotoshwaji huu ambao nia na lengo lake ni dhahiri.
Mayage anaonyesha udhaifu mkubwa pale anaposema hajaridhishwa na CHADEMA kwa kushindwa kusimamia hoja moja tu “…ya posho ya vikao kwa wabunge”. Kwani CHADEMA ndiyo inayolipa posho hiyo?
Hajui mgogoro wa sasa wa posho kulipwa kinyemela na jinsi CHADEMA kama chama inavyopiga kelele, hajui jinsi CHADEMA ilivyodai fomu ya mahudhurio ukumbini bungeni itenganishwe na fomu ya posho, na uongozi wa Bunge umekataa kufanya hivyo?
Labda hajui msimamo wa CHADEMA kwa kuwa si mpenda kusoma wala hajui ilani ya CHADEMA kifungu cha 5.5.1 (2 na 6) ya Agosti  2010, kinasema nini.
Lakini sishangai kwa vile anaandika kwa hisia badala ya utafiti. Kama ambavyo hajui pia kuwa kamati kuu ya CHADEMA kila kikao kwa mujibu wa kanuni, inatakiwa kupokea utekelezaji wa programu ya kazi kutoka kwa wabunge na  halmashauri zinazoongozwa na CHADEMA na kila kamati tendaji ya kata inapokea taarifa ya utekelezaji kutoka kwa madiwani wake.
Inawezekana utekelezaji wa mipango katika maeneo yanayoongozwa na CHADEMA unasua sua na kwa maeneo mengine hauridhishi.
Lakini pia angetafiti kidogo angegundua halmashauri zenye uzoefu za CHADEMA zimepiga hatua kiasi cha kuanzisha chuo chake cha waalimu kupunguza kero ya upungufu wa waalimu, kuanzisha chuo cha madaktari (clinical officers) na manesi kupunguza kero ya upungufu wa wataalamu hao na sasa wako mbioni kuanzisha chuo cha kilimo.
Haya yanapatikana tu kwa wenye nia na dhamira ya dhati ya kutaka kujua bila kutoa hukumu mezani. 
RC Mwanza, ma-DC wametuhujumu
Angelifanya utafiti angeligundua jinsi mkuu wa mkoa wa Mwanza alivyoingilia na kuvuruga utekelezaji wa mipango ya Jiji la Mwanza iliyoko chini ya CHADEMA, na vivyo hivyo kwa wakuu wilaya katika halmashauri zingine.
Utafiti ungelimwonyesha kuwa demokrasia kwa wengi wa viongozi wa Serikali iko kwenye midomo zaidi (lip service) lakini yanayoendelea maeneo mengi nchini ni kinyume cha demokrasia. Haya hutayajua kama huna dhamira ya kutaka kuyajua na wala hufanyi utafiti. Ndiyo msingi mkubwa wa ushauri wangu kwa Mayage.
Ni dhahiri Mayage angelifanya utafiti angeligundua maandamano yalivyowaunganisha Watanzania kudai siyo tu haki zao mbalimbali, bali kupaza sauti yao dhidi ya makali ya maisha kama vile sukari, bei ya sembe, mafuta ya kupikia, mafuta ya taa pamoja na kuwakatalia watawala kodi yao isitumike kulipa madeni ya Dowans..
CCM wameiga hawakufanikiwa
Anachokiita Mayage uanaharakati, angelijikita kwenye utafiti angeligundua matokeo yake ni nini hadi CCM wenyewe waliokuwa wakikandia maandamano wakaamua kuyaiga walipojaribu kuandamana Mbeya japo hayakufanikiwa.
Ni dhahiri Mayage amejikita kwenye mbinu mgando akidhani namna pekee ya kufanya siasa ni kufungua matawi kwa mtindo wa CCM.
Kwa kuwa hajafanya utafiti anashindwa kugundua kuwa mbinu za CCM za kufungua matawi haziwezi kufuatwa na chama kingine chochote makini kwa kuwa CCM inatumia mfumo wa dola kufanya kazi zake-watendaji wa vijiji, kata, makatibu tarafa, wakuu wa mikoa, wilaya, kwa ujumla mfumo mzima wa Serikali.
Polisi wanaingilia mipango yetu
Angetafiti angeligundua hata matawi niliyofungua au kufanya yafunguliwe kutokana na ziara ya Katibu Mkuu Jimbo la Mbinga Magharibi (Mbamba Bay), bendera zote zimeshushwa kwa amri ya OCD.
Angelikuwa mtafiti angeligundua chama makini kama CHADEMA kinakumbana na matatizo na vikwazo gani. Angelitoa ushauri jinsi ya kupambana na changamoto hizo nisingelikuwa na sababu ya kumjibu Mayage na au ningemjibu kwa kumpongeza.
Ushauri wake ungetokana na utafiti nina hakika ungewasaidia sana kuwafungua macho Watanzania badala ya kuwapotosha.
Kauli ya Mayage kuwa ‘..Ndani ya siasa wako wanasiasa wazuri tu, lakini hao hawana sauti wala nafasi ya kukielekeza  chama hicho…wenye sauti na ushawishi ndani ya chama ni wanaharakati hali inayokifanya chama kiendeshwe kiharakati kwa asilimia 80..” inathibitisha siyo tu Mayage hajafanya utafiti, lakini pia hajui ‘ABC’ ya siasa na hivyo hastahili kuandikia hata mada za kisiasa.
Chama cha siasa hakiendeshwi kwa ‘influence’, au uanaharakati kama anavyodai Mayage bali na Katiba, kanuni na taratibu za ndani ya chama husika kama zipo.
Kwa faida ya wapenzi wa CHADEMA na Watanzania kwa ujumla CHADEMA inaendeshwa misingi ya Katiba yake, na toleo la mwisho ni la mwaka 2006. CHADEMA ni kati ya vyama vichache vyenye kanuni za uendeshaji, maadili ya viongozi na wanachama, kanuni za uendeshaji wa halmashauri zinazoongozwa na na  CHADEMA ikiwa ni pamoja na serikali za mitaa zilizoko chini ya CHADEMA na hatimaye kanuni za nidhamu ikiwa ni pamoja na kanuni za nidhamu za wabunge, madiwani, na wenyeviti wa serikali za mitaa (na wajumbe wao).
Uamuzi wa CHADEMA hufanywa kupitia Sekretariati ya Kamati Kuu ya chama, Kamati Kuu, Baraza Kuu na mkutano mkuu ambacho ndicho chombo kikuu na cha mwisho cha uamuzi.
Je, ni kuwadi wa maadui zetu?
Kwamba CHADEMA inaendeshwa na wenye ‘influence’ ni kielelezo cha kile nilichokisema kuwa kauli kama hizo zinatoka tu kwa watu wenye uvivu wa kufikiri na kufanya utafiti.
Vinginevyo Mayage ana ajenda yake ambayo hajaiweka hadharani na au ni kuwadi tu wa maadui wengi wa CHADEMA.
Kama nia yake ni njema kama anavyotaka kuonyesha na kuwa anatoa ushauri kwa nia njema, huwezi kumshauri mtu usiyemfahamu, na huwezi kumfahamu mtu kama angalau humtembelei, kumjulia hali, kuomba nyaraka zake na kadhalika.
Wakati ninawapokea waandishi wengi na wa vyombo takriban vyote ofisini kwangu Mayage hajakanyaga wala hajaomba taarifa yoyote iwe kwa simu iwe kwa mahojiano. Huu ni uthibitisho kuwa Mayage ana ajenda zake anazozijua.
Kwa taratibu hizi uanaharakati na “influence” inapata wapi nafasi? Au Mayage anataka kufanya kazi kwa mapenzi ya mtu mmoja mmoja mathalan hiyo asilimia 20 anayoisema?
Je, ni kweli kuwa hiyo influence imepenya kwenye ngazi zote kuanzia sekretariati, kamati kuu, baraza kuu hadi mkutano mkuu. Kama hivyo ndivyo si ndivyo pia jina letu linavyodhihirisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo?
Au Mayage anataka tukiuke misingi ya demokrasia na asilimia 80 ya viongozi waongozwe na asilimia 20? Huo ni ulimbukeni katika siasa na itakuwa ni mfumo mpya unaobuniwa na Mayage katika chama chake kipya anachosema kitakuwa makini”.
Wapenzi na Watanzania kwa ujumla hakuna sababu ya kuwa na hofu na watu wa aina hii, na kwa taarifa yenu wako wengi wasiotutakia mema.
Naamini ufafanuzi huu wa kina utakuwa umewatoa wote hofu wale waliokuwa na shaka baada ya kusoma makala za Mayage.
Naomba nirudie tena katika hitimisho, sina tatizo na wale wote wenye nia ya kuanzisha chama kingine kipya akiwemo Mayage kama nilivyosema ni haki yao ya kikatiba.
Kwa wale ambao tumekwisha kuanza safari ya kuing’oa CCM kupitia ‘meli yetu’ ya CHADEMA, tuendelee na mikakati yetu na kila mmoja akitimiza wajibu wake, Novemba 2015 CCM itaingia kwenye kumbukumbu ya historia kama ilivyo UNIP (Zambia) na KANU (Kenya), tena vyote ni vyama vinavyojulikana kama vyama vya ukombozi.
Mwalimu aliwahi kusema “play your part, it can be done” kila kiongozi wa CHADEMA kwenye ngazi na nafasi yake atimize wajibu wake na apuuze propaganda za maadui zetu zikiwemo hizi za Mayage.

Usingizi na genes zahusiana

Usingizi na jeni zahusiana

 5 Disemba, 2011 - Saa 17:03 GMT
Usingizi
Wanasayansi wanasema mahitaji ya usingizi kwa watu yana uhusiano na jeni zao yaani genes.
Wamegundua kuwa watu wenye aina ya jeni iitwayo ABCC9 wanahitaji takriban dakika thelathini za ziada za usingizi kila usiku kuliko wale wasiokuwa nayo.
Utafiti uliofanywa ulilenga bara la Ulaya na kugundua kuwa humusi ya watu wana aina hiyo ya jeni.
Wanasayansi hao wa Ujerumani na Uingereza wamesema matokeo hayo ni muhimu kwasababu ukosefu wa usingizi unahusishwa na matatizo mengi ya kiafya, kama vile maradhi ya unene na moyo.
Viongozi wa kisiasa, kuanzia mtawala wa zamani wa Ufaransa Napoleon hadi aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Margaret Thatcher walikuwa na sifa ya kuweza kufanya kazi zao bila matatizo licha ya kulala muda wa saa nne au tano tu kila usiku.
Lakini kwa wengine akiwemo mwanafizikia Albert Einstein hata muda wa saa 10 wa usingizi haukumtosha.
Sasa wanasayansi wanasema tofauti hizi katika mahitaji yetu ya usingizi yanaweza kuelezeka kwa kutazama muundo wa jeni zetu.
Walichambua chembe chembe za asidi nasaba DNA kutoka watu 10,000 kote barani Ulaya- na kuzilinganisha na mitindo yao ya kulala.
Walifikia kauli kwamba watu walio na aina ya jeni iitwayo ABCC9 wanahitaji muda wa nusu saa zaidi usingizini ikilinganishwa na wale wasio na aina hiyo ya jeni.
Mtu mmoja kati ya kila watu watano barani Ulaya wanaaminika kuwa na jeni hiyo ya usingizi mwingi.

Mvua kubwa Dar Es Salaam

Michezo

Teknolojia

Kisa na Mkasa

Sikiliza -Tazama

Makala

MAKALA MBALIMBALI-2011

Makala

Mwandishi Wetu

2011 Current Events


2011 Current Events

Here are the key news events of the year organized into three categories: World News, U.S. News, and Business/Science News.
January 2011 Current Events

February 2011 Current Events

March 2011 Current Events

April 2011 Current
Events

May 2011 Current
Events

June 2011 Current
Events

July 2011 Current
Events

August 2011 Current
Events

September 2011 Current
Events

October 2011 Current
Events

November 2011 Current
Events

December 2011 Current
Events


2010 Current Events Current Events
Information Please® Database, © 2011 Pearson Education, Inc. All rights reserved.

More on 2011 Current Events from Infoplease:



Read more: 2011 Current Events — Infoplease.com http://www.infoplease.com/news/2011/current-events/#ixzz1i7DO7rH0

Kwanini Mkulima Mwamwindi alimpiga risasi RC Dk. Kleruu? Sehemu ya III na IV

 

Kwanini Mkulima Mwamwindi alimpiga risasi RC Dk. Kleruu? III

NAKUMBUKA alitunyoshea mkono akiwa anatabasamu. Tulizungumza kwa kushangaa, tukajiuliza; jamani hivi Serikali leo imempa Said Mwamwindi gari atembelee? Yakafuata yaliyofuatia. Maggid, ninayo mengi ya kukusimulia kwa yaliyotokea katika wakati ule….” Anasema Mzee Nzowa. Endelea kusoma simulizi hii katika sehemu yake ya pili.
“ Ndiyo, nilimfahamu Said, na jina lake hasa aliitwa Said Abdalah Siulanga Mwamwindi. Nyumba ya baba yake ilikuwa pale Mshindo karibu na ukumbi wa Welfare. Baba yake aliwahi kuwa Jumbe enzi  za ukoloni.  Kwa kweli Said alikuwa ni  mtu wa kilimo na nakumbuka alianzia kwenye magari. Alikuwa dereva kabla hajaenda kufyeka mapori ya kilimo kule Isimani.”
Je, unakumbuka wajihi wa marehemu Said Mwamwindi?
“Ah, yule bwana alikuwa pande la jitu. Mrefu na aliyeshiba hasa. Ukimwona utasema huyu jamaa amekaa kiutemi-utemi. Yaani, unavyoomwona mwanae, Amani Mwamwindi sasa, ndivyo kwa kiasi kikubwa alivyoonekana Said Mwamwindi. Wamefanana sana."
Na je, Dk.Kleruu, alikuwa mtu wa namna gani, wajihi wake na mengineyo?
”Alaa, Dk.Kleruu. Tulikuwa vijana wakati ule, na yeye alikuwa Mkuu wa Mkoa kijana hapa Iringa. Nafikiri alichukua nafasi ya Bw. Chamshama. Alikuwa mfupi kidogo. Ila bwana, alikuwa machachari sana . Nikisema ’machachari’ nadhani unanielewa.
Haraka sana tuliona dalili kuwa Dk.Kleruu asingekuwa na wakati mzuri hapa Iringa.
Alianza mapema sana kuonyesha tabia za ubwana na hata kunyanyasa aliowaongoza. Na katika hao aliowaongoza, kulikuwa na watu wazima waliomzidi umri.  Watu wenye hekima na busara kumzidi yeye, ingawa hawakusoma elimu ya darasani.”
Je, unaweza kutoka mfano wa ’ubwana’ mkubwa wa Dk.Kleruu aliouonyesha wakati huo?
”Iko mifano mingi, na ukweli Dk.Kleruu alisemwa vibaya katika midomo ya watu hapa Iringa. Ilifika mahala dereva akilipiga overtake gari la Dk.Kleruu hapa Iringa, basi, atasimamishwa na anaweza kuzabwa vibao na Kleruu mwenyewe. Aah! Jamaa yule alikuwa mbabe bwana!” Anasema Mzee Omary Nzowa huku akicheka kwa sauti. Kisha anaendelea.
”Unajua Dk.Kleruu alitokea Mtwara kabla ya kuja Iringa. Sasa kuna wakati alitamka; 'Hamnijui mimi, kawaulizeni watu wa Mtwara!' Sasa hayo si maneno ya kuwaambia watu wa Iringa, na hata mahali pengine popote,” akisimulia zaidi.
”Na nikwambie kitu kimoja Maggid, muhimu katika maisha ni kuishi vema na watu. Hata kama ni kiongozi, huwezi kufanikiwa katika kazi yako kama huna mahusiano mazuri na unaowaongoza. Na hata katika maisha ya kawaida, unaweza kuingia katika misukosuko isiyo ya lazima kama huna mahusiano mazuri na wenzako katika jamii.
”Nitakupa mfano hai unaonihusu mimi. Mwishoni mwa miaka ya 50 nilikamatwa nyumbani kwa kutokulipa kodi ya kichwa. Tulikuwa bado kwenye utawala wa mkoloni. Nilikuwa nadaiwa shilingi saba tu. Sikuwa nazo.
”Basi, nikaambiwa na askari wa kodi tuongozane hadi ofisini kwa DC. Tena walinifunga kamba mikononi. Nilifahamu, huko kwa DC ningeishia kuchapwa bakora na hata kuwekwa ndani. Unajua Maggid enzi hizo damu ilikuwa ikichemka na sisi vijana ndio tuliokuwa tukionekana kuiunga mkono TANU, ” ananiambia Mzee Nzowa akikumbuka enzi za ujana wake.
”Sasa basi, wakati tunakwenda kwa DC, niliwaomba sana wale askari wa kodi. Walikuwa Waafrika wenzetu. Nikawaambia, jamani ee, tafadhali tupite njia hii ya sokoni. Ni soko lile la zamani ambalo mpaka leo hii bado linatumika. Askari walikubali wakidhani nimechagua mwenyewe njia nitakayoonekana na watu na hivyo kujidhalilisha mwenyewe. Kumbe, mimi nilikuwa na maana yangu.
Tulipofika eneo la sokoni nikasikia jamaa zangu wakiuliza kwa sauti; ” Omary shida gani?”. Nikajibu kwa sauti; ” Kodi, shilingi 7!”. Basi, huwezi kuamini, hata kabla sijamaliza soko, vijana wale wa sokoni walichangishana. Shilingi saba zikapatikana. Kodi ile nikalipa na nikaachiwa huru. Pointi yangu hapo ni umuhimu wa mahusiano mema na watu.”
Je, unafikiri ni kwanini Dk. Kleruu alipata tabu sana kufanya kazi na watu wa Iringa?
Anasema Mzee Nzowa: ” Mi nadhani Kleruu, kwa jinsi alivyokuwa, angepata tabu kufanya kazi mahali po pote pale. Tatizo ni ile hali ya kutanguliza ubwana na kuwadharau wananchi. Hakika wakati ule Mwalimu Julius Nyerere alipata tabu sana na namna ya ku-deal na viongozi kama akina Kleruu. Kumbuka ,Tanzania kama nchi ilikuwa taifa changa sana. Hatukuwa na wasomi wengi. Nilimfahamu Nyerere, hili la Kleruu lilimsumbua sana Mwalimu.
”Nikwambie Maggid, Ujamaa na Kujitegemea kama itikadi na sera za Mwalimu haukuwa tatizo. Tatizo lilikuwa kwa baadhi ya viongozi waliopewa dhamana ya utekelezaji. Hawa hawakuwa wanasiasa, wakati mwingine walionekana kama Wanyapara. Mwalimu wakati ule hakujua kila kitu kuhusu watu aliowateua kumsaidia.
”Ni kweli Mwalimu alitia saini hukumu ya kunyongwa kwa Mwamwindi, lakini naamini hakufurahia, bali hali ya wakati ule ilimlazimisha kufanya vile.
”Sisi tuliomfahamu Mwalimu tunajua kuwa hukumu ile ni moja ya maamuzi magumu yaliyomsononesha sana Mwalimu. Unajua wakati ule kuna Wakuu wa Mikoa waliojenga hoja, kuwa kama Mwamwindi kwa tendo lile asingepata adhabu ile, basi utendaji wao wa kazi mikoani ungekuwa mgumu. Ndiyo, hoja hizo ziliibuka. Kwa kiongozi wa nchi ni mtihani. Siyasemi haya kumtetea Mwalimu bali ni kutambua ukweli kuwa Mwalimu alikuwa ni binadamu kama wewe na mimi.”
Unasema ulimfahamu Nyerere na kwamba unaamini kwa wakati ule tatizo kwa Mwalimu Nyerere ilikuwa kwa baadhi ya aliowapa dhamana ya kumsaidia katika utekelezaji. Je, Mwalimu aliwahi kulizungumza jambo hili nawe ukamsikia?
”Huo ndio ukweli. Mimi nimekuwa katika chama (TANU) tangu mwaka 1956. Kadi yangu ya uanachama wa TANU niliikatia Mbeya. Ni Nyerere mwenyewe, kwa mkono wake, pale Mbeya, mwaka 1956 alinijazia kadi yangu ya TANU. Alianza na Kanali Ayoub Simba ikaja ya kwangu.
”Hata leo, ukiangalia namba za kadi ya TANU ya Kanali Ayoub Simba na ya kwangu zinafuatana. Tulikuwa bado vijana sana, na Mwalimu alifanya mwenyewe kazi ya kuhamasisha vijana kuingia TANU. Mwenzangu Ayoub yeye akaja akaingia jeshini , akafikia mpaka cheo cha ukanali, akawa mbunge pia, kule Mafia. Yule ni kada wa siku nyingi.
”Sasa nimepata kumsikia Mwalimu akiongea kuhusu hili la uongozi? Kwa kweli si mara moja. Nimemsikia Mwalimu akitamka, kuwa njia iliyo nzuri sana ya kumsaidia katika uongozi wake ni kwa tulio karibu na watu kumwambia moja kwa moja juu ya mazuri na mabaya wanayofanya wateule wake.
”Kwamba ni hatari wananchi wakianza ama kuchoka kulalamika au kuwaogopa viongozi wao. Unajua Mwalimu hakuishia tu kutumia watu wa Usalama wa Taifa, aliwatumia pia watu wa kawaida kupata taarifa sahihi.”  Mzee, turudi kwenye kilichotokea kule Isimani, inasemekana kulikuwa na mtikisiko mkubwa hapa Iringa baada ya Dk.Kleruu kupigwa risasi na Mwamwindi. Je, hali ilikuwaje hasa?
” Ni sahihi, hali ilikuwa ngumu. Wengi tuliathirika na mkasa ule, kwa namna moja au nyingine. Unajua ilifika mahali wakati ule mtu ukigongewa mlango usiku, basi, unavaa kabisa, shati, suruali na viatu, maana huenda ukifungua mlango usirudi tena kitandani kwako!”
Hivi Iringa ya wakati ule ilionekaje, unakumbuka?
Anajibu Mzee Nzowa: ” Mji huu wa Iringa ulikuwa mdogo sana, wengi tulikuwa tunajuana. Hebu ngoja nipekue kwenye kabati langu kuona kama nina picha za zamani”. Mzee Nzowa anainuka kitini. Anakwenda kupekua picha za zamani. Nasubiri kwa shauku.
Wakati tukimsubiri  Mzee Nzowa , Jumatatu moja usiku napokea simu kutoka Uingereza;

” E bwana Maggid, niko Uingereza, nafuatilia kisa hiki cha Mwamwindi na Dk. Kleruu. Mimi nilikuwa kijijini Nyang’olo wakati wa tukio lile. Ni kijiji cha jirani na alikoishi Said Mwamwindi. Nilikuwa na miaka kumi. Nakumbuka mambo mengi sana , hata Dk. Kleruu nilimwona, alipenda sana kuja Nyang’olo. Sasa unasikia....” ( Simulizi hii itaendelea)

Add new comment

Kwanini Mkulima Mwamwindi alimpiga risasi RC Dk. Kleruu? IV

HII ni sehemu ya tatu ya simulizi kuhusu kwa nini mkulima Mwamwindi alimpiga risasi Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa wakati huo, Dk. Kleruu. Endelea...
Hivi Iringa ya wakati ule ilionekanaje, unakumbuka? Namwuliza Mzee Nzowa.” Mji huu wa Iringa ulikuwa mdogo sana, wengi tulikuwa tunajuana. Hebu ngoja nipekue kwenye kabati langu kuona kama nina picha za zamani”. Mzee Nzowa anainuka kitini. Anakwenda kupekua picha za zamani. Nasubiri kwa shauku.
Wakati tukimsubiri Mzee Nzowa, Jumatatu moja usiku napokea simu kutoka Uingereza; “Ebwana Maggid, niko Uingereza, nafuatilia kisa hiki cha Mwamwindi na Dk. Kleruu. Mimi nilikuwa kijijini Nyang’olo wakati wa tukio lile. Ni kijiji cha jirani na alikoishi marehemu Said Mwamwindi. Nilikuwa na miaka 10. Nakumbuka mambo mengi sana, hata Dk. Kleruu nilimwona, alipenda sana kuja Nyang’olo. Sasa unasikia....”
“Dk. Kleruu alikuwa akija na gari lake. Nyang’olo ni mji wa barabarani. Unajua ndio ilikuwa njia kuu ya kwenda Dodoma mpaka Arusha. Kulikuwa na biashara sana. Kulikuwa na wasomali hata waarabu. Nakumbuka Dk. Kleruu alikuwa akishika kifimbo chake na kuwafokea wazee juu ya mambo ya maendeleo. Kwa kweli wazee wa Nyang’olo hawakumpenda Kleruu,” anasema msomaji huyu ambaye sasa ana miaka 50 na anaishi nchini Uingereza.
Na wakati tukiendelea na simulizi hii ya Mwamwindi zimenifikia habari mbaya. Ni taarifa ya msiba wa Mzee Augustino Hongole Mzee Hongole ambaye, hadi kifo chake alikuwa mwenyekiti wa Bodi ya Uhariri wa gazeti la Kwanza Jamii, Njombe  amefariki majuma mawili  yaliyopita. Amezikwa kijijini kwao Lupembe., Njombe.
Kwangu mimi, Mzee Hongole ni  mmoja wa wazee waliochangia sana katika kuifanya simulizi hii iwe na maana kubwa. Maana, katika utafiti wangu juu ya kisa hiki cha Mwamwindi na Mkuu wa Mkoa Dk. Kleruu, nimepata bahati ya kufanya mazungumzo marefu ya ana kwa  ana na hata kwa njia ya simu na marehemu Mzee Hongole.
Na kweli mwandishi wa habari mwandamizi wa magazeti ya HabariLeo na Daily News, Beda Msimbe ndiye aliyenisisitiza sana umuhimu wa kumhoji Mzee Hongole huku kaka yangu Msimbe akisema; “Usichelewe sana, maana wazee hao ndio wanaondoka taratibu”.
Na hakika nimefanya jitihada za ziada za kupokea simulizi za Mzee Hongole juu ya anachokikumbuka katika wakati ule wa tukio.
Na katika hili la simulizi ya Mwamwindi mchango wa marehemu  Mzee Hongole ni mkubwa sana. Mzee Hongole amechangia kutoa elimu kubwa ya kimapokeo. Hakika, nina maelezo mengi ya Mzee Hongole ambayo nimeyahifadhi  kwa simulizi za baadae. 
Huko nyuma  nimewahi kusimulia yafuatayo niliyoyapokea kutoka kwa Mzee Hongole juu ya tukio la mkulima Mwamwindi kumpiga risasi Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Kleruu.
Mzee Hongole aliyepata kuwa mwandishi wa habari kijana sana wakati wa tukio la Mwamwindi kumuua Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Kleruu lililopotokea anasema; "Ndio kwanza nilikuwa nimepangiwa kufanya kazi kama mwandishi wa habari kwenye gazeti la Kanisa pale Iringa.
“Lilikuwa tukio kubwa sana. Kama mwandishi nilitamani kuandika kilichotokea na kupata maoni ya watu wa Iringa na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwa ujumla. Kwa wakati ule mfumo haukuruhusu kitu kama hicho. Mwamwindi story was an embargoed one (Stori ya Mwamwindi ilikuwa haiandikiki). Lakini nataka kukwambia: "Watu wengi wa Iringa hawakumpenda Dk. Kleruu kutokana na unyanyasaji wake".
Mzee Hongole anazidi kusema; “Unajua wakati huo kulikuwa na hofu kubwa juu ya dola. Waliokuwa tayari kumtetea Mwamwindi hadharani walihofia kukamatwa na makachero. Na mimi kalamu yangu ikawa nzito kwa kuogopa jela.
Lakini, kikubwa ni kuwa watu wa kanda hii walikuwa wamoja katika kumuunga mkono Mwamwindi.  Shida kubwa ilikuwa kwenye uUtekelezaji wa Azimio la Arusha. Utekelezaji ule kwa mtazamo wangu  ulifanywa kimakosa katika maeneo mengi ya nchi ikiwamo kanda yetu hii. Wananchi hawakuulizwa wanataka nini. Walilazimishwa tu na viongozi.
Nakumbuka kule Ilembula kuna wanafunzi waliolazimishwa baada ya masomo waende wakapande miche ya kahawa kwenye shamba la kijiji. Wazazi hawakupenda kilimo cha kahawa, lakini, Serikali ilitaka walime kahawa. Basi, ikatokea, kwa wazazi kuwaambia watoto wao, kuwa wakifika shambani waigeuze miche ya kahawa. Wapande juu chini. Hivyo hawakupanda, walipandua,” anasema Mzee Hongole.
Mzee Hongole anaendelea kusema; “Unajua ni mazingira kama hayo ndio yaliyochangia uzalishaji upungue. Wananchi walijisikia kushurutishwa. Hawakufanya kazi kwa moyo. Na vyombo vya habari navyo havikuwa huru kuweza kuelezea hali halisi za wananchi. Hapa utaona jinsi tulivyokuwa, kama taifa,  tukitoka kwenye reli. Maggid, nawaonea wivu sana katika wakati wenu huu kama wanahabari.
“Sisi tulisomea taaluma hii. Tena mimi nilipelekwa na Kanisa mpaka Sweden. Lakini, taaluma zetu zikaishia kufanya kazi ya kusifia Serikali tu, hata kwa mambo ya kipuuzi yaliyofanywa na baadhi ya viongozi. Wakati huo wa tukio la Mwamwindi watu wengi walikuwa na hamu ya kutaka kuujua ukweli. Lakini, sisi wanahabari tuliogopa hata kufika kijijini kwa Mwamwindi kuwahoji waliokuwepo siku ya tukio”
Mzee Hongole anasisitiza kwa kusema kuwa wakati umefika kwa Watanzania kuipitia upya historia yao. Hii itasaidia kuwafanya vijana wa kizazi hiki kujitambua. Watajenga mioyo ya uzalendo na kuwa tayari kuipigania nchi yao.
“Mimi nina shaka kuwa vijana wa siku hizi wamekosa kujiamini kwa vile hawajitambui. Hawaijui historia yao. Wana kiu ya kutaka kuifahamu historia yao. Ni kazi yenu nyinyi waandishi vijana kufanya tafiti juu ya historia yetu na kuisimulia,” anasema Mzee Augustino Hongole. . Mungu Amlaze Mahali Pema Peponi, Amen.

Mwandishi wa BBC John Ngahyoma afariki

Mwandishi wa BBC John Ngahyoma afariki

 30 Disemba, 2011 - Saa 17:10 GMT
Marehemu John Ngahyoma
Mwandishi wa BBC John Ngahyoma alifariki Ijumaa mjini Daresalaam
Mwandishi wa BBC John Ngahyoma amefariki dunia Ijumaa asubuhi nyumbani kwake mjini Dar Es Salaam.
Bwana Ngahyoma ameugua maradhi ya moyo kwa kipindi kirefu, na mwaka huu unaomalizika wa 2011 alifanyiwa upasuaji nchini India.
Amemwacha mke na watoto watatu.
Kaka mkubwa wa marehemu John, Ngalinecha Ngahyoma ameambia BBC kwamba mazishi yatafanyika jumapili, katika makaburi ya Kinondoni.
Ngahyoma ametumika katika BBC kwa kipindi kisichopungua miaka kumi.
Marehemu John Ngahyoma alizaliwa mwezi November mwaka 1960. Baada ya elimu ya Msingi alisoma katika sekondari ya Azania mijini Dar es Salaam na baadaye kuchukua Diploma katika chuo kikuuu cha St Augustine jijini Mwanza wakati huo kikijulikana kama Nyegezi Social.
Baadaye aliajiriwa katika magazeti ya Mwafrika na Daily News na baadaye Radio One na Itv Kabla yaa Kujiunga na Idhaa ya Kiswahili ya BBC.
Alikuwa mkuu mkuu wa Ofisi ya BBC Tanzania hadi mauti yalipomkuta Ijumaa asubuhi.
Waandishi mbali mbali wamekuwa wakituma risala za rambi rambi kufuatia kufariki kwa Bwana Ngahyoma.
Mwandishi wa BBC visiwani Zanzibar Ally Saleh Alberto ameandika haya kuhusu alivyomfahamu marehemu Ngahyoma.
Kwa karibu ya mwaka mmoja na nusu hivi sauti ya John Ngahyoma imekuwa haisikiki kukata mawimbi ya idhaa maarufu kuliko zote duniani BBC. Ni sauti
iliyokuwa imezoeleka. Kumbe mwenzetu alikuwa akipata majaribu ya Muumbaji ambaye aliamua kumpamaradhi ambayo ni yeye peke yake ambaye ndio angeweza kuyatoa hata waganga
na waganguzi wa dunia nzima wangekusanyika.


Muumbaji akaamua pia hatimae achukue roho ya kiumbe chake, ambacho hukiomba kwa kufumba na kufumbua na pamoja na maringo yetu yote binaadamu lakini
nguvu hii ya Muumba hutuamulia juu ya kilele cha mafanikio yetu, kama ambayo Ngahyoma alikuwa amefanikiwa kuyafika.


Nilianza kumjua Ngahyoma kama mwandishi wa Independent Television ITV na hasa nikimuona akitangaza habari za michezo. Alikuwa na fasaha nzuri ya
Kiswahili kama vile anatoka Pwani na mara nyingi nikawa nasema huyu atafika mbali.


Mara nikawa namuona akisoma taarifa ya habari. Huyu pamoja na kutoka mabara lakini alikuwa anamudu matamshi yote ya Kiswahili vilivyo na alikuwa mwingi
wa nahau na ndio maana mara akaajiriwa na BBC kwa maana BBC ilikiona kipaji chake.


Ni sifa ya BBC kwamba muajiriwa hutakiwa kufanya vitu vingi au niseme kila kitu. Mbali ya kuongoza vipindi, lakini muajiriwa pia huwa muandishi na
huko kwenye uandishi basi huwa ni fani zote.


Na kwa wengi huo huwa mtihani na ndio maana kuna wachache wetu ambao wamejikita katika fani chache, lakini wengi wetu ukitutupa kwenye uchumi
utafikiri wachumi, kwenye siasa utafikiri wahadhiri wa siasa na kwenye michezo ohooo huko ndio usiseme.


Hiyo pia ilikuwa ni sifa ya Ngahyoma. Aliweza kujijengea heshima katika kada ya uandishi alipojiunga na BBC kwa sababu talenta yake, chembilecho
wanavyosema Wakenya ndipo ilipokuja sio tu kujulikana kwa ufasaha lakini pia kun'gara kama mwezi.


Jina Ngahyoma likaanza kujulikana Tanzania na ikawa ni moja ya alama za BBC nchini Tanzania na watu wengi wakataka kujitambulisha nae na kwa hivyo
milango ya kupata habari ikawa wazi zaidi kwa BBC kote Tanzania.


Alijichanganya kirahisi. Kwenye michezo alijenga vyanzo vya habari lakini zaidi marafiki; kwenye biashara alipenya lakini akaweza kupenyezewa taarifa
nyingi zilizoipa sifa BBC na kwenye siasa alikuwa mwepesi wa kujua mstari wake unaishia wapi na kwa hivyo akaheshimika na kila kiongozi na chama cha
siasa.


Hakuna wakati mgumu alioupata Ngahyoma kama alivyohamishwa na mkubwa wetu wakati huo Tido Mhando kwenda Zanzibar, wakati wa kipindi cha Uchaguzi Mkuu
wa 2005 ambako alipiga kambi huko kwa miezi 6 kuiwakilisha BBC.


Ngahyoma alijikuta katika ushindani mkali wa kisiasa huko Visiwani ambako siasa zilikuwa ni ngumu na ushindani baina ya CUF na CCM ukiwa mkali na
kutishia hata uhuru na usalama wa waandishi wa habari.Ninalomsifu Ngahyoma kulimudu ni kufanya kazi yake kisawa sawa kabisa na kila upande ukaridhika kuwa ameripoti kipindi cha Uchaguzi bila ya kulalia
upande wowote ule.


Na hapo ndipo Ngahyoma alipokuwa amewiva na sikuona ajabu basi baada ya kuondoka Vicky Ntetema kama Mkuu wa Kituo cha Dar es salaam alikuwa ni
Ngahyoma aliyechukua nafasi hiyo.Kama Bosi wangu ilikuwa rahisi kufanya kazi na Ngahyoma. "Ehe Brother Ally," kama alivyozoea kuniita, maana mimi ni mkubwa kiumri kwake, " Kuna
nini leo Zanzibar."


Alikuwa rahisi kufanya kazi na watu na alimpa kila mtu uhuru wake lakini hakuwa akiogopa kumkosoa mtu au kutoa muongozo kwa analolihisi linafaa
kufanywa kwa faida ya BBC.Mbele ya Mungu ni dhambi kusema hakuna pengo la binaadamu ambalo haliwezi kujazwa, lakini kwa binaadamu ni dhaifu tunasema kuwa pengo la Ngahyoma
linataka mtu wa mbegu maalum kulijaza.


Si rahisi kumpata mtu rahimu, karimu, mchangamfu, mchapa kazi, mtu wa watu,msaidizi, muongozaji, mcheshi, mchekeshaji ndani ya binaadamu mmoja na
hivyo ndivyo alivyokuwa Ngahyoma.Ni sisi tuliokuwa nae karibu ndio tunaojua ni jinsi gani tumempoteza mtu miongoni mwetu na inshallah Mwenyenzi Mungu atupe subira, lakini asitume
sahau ya kumsahau Ngahyoma, maana kutokana na kuendelea kumkumbuka ndipo ambapo tutamuenzi