Haki miliki ya pichaRoma MkatolikiImage caption
Msanii Roma mkatoliki adaiwa kupatikana katika kituo kimoja cha polisi Jijini Dar Es Salaam
Msanii Roma
Mkatoliki aliyedaiwa kutoweka na watu wasiojulikana nchini Tanzania sasa
amepatikana katika kituo cha polisi cha Oysterbay jijini Dar.
Habari
hizo zimethibtishwa na mmiliki wa studio za Tongwe ambapo msanii huyo
na wenzake wawili wanadaiwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana siku ya
Jumatano jioni.
Hata
hivyo mmiliki huyo J Mada anasema kuwa hakuna maelezo ya kutosha
kuhusiana na wapi walipokuwa na ni akina nani aliokuwa wanawazuia.
Haki miliki ya pichaJamii ForumsImage caption
Mtandao wa jamii forums
Mtandao wa Jamii Forums unasema kuwa kupatikana kwao
kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na
mashabiki kuhusu kuachiliwa huru, ndani na nje ya mitandao ya kijamii. Serikali yaomba usaidizi kumtafuta Roma Mkatoliki
Awali,
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro
alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea
(kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.
Image caption
Price alipigwa risasi na mwanawe akiendesha gari
Mvulana wa umri wa miaka miwili amempiga risasi na kumuua mamake kimakosa katika mji wa Milwaukee, Marekani.
Mtoto huyo alipata bunduki hiyo sehemu ya nyuma ya gari.
Mwanamke
huyo, Patrice Price, 26, alikuwa akiendesha gari la mpenzi wake ambaye
ni mlinzi na ambaye alikuwa ameacha bunduki yake kwenye gari, babake
Andre Price amesema.
Polisi wa Milwaukee wanasema mwanamke huyo alipigwa risasi moja kutoka nyuma akiendesha gari mapema Jumanne asubuhi.
Mamake Price na mwanawe mwingine wa kiume mwenye umri wa mwaka mmoja walikuwa kwenye gari hilo wakati wa kutokea kwa kisa hicho.
Bw Price alisema ana binti mwingine mkubwa, lakini akasema Patrice alikuwa na bidii sana.
“Sasa hayupo nasi tena. Inaniuma sana,” Bw Price aliambia kituo cha habari cha WISN, Milwaukee.
Mwezi uliopita, mvulana wa umri wa miaka minne alimpiga risasi mamake Jamie Gilt katika jimbo la Florida katika hali sawa.
Bi Gilt alinusurika na majeraha.
Mtoto wa umri wa mwaka mmoja unusu amepatikana akiwa hai kwenye vifusi vya jengo lililoporomoka Ijumaa jijini Nairobi.
Jengo hilo la ghorofa sita liliporomoka katika mtaa wa Huruma baada ya mvua kubwa kunyesha.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation, msichana huyo alitolewa kwenye vifusi mwendo wa saa kumi usiku na kukimbizwa hospitalini.
Kamanda wa kitengo cha taifa cha kudhibiti majanga Pius Maasai anasema hali ya mtoto huyo ni thabiti, kwa mujibu wa gazeti hilo.
Watu 22 wamethibitishwa kufariki na wengine karibu 90 hawajulikani walipo.
Juhudi za uokoaji bado zinaendelea siku ya nne baada ya mkasa huo kutokea.
Kufikia sasa, watu 136 wameokolewa.
Polisi
wanasema wamiliki wa jumba hilo, ambalo maafisa wa baraza la jiji
wanasema halikufaa kuishi watu, wamekamatwa na wanazuiliwa na polisi.
Taarifa zinasema watafikishwa mahakamani baadaye Jumanne.
Wanafunzi
katika shule moja nchini Uingereza wameunda mipira ya kondomu
inayowaonya watumiaji wanapojamiana na mtu aliyeambukizwa maradhi ya
zinaa.
Kondomu hiyo inabadili rangi pindi inapokutana na majimaji ya mtu anayeugua maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
Kulingana na wanafunzi hao kondomu hiyo inabadili rangi tofauti kulingana na bakteria iliyopo.
Uvumbuzi
huu ni wa Daanyaal Ali, 14, Muaz Nawaz, 13 na Chirag Shah, 14, ambao
ni wanafunzi katika shule ya Isaac Newton Academy iliyoko Ilford,
Essex, nchini Uingereza.
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
''tuliazimia kumpa onyo
mtumiaji wa mipira hii kuwa mpenzi wake yuko salama ama ni mgonjwa bila
ya wasiwasi wa kupimwa hospitalini''.
Wanafunzi hao tayari wametunukiwa, tuzo la ubunifu la ''the TeenTech'' .
Daanyall alisema kuwa "Walizindua kondomu hiyo ilikuifaidi kizazi kijacho''
''Kwa
hakika swala la usalama wa mpenzi wako ni swala la kibinafsi kwa hivyo
ni swala linalopaswa kupewa kipaombele haswa ikifahamika kuwa tunawajibu
wa kuchochea ngono salama bila ya kuwashurutisha wapenzi wetu kufika
hospitalini bila wao wenyewe kukusudia''
Wavumbuzi hao wanasema kuwa hiyo ni mojawepo ya njia salama ya kubaini usalama penzi lenyu
Wanafunzi hao waliwalitunukiwa pauni elfu moja pamoja na fursa ya kuzuru Kasri la Malkia wa Uingereza Buckingham Palace.
Muasisi wa kampuni ya ubunifu wa kiteknolojia, TeenTech, Bwana Maggie Philbin, alisema kuwa
"Ni
wajibu wetu kama jamii kuchochea ubunifu unaopatikana madarasani
kuchochewa na kupigwa msasa kwa minajili ya kuboresha maisha ya
mwanadamu''
Tayari
mtandao huo wa kijamii wa Facebook unakusanya taarifa kutoka katika
picha zako ili kubaini migao ya maoni kutoka kwa marafiki wako pale
wanapoweka mtandaoni picha.
Sasa inaonekana mitandao ya kijamii inachukua mkondo mwingine wa kuboreshwa zaidi.
Watafiti
kutoka katika idara ya upelelezi ya Facebook wamekuwa wakiifanyia kazi
teknolojia hiyo mpya ambayo nia kuu ni kumtambua mtu hata kama uso wake
hauonekani bayana kwenye picha.
Teknolojia hiyo iitwayo 'algorithm', inaangazia zaidi ya viungo mia moja vya mwanadamu.
Inatumika kwa pamoja katika kutambua uso wa mtu na pia mwili mzima wa binadamu.
Watafiti hao walitumia njia hiyo kwa kuzifanyia majaribio picha elfu 37 za watu ambazo zilitolewa kutoka kwa 'Flickr Commons'.
Wanasema kuwa njia hiyo ilitoa matokeo asilimia 83 ya watu 581 tofauti.
Matokeo hayo yaliwasilishwa mapema mwezi huu wa Juni katika kongamano la wakfu wa Computer Vision.
Kitengo
cha ujasusi nchini Marekani NSA kiliwachunguza marais wa Ufaransa
akiwemo Jacques Chirac,Nicolas Sarkozy na Francois Hollande mwaka
2006-12,kulingana na mtandao wa wikileaks.
Mtandao huo ulipata habari hizo kutoka kwa ripoti za kiintelijensia na stakhabadhi nyengine za kiufundi za NSA.
Afisa mmoja wa Ufaransa amesema kuwa upelelezi wa washirika haufai.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande anatarajiwa kujadili swala hilo na maafisa wa usalama.
Marekani haijathibitisha ukweli wa stakhabadhi hizo
.
Wikileaks
Mwaka 2013 shirika la ujasusi la Marekani NSA lilishtumiwa kwa kumpeleleza kansela wa Ujerumani Angela Merkel.
Siku
ya jumanne,Wikileaks ilisema kuwa ilianza kuchapisha faili zilizo na
kichwa ''Espionage Elysee'' ikiwa ni kumbukumbu za ikulu ya rais wa
Ufaransa.
Imesema kuwa faili hizo za siri zilipatikana kupitia
upelelezi wa moja kwa moja wa mawasiliano uliofanywa na shirika hilo kwa
marais hao watatu wa Ufaransa pamoja na balozi wa Ufaransa nchini
Marekani.
Moja ya faili hizo ilioandikwa mwaka 2012,ni kuhusu rais
Hollande alivyokuwa akizungumza kuhusu kuondoka kwa Ugiriki katika
muungano wa Ulaya.
Nyengine ya mwaka 2011 inadai kuwa bwana
Sarkozy aliamua mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina bila
kuhusisha Marekani.
Mwanzilishi wa Wikileaks Julian Assange
Faili nyengine ilioandikwa
mwaka 2010 inadai kwamba maafisa wa Ufaransa walijua kwamba Marekani
ilikuwa ikiwapeleleza na kwamba walipanga kutoa malalamishi yao.
Kulingana
na habari za mawasiliano yaliodukuliwa,balozi wa Ufaransa nchini
Marekani na mshauri wa rais Sarkozy walijadiliana kuhusu mpango wa
Sarkozy kutoa ghadhabu zake kuhusu kukataa kwa Marekani kutia saini
makubaliano ya ushirikiano wa kijasusi,ikiwa lengo ni kwa Marekani
kuendelea kuipeleleza Ufaransa.
Bondia wa Marekani Floyd Mayweather ameshinda pigano lililosubiri kwa wingi katika miongo kadhaa.
Mayweather amshinda Pacquiao
Bondia huyo ambaye hajashindwa alimshinda mpinzani wake raia wa Ufilipino Manny Pacquiao kwa wingi wa pointi.
Pacquiao akimpiga makonde mayweather
Mashabiki wengi waliojaa katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena mjini Las Vegas walimzoma mara kwa mara Mayweather.
Mayweather ashinda kwa wingi wa pointi
Kote duniani wateja millioni 3
walilipa kuliona pigano hilo ambalo ndio pigano lililovutia kitita
kikubwa cha fedha katika historia ya ndondi.
Mayweather
Tiketi nyingi za pigano hilo ziliuzwa katika bei ya makumi ya maelfu ya dola.
Mkuu wa majeshi ya Burundi Meja Jenerali Prime Niyongabo
Mkuu
wa majeshi nchini Burundi Meja Jenerali Prime Niyongabo ametoa wito kwa
wanasiasa kutotumia jeshi la taifa kwa manufaa yao ya kisiasa.
Jenerali
Niyongabo amekariri tangazo lililotolewa na waziri wa ulinzi Jumamosi
kuwa jeshi la nchi hiyo litahakikisha kuwa mkataba wa Arusha
umetekelezwa kikamilifu na kuwa jeshi hilo halitumiwi na mtu au chama
chochote cha kisiasa.
Kuhusiana na maandamano yanayoendelea, mkuu
huyo wa jeshi amesema kuwa maandamano hayo sio halali na wanaichi
wanapaswa kutumia mbinu za sheria zilizopo kutatua mizozo yao.
Polisi wa kuzuia ghasia wakikabiliana na waandamanaji katika mitaa ya Bujumbura nchini Burundi
Wakati huo huo Meja Jenerali
Niyongabo amesema jeshi hilo litasalia kuwa lenye nidhamu ya hali ya juu
na tiifu kwa taifa la Burundi na wala sio kwa mwanasiasa yeyote.
Ameongeza
kusema kufikia sasa jeshi limefanya kazi nzuri kuhakikisha kuwepo kwa
usalama nchini Burundi na katika mataifa mengine wanakohudumu katika
vikosi vya Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika.
Mkuu huyo wa
majeshi amesema wanajeshi wataendelea kushirikiana na polisi kushika
doria ili kuhakikisha amani na utulivu vinakuwepo nchini Burundi.
Huku
hayo yakijitokeza muungano wa upinzani umesema kuwa maandamano
yataendelea siku ya Jumatatu baada ya mapunziko ya siku mbili.
Upinzani umepinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza ya kuwania muhula wa tatu kama rais.
Fumbo la siku zote kwamba wanawake
ni wanene kuliko wanaume limepata ufumbuzi...ni wanene kwa wanahitaji
mwili wenye umbo zuri na makalio makubwa ili kupata watoto waliojaaliwa
werevu.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa wanaakademia ambao wanasema
kuwa wanawake wenye makalio na mapaja makubwa na umbo zuri kutokana na
mafuta mfano kama
Kim Kardashian hupata watoto werevu.
Nini hasa kinawafanya
watoto wao kuwa werevu basi? Mafuta yanayopatikana katika sehemu za
mwili wa mwanamke huwa na manufaa makubwa sana kwa watoto hasa
wanapokuwa wananyonya, mafuta haya hupitia kwenye maziwa ya mama hadi
kwa mwili wa mtoto.
Profesa Will Lassek wa chuo kikuu cha
Pittsburgh University, Pennsylvania, aliyeongoza utafiti huo, anasema
mafuta yanayopatikana katika sehemu hizo za mwili, husaidia sana katika
kukuza ubongo wa matoto mchanga.
'Unahitaji mafuta mengi ya
mwilini ili kuwa na mfumo mzuri wa neva na mafuta katika sehemu hizi za
mwili yaani mapaja na makalio, huwa yina madini yajulikanayo kama DHA
(docosahexaenoic acid), ambayo ni muhimu sana katika kutengeza ubongo wa
binadamu.
Inaonekana kama wanawake wameweza kujua mbinu za kuhifadhi mafuta katika sehemu hizo za mwili hadi wanapopata mtoto.
Kwa
mda mrefu haijajulikana kwa nini wanawake wanakuwa wanene
sana.......mafuta ya mwili wao yakiwa ni asilimia 30 ya uzani wa mwili.
Professa
Lassek anasema kwamba mafuta hayo ni kiwango sawa na yale
yanayopatikana katika wanyama kama Dubu au Nyangumi wanapojiandaa kuzaa.
Wanasayansi
wanasema mafuta yanayopatikana katika mapaja na makalio ya wanawake
ndio yanayotumika kutengeza ubongo wa watoto wachanga.
Mafuta
mengi katika mwili wa mwanamke huisha mwilini pindi mama anapomnyonyesha
mtoto wake, kulingana na Profesa Lassek, aliyechapisha utafiti wake
katika kitabu chake kipya chenye kichwa ''Kwa nini wanawake wanahitaji
mafuta mwilini. ''
Wanawake wanaonyonyesha hupoteza kilo nusu ya mafuta mwilini kila mwezi.
Matokeo ya uchaguzi mkuu wa Zambia uliofanyika jana yatatangazwa kama ilivyopangwa awali.
Hata
hivyo kutangazwa kwa matokeo hayo kunakabiliwa na changamoto mbalimbali
kutokana na baadhi ya vituo vya kupigia kura kushindwa kupiga kura
jana, na hivyo kufanyika leo.
Vituo hamsini na moja vitapiga kura
hii leo na sababu kubwa ni mvua kubwa iliyo nyesha nchi yote ya Zambia
,hali mbaya ya hewa na kucheleweshwa kwa karatasi za kupigia kura ni
sababu zilizotajwa kusababisha wananchi wa Zambia kutopiga kura na leo
wapewe haki hiyo.
Hali mbaya ya hewa pia huenda ikasababisha hata
matokeo ya uchaguzi kutolewa kama ilivyosemwa awali,naye Rafael
Phiri,msemaji wa tume ya uchaguzi ya Zambia amethibitisha kuwa endapo
yatachelewa sana haitazidi tarehe ishirini na nne mwezi huu.
Rais
wa Marekani Barak Obama, amesema Marekani inafanya mabadiliko ya
kiuchumi na kijamii baada ya miaka mingi ya kujirudia kwa mdororo wa
uchumi na vita, huku uchumi ukiongeza ajira kwa kasi kubwa kuliko wakati
wowote tangu mwaka 1999.
Pia amesema Wamarekani wengi zaidi wana bima za afya kuliko wakati wowote kabla ya hapo.
Akihutubia
taifa kupitia baraza la Congress lenye wajumbe wengi kutoka chama cha
Republican, Rais Obama ametumia hotuba hiyo kutangaza mpango wa kujenga
uchumi wa kati kwa wananchi wote wa Marekani, ambapo wananchi wa kipato
cha chini watapata huduma za afya na elimu kwa gharama nafuu.
Rais
Obama ametangaza hatua za kusaidia familia za wafanyakazi kunufaika
kutokana na kukua kwa uchumi.Mkakati wa Bwana Obama anaouelezea kama
uchumi wa daraja la kati, unahusisha kupandisha kodi kwa matajiri.
Hotuba
ya Rais Obama ilibeba mapendekezo kuhusu kodi, vyuo vya jamii, huduma
za internet, usalama katika mtandao wa komputa na likizo ya ugonjwa.
Bwana Obama amesema hali ya kutoka katika mdororo wa uchumi imetoa fursa ya kuongezeka kwa kipato na fursa kwa kila mtu.
Amesema
uchumi wa daraja la kati ni wazo kwamba nchi hiyo inafanya vizuri
kabisa wakati kila mtu anapata haki katika mapato na kila mtu anatendewa
haki kama ilivyoanishwa katika sheria za nchi hiyo.
Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba akisaidiwa kutolewa katika vurugu
Katika
mazingira ya kutatanisha, siku ya Jumapili vurugu zimekatisha mdahalo
uliokuwa ukiendelea kujadili mchakato wa katiba mpya ya Tanzania huku
baadhi ya watu wakipigwa na kujeruhiwa.
Mdahalo huo uliokuwa
ukitangazwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni ulivurugika
kutokana na kundi la vijana wapatao 20 kuanza kumzomea aliyekuwa
mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba,
alipokuwa akiwasilisha mada yake.
Vijana hao ambao haijajulikana
walitokea wapi au walikuwa na ajenda gani waliinua mabango ya kupinga
msimamo wa waliokuwa wakiendesha mdahalo na kusema rasimu ya katiba
iliyopendekezwa inakidhi mahitaji yote na kusema hakuna haja ya mdahalo.
Jaji
Warioba ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania alifanikiwa kutoka
nje ya ukumbi ulipokuwa ukifanyika mdahalo huo mjini Dar Es Salaam,
lakini wapo watu waliojeruhiwa kutokana na kurushwa viti na vitu
vingine.
BBC iliwasiliana na Jaji Warioba apate kueleza
yaliyotokea na kama yuko salama baada ya vurugu hizo, lakini aliomba
radhi kwa kusema hayupo tayari kulizungumzia swala hilo.
Kiongozi
wa kitengo cha hamasa umoja wa vijana CCM (UVCCM), Paul Makonda,
aliyekuwepo ukumbini alidaiwa kuhusika na vurugu. Lakini alipoulizwa na
BBC kujibu tuhuma hizo Bw Makonda amekanusha kuhusika nazo huku akisema
kwamba alihudhuria mdahalo kwasababu ulikuwa wazi kwa kila mtu.
Wakati
wa vikao vya Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma, Makonda aliwahi kutoa
kauli za kumkebehi Jaji Warioba ambaye tume yake iliandaa rasimu ya
iliyokuwa ikijadiliwa na bunge hilo.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi
mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, aliieleza BBC kuwa hana maelezo ya
kutosha na kwamba atalizungumzia akipata taarifa rasmi ya kiofisi.
Tanzania
ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya. Rasimu iliyodaliwa na
kupitishwa na bunge lililosusiwa na vyama vya upinzani inatarajiwa
kupigiwa kura na wananchi mwezi Aprili, 2015.
Wachambuzi wa
maswala ya kisiasa wameeleza wasi wasi kuwa endapo hakutakuwa na
kuvumiliana hali ya kisiasa nchini humo inaweza kubadilika na kuleta
ghasia ambazo zinaweza kuepukika.
Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba akisaidiwa kutolewa katika vurugu
Katika
mazingira ya kutatanisha, siku ya Jumapili vurugu zimekatisha mdahalo
uliokuwa ukiendelea kujadili mchakato wa katiba mpya ya Tanzania huku
baadhi ya watu wakipigwa na kujeruhiwa.
Mdahalo huo uliokuwa
ukitangazwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni ulivurugika
kutokana na kundi la vijana wapatao 20 kuanza kumzomea aliyekuwa
mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba,
alipokuwa akiwasilisha mada yake.
Vijana hao ambao haijajulikana
walitokea wapi au walikuwa na ajenda gani waliinua mabango ya kupinga
msimamo wa waliokuwa wakiendesha mdahalo na kusema rasimu ya katiba
iliyopendekezwa inakidhi mahitaji yote na kusema hakuna haja ya mdahalo.
Jaji
Warioba ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania alifanikiwa kutoka
nje ya ukumbi ulipokuwa ukifanyika mdahalo huo mjini Dar Es Salaam,
lakini wapo watu waliojeruhiwa kutokana na kurushwa viti na vitu
vingine.
BBC iliwasiliana na Jaji Warioba apate kueleza
yaliyotokea na kama yuko salama baada ya vurugu hizo, lakini aliomba
radhi kwa kusema hayupo tayari kulizungumzia swala hilo.
Kiongozi
wa kitengo cha hamasa umoja wa vijana CCM (UVCCM), Paul Makonda,
aliyekuwepo ukumbini alidaiwa kuhusika na vurugu. Lakini alipoulizwa na
BBC kujibu tuhuma hizo Bw Makonda amekanusha kuhusika nazo huku akisema
kwamba alihudhuria mdahalo kwasababu ulikuwa wazi kwa kila mtu.
Wakati
wa vikao vya Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma, Makonda aliwahi kutoa
kauli za kumkebehi Jaji Warioba ambaye tume yake iliandaa rasimu ya
iliyokuwa ikijadiliwa na bunge hilo.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi
mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, aliieleza BBC kuwa hana maelezo ya
kutosha na kwamba atalizungumzia akipata taarifa rasmi ya kiofisi.
Tanzania
ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya. Rasimu iliyodaliwa na
kupitishwa na bunge lililosusiwa na vyama vya upinzani inatarajiwa
kupigiwa kura na wananchi mwezi Aprili, 2015.
Wachambuzi wa
maswala ya kisiasa wameeleza wasi wasi kuwa endapo hakutakuwa na
kuvumiliana hali ya kisiasa nchini humo inaweza kubadilika na kuleta
ghasia ambazo zinaweza kuepukika.
"Sitamwaacha binti yangu ateseke kama mimi ninavyoteseka nikiwa katika siku zangu. Familia yangu inafanya nijihisi najisi.
"Siruhusiwi kwenda jikoni, Siwezi kuingia hekaluni, Siwezi kukaa na wengine."
Kuna
hisia ya dhamira katika sauti ya Manju Baluni mwenye umri wa miaka 32.
Nilikutana naye katika kijiji cha Uttarakhand, jimbo lenye miinuko
kaskazini mwa India.
Nchini India,kuna ukimya kuhusu suala la afya
ya wanawake, hususan wawapo katika siku zao. Kuna mwiko uliojikita
katika jamii hizi kuhusu suala la mwanamke awapo katika hedhi: wanawake
si wasafi, wachafu, wagonjwa na wakati mwingine wamelaanika katika
kipindi hicho.
'Wasiwasi na Mashaka'
Watu wanaamini kuwa wanawake wanaokuwa katika hedhi hawatakiwi kuoga na wana upungufu wa damu.
Uchunguzi
wa hivi karibuni wa kampuni ya kutengeneza taulo maalum za kujisitiri
kina mama wanapokuwa katika hedhi umeonyesha kuwa asilimia 75% ya
wanawake wanaoishi mijini bado wananua taulo hizo zikiwa zimefungwa
katika mifuko au gazeti ili kutoonyesha kilichomo ndani kwa sababu ya
aibu inayohusishwa na hedhi.
Mwanamke akikunja taulo za kujihifadhi wakati wa siku zake nchini India
Na kamwe hawawaombi wanaume katika familia kuwanunulia taulo hizo maalum.
Nimekulia katika nyumba yenye wanawake wengi, lakini bado hatuwezi kujadili kwa uwazi suala hili ambalo ni la kawaida.
Wasichana
wanajifunza kuficha nguo zao wanazotumia wawapo kwenye hedhi kwa
wanaume baada ya kuzifua, anasema Rupa Jha. Mama yangu alitumia mashuka
makuu kuu na kuzificha katika sanduku, tayari kwa kutumiwa na mabinti
zake wanne.
Changamoto kubwa ni namna ya kukausha vipande hivyo
vya nguo. Nina kumbukumbu za kuhisi wasiwasi na mashaka juu ya mchakato
mzima.
Nilifundishwa mbinu nadada zangu wakubwa - namna ya kuficha
nguo zenye madoa ya damu chini ya nguo nyingine bila ya mwanaume yeyote
kugundua. Hatukuthubutu kuziacha peupe kwenye jua ili zikauke kabisa.
Nilihisi 'mchafu sana'
Matokeo ni kwamba kamwe hazikukauka vizuri, ziliacha harufu ya uvundo. Nguo hizo zisizo safi zilitumika tena na tena.
Wanawake wakisikiliza mwezeshaji kuhusu hali zao za usafi nchini India
Ukosefu wa maji ulifanya kazi
ya ufuaji kuwa ngumu na isiyo na usafi. Hali hiyo haijabadilika sana
tangu wakati huo kwa wanawake wengi wa Kihindi.
Uchunguzi mwingi
uliofanyika siku za karibuni umeonyesha kuwa mila hizi zimesababisha
madhara makubwa ya kiafya. Imeripotiwa kuwa mmoja kati ya wasichana
watano nchini India anaacha masomo kutokana na kadhia ya hedhi.
Baadhi
ya wasichana wanaacha kwenda shule wawapo katika kipindi cha hedhi.
Margdarshi mwenye umri wa miaka kumi na mitano anaishi katika kijiji cha
ndani cha Uttarakashi.
Anapenda kwenda shule japo inamaanisha
safari ngumu akipita katika eneo lenye vilima vikali. Kamwe hajawahi
kukosa masomo, isipokuwa kwa mwaka jana wakati ambapo nusura aache
masomo baada ya kupata siku zake kwa mara ya kwanza.
"Tatizo kubwa
kuliko yote ilikuwa namna ya kukabiliana na hali hiyo. Bado lipo.
Najisikia kufedheheshwa, hasira na mchafu sana. Mwanzoni niliacha kwenda
shule."
'Suala la kibinadamu'
Anataka kuwa daktari na
anashangaa kwa nini wavulana katika darasa lake wakati wa somo la elimu
ya viumbe(baolojia) wanacheka sana mwalimu anapoelezea njia ya hedhi.
"Nachukia.
Natamani tungekuwa huru zaidi na kujisikia huru tunapozungumzia suala
hili. Hali hii inatokea kwa kila mwanamke kwa hiyo kuna nini cha
kuchekesha hapo?"
Mama nchini India
Anshu Gupta, mwanzilishi wa
shirika lisilo la kiserikali, Goonj, anahisi kuwa tatizo hili limejikita
katika ukweli kwamba linahusishwa na wanawake.
Nchini India
wanawake wanatumia taulo za kujihifadhi wakati wawapo katika siku zao
kwa kutumia nguo kuu kuu. "Si suala la wanawake pekee. Ni suala la
kibinadamu lakini tumelibagua. Baadhi yetu tunataka kuondokana na
utamaduni huu wa kuona aibu na kunyamaza. Tunahitaji kuvunja utamaduni
huu."
Shirika hili linafanya kazi katika majimbo 21 kati ya 30.
Shirika
hili pia linatengeneza taulo rahisi kutokana na nguo zilizochakatwa
upya ili kuwasaidia asilimia 70% ya wanawake wa India ambao hawawezi
kupata taulo salama na safi.
Muhimu zaidi, wanaanza kuzungumzia suala hili. Bila kuhisi kufedheheka.
Makala
ya BBC ya BBC's 100 Women yamekuwa yakitangazwa katika mtandao, katika
televisheni na radio ya Idhaa ya Dunia tangu Oktoba 27-29. Changia maoni
yako katika mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter, ukitumia alama
#100Women.
Kituo
kimoja cha televisheni nchini Marekani kinachorusha kila siku kipindi
cha mhubiri Pat Robertson kiliomba radhi Jumatatu kwa madai yake potofu
kwamba wasafiri wanaokwenda Kenya wanaweza kupata maambukizi ya Ukimwi
kwa njia ya taulo.
"Dr Robertson alikosea kusema juu ya uwezekanao
wa kupata Ukimwi kwa njia ya mataulo," kimesema kituo cha Utangazaji
cha Kikristo, CBN, katika mtandao wa Facebook.
"CBN imegundua mara
moja kosa hili na kuondoa kauli hiyo kutoka kwa maktaba ya mtandao huo.
CBN inaomba radhi kwa mkanganyiko wowote."
Mhubiri huyo mwenye
umri wa miaka 84, mwinjilisti mkongwe ameonya katika kipindi chake cha
"700 Club" cha Oktoba 16 kwamba wasafiri watalazimika kuchukua tahadhari
ya hali ya juu ya kiafya wawapo nchini Kenya.
"Unaweza kupata
Ukimwi nchini Kenya," Bwana Robertson aliwaambia watazamaji wake
wanaokadiriwa kufikia milioni moja. "Watu wana ukimwi. Unatakiwa kuwa
makini. Nina maana kuwa, mataulo yanaweza kuwa na virusi vya Ukimwi."
Virusi vya HIV vinapatikana tu katika damu ya mwili na huenezwa tu kutoka kwa mwathiriwa
Madai ya Bwana Robertson haraka yalishambuliwa na makundi yanayojihusisha na masuala ya ugonjwa wa Ukimwi.
Wamesema
kuwa Ofisi ya serikali ya Marekani ya Masuala ya Afya ya kina Mama
inasema virusi vya Ukimwi haviwezi kuambukiza kwa njia ya "kushirikiana
vyombo vya chakula, mataulo na mashuka, simu au vyoo ."
'Hatari ya kutembelea Kenya'
Matamshi
ya Bwana Robertson yamekuja kutokana na swali alilotumiwa kwa njia ya
barua pepe na mtu asiyejulikana ambaye alielezea wasiwasi juu ya madhara
ya kutembelea Kenya wakati wa mlipuko wa Ebola barani Afrika.
Alimhakikishia
mtazamaji wa kipindi chake kuwa hakuna mgonjwa wa Ebola nchini Kenya
akisema Kenya iko mbali na kitovu cha mlipuko wa Ebola, Afrika
Magharibi.
Lakini Bwana Robertson alieleza hatari ya kuambukizwa magonjwa mengine nchini Kenya pamoja na Ukimwi.
Mbu
wanaweza kusababisha madhara makubwa ya ugonjwa, amesema, akiongezea
kwamba, "usafi akielezea kuwa tatizo lingine. Unakunywa maji,
hayajachujwa, unaweza kupata ugonjwa wa matumbo"
Jopo la Umoja wa Mataifa la wataalamu wa sayansi ya hali ya hewa,
limeonya leo kuwa mabadiliko makubwa yanatokea katika hali ya hewa
duniani na haitawezekana kurejesha hali ya zamani iwapo gesi
zinazozidisha joto duniani, hazitaondoshwa kabisa ufikapo mwisho wa
karne.
Ripoti iliyokubaliwa kwenye mkutano mjini Copenhagen, imechapishwa leo.
Dakta Peter Gleick ni mwana-sayansi wa mabadiliko ya hali ya hewa ambaye ameiona ripoti hiyo.
Aliiambia BBC, ushahidi wa kisayansi ni mzito sasa, kuwa binaadamu ndiye chanzo cha mabadiliko ya hali ya hewa:
"Bila ya shaka watu wasioamini kuwa wanaadamu ndio wanasababisha mabadiliko ya hali ya hewa, hawataki kusikiliza sayansi.
Kuna maswala magumu ya kisiasa yanahitaji kuamuliwa, lakini siyo ya kisayansi tena.
Ushahidi katika sayansi ni thabiti - kwamba hali ya hewa inabadilika; kwamba wanaadamu ndio wanayosababisha hayo.
Na kwamba ikiwa hatuchukui hatua sasa, basi totaona matokeo makubwa na hasara itakuwa kubwa kwa watu na dunia yenyewe."
Na
Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Marekani, John Kerry, alisema wale
wanaodharau sayansi kuhusu hali ya hewa iliomo kwenye ripoti hiyo,
wanahatarisha maisha yetu, watoto na wajukuu wetu.
Maofisa
wa serikali nchini Iraq wamesema wapiganaji wa Islamic State wameua
watu zaidi ya 300 wa madhehebu ya Sunni ambao wamekuwa wakipigana na
kundi hilo katika jimbo la Anbar.
Waziri wa Iraq wa masuala ya
haki za binadamu amesema kuwa miili zaidi 50 ikiwemo ya wanawake na
watoto ilikutwa ikielea katika visima.
Hata hivyo vyanzo kutoka
jamii ya Al-Bu Nimr vimeerifu kuwa kumekuwa na mauaji kwa awamu tatu
tangu alhamisi wiki iliyopita maeneo mbalimbali ya Iraq wakiwemo wale
wanajitoa mhanga katika mabomu.
Mashambulizi zaidi yanatarajiwa kwa waumini wa dini ya Shia katika sherehe za za Ashura.
A Microsoft account helps us personalize your Microsoft experiences and keeps your music, documents, app favorites, settings and more in sync with your Phone, PC or Xbox. Sign inNew here? Sign up