Sunday, April 9, 2017

Roma Mkatoliki na wenzake wapatikana Tanzania



Haki miliki ya picha Roma Mkatoliki
Image caption Msanii Roma mkatoliki adaiwa kupatikana katika kituo kimoja cha polisi Jijini Dar Es Salaam

Msanii Roma Mkatoliki aliyedaiwa kutoweka na watu wasiojulikana nchini Tanzania sasa amepatikana katika kituo cha polisi cha Oysterbay jijini Dar.
Habari hizo zimethibtishwa na mmiliki wa studio za Tongwe ambapo msanii huyo na wenzake wawili wanadaiwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana siku ya Jumatano jioni.
Hata hivyo mmiliki huyo J Mada anasema kuwa hakuna maelezo ya kutosha kuhusiana na wapi walipokuwa na ni akina nani aliokuwa wanawazuia.



Haki miliki ya picha Jamii Forums
Image caption Mtandao wa jamii forums
Mtandao wa Jamii Forums unasema kuwa kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru, ndani na nje ya mitandao ya kijamii.
Serikali yaomba usaidizi kumtafuta Roma Mkatoliki
Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.

Tuesday, May 3, 2016

Mtoto wa miaka 2 amuua mamake Marekani

Mtoto wa miaka 2 amuua mamake Marekani

  • 28 Aprili 2016
 
Image caption Price alipigwa risasi na mwanawe akiendesha gari
Mvulana wa umri wa miaka miwili amempiga risasi na kumuua mamake kimakosa katika mji wa Milwaukee, Marekani.
Mtoto huyo alipata bunduki hiyo sehemu ya nyuma ya gari.
Mwanamke huyo, Patrice Price, 26, alikuwa akiendesha gari la mpenzi wake ambaye ni mlinzi na ambaye alikuwa ameacha bunduki yake kwenye gari, babake Andre Price amesema.
Polisi wa Milwaukee wanasema mwanamke huyo alipigwa risasi moja kutoka nyuma akiendesha gari mapema Jumanne asubuhi.
Mamake Price na mwanawe mwingine wa kiume mwenye umri wa mwaka mmoja walikuwa kwenye gari hilo wakati wa kutokea kwa kisa hicho.
Bw Price alisema ana binti mwingine mkubwa, lakini akasema Patrice alikuwa na bidii sana.
“Sasa hayupo nasi tena. Inaniuma sana,” Bw Price aliambia kituo cha habari cha WISN, Milwaukee.
Mwezi uliopita, mvulana wa umri wa miaka minne alimpiga risasi mamake Jamie Gilt katika jimbo la Florida katika hali sawa.
Bi Gilt alinusurika na majeraha.

Mtoto mchanga atolewa kwenye vifusi Nairobi

Mtoto mchanga atolewa kwenye vifusi Nairobi

  • 3 Mei 2016. chanzo , bbcswahili
Jengo
Mtoto wa umri wa mwaka mmoja unusu amepatikana akiwa hai kwenye vifusi vya jengo lililoporomoka Ijumaa jijini Nairobi.
Jengo hilo la ghorofa sita liliporomoka katika mtaa wa Huruma baada ya mvua kubwa kunyesha.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation, msichana huyo alitolewa kwenye vifusi mwendo wa saa kumi usiku na kukimbizwa hospitalini.
Kamanda wa kitengo cha taifa cha kudhibiti majanga Pius Maasai anasema hali ya mtoto huyo ni thabiti, kwa mujibu wa gazeti hilo.
Watu 22 wamethibitishwa kufariki na wengine karibu 90 hawajulikani walipo.
Juhudi za uokoaji bado zinaendelea siku ya nne baada ya mkasa huo kutokea.
Kufikia sasa, watu 136 wameokolewa.
Polisi wanasema wamiliki wa jumba hilo, ambalo maafisa wa baraza la jiji wanasema halikufaa kuishi watu, wamekamatwa na wanazuiliwa na polisi.
Taarifa zinasema watafikishwa mahakamani baadaye Jumanne.

Wednesday, June 24, 2015

Kondomu inayotambua maambukizi ya Zinaa

Kondomu inayotambua maambukizi ya Zinaa

 
Kondomu inayotambua maambukizi ya zinaa
Wanafunzi katika shule moja nchini Uingereza wameunda mipira ya kondomu inayowaonya watumiaji wanapojamiana na mtu aliyeambukizwa maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo inabadili rangi pindi inapokutana na majimaji ya mtu anayeugua maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
Kulingana na wanafunzi hao kondomu hiyo inabadili rangi tofauti kulingana na bakteria iliyopo.
Uvumbuzi huu ni wa Daanyaal Ali, 14, Muaz Nawaz, 13 na Chirag Shah, 14, ambao ni wanafunzi katika shule ya Isaac Newton Academy iliyoko Ilford, Essex, nchini Uingereza.
 null
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
''tuliazimia kumpa onyo mtumiaji wa mipira hii kuwa mpenzi wake yuko salama ama ni mgonjwa bila ya wasiwasi wa kupimwa hospitalini''.
Wanafunzi hao tayari wametunukiwa, tuzo la ubunifu la ''the TeenTech'' .
Daanyall alisema kuwa "Walizindua kondomu hiyo ilikuifaidi kizazi kijacho''
''Kwa hakika swala la usalama wa mpenzi wako ni swala la kibinafsi kwa hivyo ni swala linalopaswa kupewa kipaombele haswa ikifahamika kuwa tunawajibu wa kuchochea ngono salama bila ya kuwashurutisha wapenzi wetu kufika hospitalini bila wao wenyewe kukusudia''
 null
Wavumbuzi hao wanasema kuwa hiyo ni mojawepo ya njia salama ya kubaini usalama penzi lenyu
Wanafunzi hao waliwalitunukiwa pauni elfu moja pamoja na fursa ya kuzuru Kasri la Malkia wa Uingereza Buckingham Palace.
Muasisi wa kampuni ya ubunifu wa kiteknolojia, TeenTech, Bwana Maggie Philbin, alisema kuwa
"Ni wajibu wetu kama jamii kuchochea ubunifu unaopatikana madarasani kuchochewa na kupigwa msasa kwa minajili ya kuboresha maisha ya mwanadamu''

Facebook kukutambua bila picha ya uso Dakika 49 zilizopita Mshirikishe mwenzako Facebook Tayari mtandao huo wa kijamii wa Facebook unakusanya taarifa kutoka katika picha zako ili kubaini migao ya maoni kutoka kwa marafiki wako pale wanapoweka mtandaoni picha. Sasa inaonekana mitandao ya kijamii inachukua mkondo mwingine wa kuboreshwa zaidi. Watafiti kutoka katika idara ya upelelezi ya Facebook wamekuwa wakiifanyia kazi teknolojia hiyo mpya ambayo nia kuu ni kumtambua mtu hata kama uso wake hauonekani bayana kwenye picha. Teknolojia hiyo iitwayo 'algorithm', inaangazia zaidi ya viungo mia moja vya mwanadamu. Inatumika kwa pamoja katika kutambua uso wa mtu na pia mwili mzima wa binadamu. Watafiti hao walitumia njia hiyo kwa kuzifanyia majaribio picha elfu 37 za watu ambazo zilitolewa kutoka kwa 'Flickr Commons'. Wanasema kuwa njia hiyo ilitoa matokeo asilimia 83 ya watu 581 tofauti. Matokeo hayo yaliwasilishwa mapema mwezi huu wa Juni katika kongamano la wakfu wa Computer Vision.

Facebook kukutambua bila picha ya uso


 
Facebook
Tayari mtandao huo wa kijamii wa Facebook unakusanya taarifa kutoka katika picha zako ili kubaini migao ya maoni kutoka kwa marafiki wako pale wanapoweka mtandaoni picha.
Sasa inaonekana mitandao ya kijamii inachukua mkondo mwingine wa kuboreshwa zaidi.
Watafiti kutoka katika idara ya upelelezi ya Facebook wamekuwa wakiifanyia kazi teknolojia hiyo mpya ambayo nia kuu ni kumtambua mtu hata kama uso wake hauonekani bayana kwenye picha.
Teknolojia hiyo iitwayo 'algorithm', inaangazia zaidi ya viungo mia moja vya mwanadamu.
Inatumika kwa pamoja katika kutambua uso wa mtu na pia mwili mzima wa binadamu.
Watafiti hao walitumia njia hiyo kwa kuzifanyia majaribio picha elfu 37 za watu ambazo zilitolewa kutoka kwa 'Flickr Commons'.
Wanasema kuwa njia hiyo ilitoa matokeo asilimia 83 ya watu 581 tofauti.
Matokeo hayo yaliwasilishwa mapema mwezi huu wa Juni katika kongamano la wakfu wa Computer Vision.

US iliwachunguza marais wa Ufaransa

US iliwachunguza marais wa Ufaransa


 
Marais wa Ufaransa
Kitengo cha ujasusi nchini Marekani NSA kiliwachunguza marais wa Ufaransa akiwemo Jacques Chirac,Nicolas Sarkozy na Francois Hollande mwaka 2006-12,kulingana na mtandao wa wikileaks.
Mtandao huo ulipata habari hizo kutoka kwa ripoti za kiintelijensia na stakhabadhi nyengine za kiufundi za NSA.
Afisa mmoja wa Ufaransa amesema kuwa upelelezi wa washirika haufai.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande anatarajiwa kujadili swala hilo na maafisa wa usalama.
Marekani haijathibitisha ukweli wa stakhabadhi hizo
.null
Wikileaks
Mwaka 2013 shirika la ujasusi la Marekani NSA lilishtumiwa kwa kumpeleleza kansela wa Ujerumani Angela Merkel.
Siku ya jumanne,Wikileaks ilisema kuwa ilianza kuchapisha faili zilizo na kichwa ''Espionage Elysee'' ikiwa ni kumbukumbu za ikulu ya rais wa Ufaransa.
Imesema kuwa faili hizo za siri zilipatikana kupitia upelelezi wa moja kwa moja wa mawasiliano uliofanywa na shirika hilo kwa marais hao watatu wa Ufaransa pamoja na balozi wa Ufaransa nchini Marekani.
Moja ya faili hizo ilioandikwa mwaka 2012,ni kuhusu rais Hollande alivyokuwa akizungumza kuhusu kuondoka kwa Ugiriki katika muungano wa Ulaya.
Nyengine ya mwaka 2011 inadai kuwa bwana Sarkozy aliamua mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina bila kuhusisha Marekani.
 null
Mwanzilishi wa Wikileaks Julian Assange
Faili nyengine ilioandikwa mwaka 2010 inadai kwamba maafisa wa Ufaransa walijua kwamba Marekani ilikuwa ikiwapeleleza na kwamba walipanga kutoa malalamishi yao.
Kulingana na habari za mawasiliano yaliodukuliwa,balozi wa Ufaransa nchini Marekani na mshauri wa rais Sarkozy walijadiliana kuhusu mpango wa Sarkozy kutoa ghadhabu zake kuhusu kukataa kwa Marekani kutia saini makubaliano ya ushirikiano wa kijasusi,ikiwa lengo ni kwa Marekani kuendelea kuipeleleza Ufaransa.

Monday, May 4, 2015

Floyd Mayweather amshinda Pacquiao

Floyd Mayweather amshinda Pacquiao

  • 3 Mei 2015
Pacquiao na Mayweather
Bondia wa Marekani Floyd Mayweather ameshinda pigano lililosubiri kwa wingi katika miongo kadhaa.
Mayweather amshinda Pacquiao
Bondia huyo ambaye hajashindwa alimshinda mpinzani wake raia wa Ufilipino Manny Pacquiao kwa wingi wa pointi.
Pacquiao akimpiga makonde mayweather
Mashabiki wengi waliojaa katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena mjini Las Vegas walimzoma mara kwa mara Mayweather.
Mayweather ashinda kwa wingi wa pointi
Kote duniani wateja millioni 3 walilipa kuliona pigano hilo ambalo ndio pigano lililovutia kitita kikubwa cha fedha katika historia ya ndondi.
Mayweather
Tiketi nyingi za pigano hilo ziliuzwa katika bei ya makumi ya maelfu ya dola.

Mkuu wa majeshi Burundi akemea wanasiasa

Mkuu wa majeshi Burundi akemea wanasiasa

  • 3 Mei 2015
Mkuu wa majeshi ya Burundi Meja Jenerali Prime Niyongabo
Mkuu wa majeshi nchini Burundi Meja Jenerali Prime Niyongabo ametoa wito kwa wanasiasa kutotumia jeshi la taifa kwa manufaa yao ya kisiasa.
Jenerali Niyongabo amekariri tangazo lililotolewa na waziri wa ulinzi Jumamosi kuwa jeshi la nchi hiyo litahakikisha kuwa mkataba wa Arusha umetekelezwa kikamilifu na kuwa jeshi hilo halitumiwi na mtu au chama chochote cha kisiasa.
Kuhusiana na maandamano yanayoendelea, mkuu huyo wa jeshi amesema kuwa maandamano hayo sio halali na wanaichi wanapaswa kutumia mbinu za sheria zilizopo kutatua mizozo yao.
Polisi wa kuzuia ghasia wakikabiliana na waandamanaji katika mitaa ya Bujumbura nchini Burundi
Wakati huo huo Meja Jenerali Niyongabo amesema jeshi hilo litasalia kuwa lenye nidhamu ya hali ya juu na tiifu kwa taifa la Burundi na wala sio kwa mwanasiasa yeyote.
Ameongeza kusema kufikia sasa jeshi limefanya kazi nzuri kuhakikisha kuwepo kwa usalama nchini Burundi na katika mataifa mengine wanakohudumu katika vikosi vya Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika.
Mkuu huyo wa majeshi amesema wanajeshi wataendelea kushirikiana na polisi kushika doria ili kuhakikisha amani na utulivu vinakuwepo nchini Burundi.
Huku hayo yakijitokeza muungano wa upinzani umesema kuwa maandamano yataendelea siku ya Jumatatu baada ya mapunziko ya siku mbili.
Upinzani umepinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza ya kuwania muhula wa tatu kama rais.

Tuesday, January 20, 2015

Eti mafuta ya mwilini hukuza ubongo?



Eti mafuta ya mwilini hukuza ubongo?





Fumbo la siku zote kwamba wanawake ni wanene kuliko wanaume limepata ufumbuzi...ni wanene kwa wanahitaji mwili wenye umbo zuri na makalio makubwa ili kupata watoto waliojaaliwa werevu.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa wanaakademia ambao wanasema kuwa wanawake wenye makalio na mapaja makubwa na umbo zuri kutokana na mafuta mfano kama Kim Kardashian hupata watoto werevu.
Nini hasa kinawafanya watoto wao kuwa werevu basi? Mafuta yanayopatikana katika sehemu za mwili wa mwanamke huwa na manufaa makubwa sana kwa watoto hasa wanapokuwa wananyonya, mafuta haya hupitia kwenye maziwa ya mama hadi kwa mwili wa mtoto.
Profesa Will Lassek wa chuo kikuu cha Pittsburgh University, Pennsylvania, aliyeongoza utafiti huo, anasema mafuta yanayopatikana katika sehemu hizo za mwili, husaidia sana katika kukuza ubongo wa matoto mchanga.



'Unahitaji mafuta mengi ya mwilini ili kuwa na mfumo mzuri wa neva na mafuta katika sehemu hizi za mwili yaani mapaja na makalio, huwa yina madini yajulikanayo kama DHA (docosahexaenoic acid), ambayo ni muhimu sana katika kutengeza ubongo wa binadamu.
Inaonekana kama wanawake wameweza kujua mbinu za kuhifadhi mafuta katika sehemu hizo za mwili hadi wanapopata mtoto.
Kwa mda mrefu haijajulikana kwa nini wanawake wanakuwa wanene sana.......mafuta ya mwili wao yakiwa ni asilimia 30 ya uzani wa mwili.
Professa Lassek anasema kwamba mafuta hayo ni kiwango sawa na yale yanayopatikana katika wanyama kama Dubu au Nyangumi wanapojiandaa kuzaa.
Wanasayansi wanasema mafuta yanayopatikana katika mapaja na makalio ya wanawake ndio yanayotumika kutengeza ubongo wa watoto wachanga.
Mafuta mengi katika mwili wa mwanamke huisha mwilini pindi mama anapomnyonyesha mtoto wake, kulingana na Profesa Lassek, aliyechapisha utafiti wake katika kitabu chake kipya chenye kichwa ''Kwa nini wanawake wanahitaji mafuta mwilini. ''
Wanawake wanaonyonyesha hupoteza kilo nusu ya mafuta mwilini kila mwezi.

Hali mbaya ya hewa yaikabili Zambia

Hali mbaya ya hewa yaikabili Zambia



Matokeo ya uchaguzi mkuu wa Zambia uliofanyika jana yatatangazwa kama ilivyopangwa awali.
Hata hivyo kutangazwa kwa matokeo hayo kunakabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na baadhi ya vituo vya kupigia kura kushindwa kupiga kura jana, na hivyo kufanyika leo.
Vituo hamsini na moja vitapiga kura hii leo na sababu kubwa ni mvua kubwa iliyo nyesha nchi yote ya Zambia ,hali mbaya ya hewa na kucheleweshwa kwa karatasi za kupigia kura ni sababu zilizotajwa kusababisha wananchi wa Zambia kutopiga kura na leo wapewe haki hiyo.
Hali mbaya ya hewa pia huenda ikasababisha hata matokeo ya uchaguzi kutolewa kama ilivyosemwa awali,naye Rafael Phiri,msemaji wa tume ya uchaguzi ya Zambia amethibitisha kuwa endapo yatachelewa sana haitazidi tarehe ishirini na nne mwezi huu.

Rais Obama ataka mgao sawa wa rasilimali

Rais Obama ataka mgao sawa wa rasilimali 

 
Rais Barack Obama wa Marekani
Rais wa Marekani Barak Obama, amesema Marekani inafanya mabadiliko ya kiuchumi na kijamii baada ya miaka mingi ya kujirudia kwa mdororo wa uchumi na vita, huku uchumi ukiongeza ajira kwa kasi kubwa kuliko wakati wowote tangu mwaka 1999.
Pia amesema Wamarekani wengi zaidi wana bima za afya kuliko wakati wowote kabla ya hapo.
Akihutubia taifa kupitia baraza la Congress lenye wajumbe wengi kutoka chama cha Republican, Rais Obama ametumia hotuba hiyo kutangaza mpango wa kujenga uchumi wa kati kwa wananchi wote wa Marekani, ambapo wananchi wa kipato cha chini watapata huduma za afya na elimu kwa gharama nafuu.
Rais Obama ametangaza hatua za kusaidia familia za wafanyakazi kunufaika kutokana na kukua kwa uchumi.Mkakati wa Bwana Obama anaouelezea kama uchumi wa daraja la kati, unahusisha kupandisha kodi kwa matajiri.
Hotuba ya Rais Obama ilibeba mapendekezo kuhusu kodi, vyuo vya jamii, huduma za internet, usalama katika mtandao wa komputa na likizo ya ugonjwa.
Bwana Obama amesema hali ya kutoka katika mdororo wa uchumi imetoa fursa ya kuongezeka kwa kipato na fursa kwa kila mtu.
Amesema uchumi wa daraja la kati ni wazo kwamba nchi hiyo inafanya vizuri kabisa wakati kila mtu anapata haki katika mapato na kila mtu anatendewa haki kama ilivyoanishwa katika sheria za nchi hiyo.

Monday, November 3, 2014

Warioba adhalilishwa mdahalo wa Katiba

Warioba adhalilishwa mdahalo wa Katiba

  • 2/11/2014
Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba akisaidiwa kutolewa katika vurugu
Katika mazingira ya kutatanisha, siku ya Jumapili vurugu zimekatisha mdahalo uliokuwa ukiendelea kujadili mchakato wa katiba mpya ya Tanzania huku baadhi ya watu wakipigwa na kujeruhiwa.
Mdahalo huo uliokuwa ukitangazwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni ulivurugika kutokana na kundi la vijana wapatao 20 kuanza kumzomea aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alipokuwa akiwasilisha mada yake.
Vijana hao ambao haijajulikana walitokea wapi au walikuwa na ajenda gani waliinua mabango ya kupinga msimamo wa waliokuwa wakiendesha mdahalo na kusema rasimu ya katiba iliyopendekezwa inakidhi mahitaji yote na kusema hakuna haja ya mdahalo.
Jaji Warioba ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania alifanikiwa kutoka nje ya ukumbi ulipokuwa ukifanyika mdahalo huo mjini Dar Es Salaam, lakini wapo watu waliojeruhiwa kutokana na kurushwa viti na vitu vingine.
BBC iliwasiliana na Jaji Warioba apate kueleza yaliyotokea na kama yuko salama baada ya vurugu hizo, lakini aliomba radhi kwa kusema hayupo tayari kulizungumzia swala hilo.
Kiongozi wa kitengo cha hamasa umoja wa vijana CCM (UVCCM), Paul Makonda, aliyekuwepo ukumbini alidaiwa kuhusika na vurugu. Lakini alipoulizwa na BBC kujibu tuhuma hizo Bw Makonda amekanusha kuhusika nazo huku akisema kwamba alihudhuria mdahalo kwasababu ulikuwa wazi kwa kila mtu.
Wakati wa vikao vya Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma, Makonda aliwahi kutoa kauli za kumkebehi Jaji Warioba ambaye tume yake iliandaa rasimu ya iliyokuwa ikijadiliwa na bunge hilo.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, aliieleza BBC kuwa hana maelezo ya kutosha na kwamba atalizungumzia akipata taarifa rasmi ya kiofisi.
Tanzania ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya. Rasimu iliyodaliwa na kupitishwa na bunge lililosusiwa na vyama vya upinzani inatarajiwa kupigiwa kura na wananchi mwezi Aprili, 2015.
Wachambuzi wa maswala ya kisiasa wameeleza wasi wasi kuwa endapo hakutakuwa na kuvumiliana hali ya kisiasa nchini humo inaweza kubadilika na kuleta ghasia ambazo zinaweza kuepukika.
  • Saa 9 zilizopita
Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba akisaidiwa kutolewa katika vurugu
Katika mazingira ya kutatanisha, siku ya Jumapili vurugu zimekatisha mdahalo uliokuwa ukiendelea kujadili mchakato wa katiba mpya ya Tanzania huku baadhi ya watu wakipigwa na kujeruhiwa.
Mdahalo huo uliokuwa ukitangazwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni ulivurugika kutokana na kundi la vijana wapatao 20 kuanza kumzomea aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alipokuwa akiwasilisha mada yake.
Vijana hao ambao haijajulikana walitokea wapi au walikuwa na ajenda gani waliinua mabango ya kupinga msimamo wa waliokuwa wakiendesha mdahalo na kusema rasimu ya katiba iliyopendekezwa inakidhi mahitaji yote na kusema hakuna haja ya mdahalo.
Jaji Warioba ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania alifanikiwa kutoka nje ya ukumbi ulipokuwa ukifanyika mdahalo huo mjini Dar Es Salaam, lakini wapo watu waliojeruhiwa kutokana na kurushwa viti na vitu vingine.
BBC iliwasiliana na Jaji Warioba apate kueleza yaliyotokea na kama yuko salama baada ya vurugu hizo, lakini aliomba radhi kwa kusema hayupo tayari kulizungumzia swala hilo.
Kiongozi wa kitengo cha hamasa umoja wa vijana CCM (UVCCM), Paul Makonda, aliyekuwepo ukumbini alidaiwa kuhusika na vurugu. Lakini alipoulizwa na BBC kujibu tuhuma hizo Bw Makonda amekanusha kuhusika nazo huku akisema kwamba alihudhuria mdahalo kwasababu ulikuwa wazi kwa kila mtu.
Wakati wa vikao vya Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma, Makonda aliwahi kutoa kauli za kumkebehi Jaji Warioba ambaye tume yake iliandaa rasimu ya iliyokuwa ikijadiliwa na bunge hilo.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, aliieleza BBC kuwa hana maelezo ya kutosha na kwamba atalizungumzia akipata taarifa rasmi ya kiofisi.
Tanzania ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya. Rasimu iliyodaliwa na kupitishwa na bunge lililosusiwa na vyama vya upinzani inatarajiwa kupigiwa kura na wananchi mwezi Aprili, 2015.
Wachambuzi wa maswala ya kisiasa wameeleza wasi wasi kuwa endapo hakutakuwa na kuvumiliana hali ya kisiasa nchini humo inaweza kubadilika na kuleta ghasia ambazo zinaweza kuepukika.

Hedhi yawa fedheha kwa wanawake India

Hedhi yawa fedheha kwa wanawake India

  • 31 Oktoba 2014

Wanawake wakifua na kuoga nchini India

"Sitamwaacha binti yangu ateseke kama mimi ninavyoteseka nikiwa katika siku zangu. Familia yangu inafanya nijihisi najisi.
"Siruhusiwi kwenda jikoni, Siwezi kuingia hekaluni, Siwezi kukaa na wengine."
Kuna hisia ya dhamira katika sauti ya Manju Baluni mwenye umri wa miaka 32. Nilikutana naye katika kijiji cha Uttarakhand, jimbo lenye miinuko kaskazini mwa India.
Nchini India,kuna ukimya kuhusu suala la afya ya wanawake, hususan wawapo katika siku zao. Kuna mwiko uliojikita katika jamii hizi kuhusu suala la mwanamke awapo katika hedhi: wanawake si wasafi, wachafu, wagonjwa na wakati mwingine wamelaanika katika kipindi hicho.
'Wasiwasi na Mashaka'
Watu wanaamini kuwa wanawake wanaokuwa katika hedhi hawatakiwi kuoga na wana upungufu wa damu.
Uchunguzi wa hivi karibuni wa kampuni ya kutengeneza taulo maalum za kujisitiri kina mama wanapokuwa katika hedhi umeonyesha kuwa asilimia 75% ya wanawake wanaoishi mijini bado wananua taulo hizo zikiwa zimefungwa katika mifuko au gazeti ili kutoonyesha kilichomo ndani kwa sababu ya aibu inayohusishwa na hedhi.
 

Mwanamke akikunja taulo za kujihifadhi wakati wa siku zake nchini India
Na kamwe hawawaombi wanaume katika familia kuwanunulia taulo hizo maalum.
Nimekulia katika nyumba yenye wanawake wengi, lakini bado hatuwezi kujadili kwa uwazi suala hili ambalo ni la kawaida.
Wasichana wanajifunza kuficha nguo zao wanazotumia wawapo kwenye hedhi kwa wanaume baada ya kuzifua, anasema Rupa Jha. Mama yangu alitumia mashuka makuu kuu na kuzificha katika sanduku, tayari kwa kutumiwa na mabinti zake wanne.
Changamoto kubwa ni namna ya kukausha vipande hivyo vya nguo. Nina kumbukumbu za kuhisi wasiwasi na mashaka juu ya mchakato mzima.
Nilifundishwa mbinu nadada zangu wakubwa - namna ya kuficha nguo zenye madoa ya damu chini ya nguo nyingine bila ya mwanaume yeyote kugundua. Hatukuthubutu kuziacha peupe kwenye jua ili zikauke kabisa.
Nilihisi 'mchafu sana'
Matokeo ni kwamba kamwe hazikukauka vizuri, ziliacha harufu ya uvundo. Nguo hizo zisizo safi zilitumika tena na tena.
 

Wanawake wakisikiliza mwezeshaji kuhusu hali zao za usafi nchini India
Ukosefu wa maji ulifanya kazi ya ufuaji kuwa ngumu na isiyo na usafi. Hali hiyo haijabadilika sana tangu wakati huo kwa wanawake wengi wa Kihindi.
Uchunguzi mwingi uliofanyika siku za karibuni umeonyesha kuwa mila hizi zimesababisha madhara makubwa ya kiafya. Imeripotiwa kuwa mmoja kati ya wasichana watano nchini India anaacha masomo kutokana na kadhia ya hedhi.
Baadhi ya wasichana wanaacha kwenda shule wawapo katika kipindi cha hedhi. Margdarshi mwenye umri wa miaka kumi na mitano anaishi katika kijiji cha ndani cha Uttarakashi.
Anapenda kwenda shule japo inamaanisha safari ngumu akipita katika eneo lenye vilima vikali. Kamwe hajawahi kukosa masomo, isipokuwa kwa mwaka jana wakati ambapo nusura aache masomo baada ya kupata siku zake kwa mara ya kwanza.
"Tatizo kubwa kuliko yote ilikuwa namna ya kukabiliana na hali hiyo. Bado lipo. Najisikia kufedheheshwa, hasira na mchafu sana. Mwanzoni niliacha kwenda shule."
'Suala la kibinadamu'
Anataka kuwa daktari na anashangaa kwa nini wavulana katika darasa lake wakati wa somo la elimu ya viumbe(baolojia) wanacheka sana mwalimu anapoelezea njia ya hedhi.
"Nachukia. Natamani tungekuwa huru zaidi na kujisikia huru tunapozungumzia suala hili. Hali hii inatokea kwa kila mwanamke kwa hiyo kuna nini cha kuchekesha hapo?"
 

Mama nchini India
Anshu Gupta, mwanzilishi wa shirika lisilo la kiserikali, Goonj, anahisi kuwa tatizo hili limejikita katika ukweli kwamba linahusishwa na wanawake.
Nchini India wanawake wanatumia taulo za kujihifadhi wakati wawapo katika siku zao kwa kutumia nguo kuu kuu. "Si suala la wanawake pekee. Ni suala la kibinadamu lakini tumelibagua. Baadhi yetu tunataka kuondokana na utamaduni huu wa kuona aibu na kunyamaza. Tunahitaji kuvunja utamaduni huu."
Shirika hili linafanya kazi katika majimbo 21 kati ya 30.
Shirika hili pia linatengeneza taulo rahisi kutokana na nguo zilizochakatwa upya ili kuwasaidia asilimia 70% ya wanawake wa India ambao hawawezi kupata taulo salama na safi.
Muhimu zaidi, wanaanza kuzungumzia suala hili. Bila kuhisi kufedheheka.
Makala ya BBC ya BBC's 100 Women yamekuwa yakitangazwa katika mtandao, katika televisheni na radio ya Idhaa ya Dunia tangu Oktoba 27-29. Changia maoni yako katika mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter, ukitumia alama #100Women.

Taulo Kenya zina ukimwi',asema mhubiri

Taulo Kenya zina ukimwi',asema mhubiri

  • 22 Oktoba 2014
Kituo kimoja cha televisheni nchini Marekani kinachorusha kila siku kipindi cha mhubiri Pat Robertson kiliomba radhi Jumatatu kwa madai yake potofu kwamba wasafiri wanaokwenda Kenya wanaweza kupata maambukizi ya Ukimwi kwa njia ya taulo.
"Dr Robertson alikosea kusema juu ya uwezekanao wa kupata Ukimwi kwa njia ya mataulo," kimesema kituo cha Utangazaji cha Kikristo, CBN, katika mtandao wa Facebook.
"CBN imegundua mara moja kosa hili na kuondoa kauli hiyo kutoka kwa maktaba ya mtandao huo. CBN inaomba radhi kwa mkanganyiko wowote."
Mhubiri huyo mwenye umri wa miaka 84, mwinjilisti mkongwe ameonya katika kipindi chake cha "700 Club" cha Oktoba 16 kwamba wasafiri watalazimika kuchukua tahadhari ya hali ya juu ya kiafya wawapo nchini Kenya.
"Unaweza kupata Ukimwi nchini Kenya," Bwana Robertson aliwaambia watazamaji wake wanaokadiriwa kufikia milioni moja. "Watu wana ukimwi. Unatakiwa kuwa makini. Nina maana kuwa, mataulo yanaweza kuwa na virusi vya Ukimwi."
Virusi vya HIV vinapatikana tu katika damu ya mwili na huenezwa tu kutoka kwa mwathiriwa
Madai ya Bwana Robertson haraka yalishambuliwa na makundi yanayojihusisha na masuala ya ugonjwa wa Ukimwi.
Wamesema kuwa Ofisi ya serikali ya Marekani ya Masuala ya Afya ya kina Mama inasema virusi vya Ukimwi haviwezi kuambukiza kwa njia ya "kushirikiana vyombo vya chakula, mataulo na mashuka, simu au vyoo ."
'Hatari ya kutembelea Kenya'
Matamshi ya Bwana Robertson yamekuja kutokana na swali alilotumiwa kwa njia ya barua pepe na mtu asiyejulikana ambaye alielezea wasiwasi juu ya madhara ya kutembelea Kenya wakati wa mlipuko wa Ebola barani Afrika.
Alimhakikishia mtazamaji wa kipindi chake kuwa hakuna mgonjwa wa Ebola nchini Kenya akisema Kenya iko mbali na kitovu cha mlipuko wa Ebola, Afrika Magharibi.
Lakini Bwana Robertson alieleza hatari ya kuambukizwa magonjwa mengine nchini Kenya pamoja na Ukimwi.
Mbu wanaweza kusababisha madhara makubwa ya ugonjwa, amesema, akiongezea kwamba, "usafi akielezea kuwa tatizo lingine. Unakunywa maji, hayajachujwa, unaweza kupata ugonjwa wa matumbo"

Mazingira yahitaji hatua haraka

Mazingira yahitaji hatua haraka

  • 2 Novemba 2014
Jopo la Umoja wa Mataifa la wataalamu wa sayansi ya hali ya hewa, limeonya leo kuwa mabadiliko makubwa yanatokea katika hali ya hewa duniani na haitawezekana kurejesha hali ya zamani iwapo gesi zinazozidisha joto duniani, hazitaondoshwa kabisa ufikapo mwisho wa karne.
Ripoti iliyokubaliwa kwenye mkutano mjini Copenhagen, imechapishwa leo.
Dakta Peter Gleick ni mwana-sayansi wa mabadiliko ya hali ya hewa ambaye ameiona ripoti hiyo.
Aliiambia BBC, ushahidi wa kisayansi ni mzito sasa, kuwa binaadamu ndiye chanzo cha mabadiliko ya hali ya hewa:
"Bila ya shaka watu wasioamini kuwa wanaadamu ndio wanasababisha mabadiliko ya hali ya hewa, hawataki kusikiliza sayansi.
Kuna maswala magumu ya kisiasa yanahitaji kuamuliwa, lakini siyo ya kisayansi tena.
Ushahidi katika sayansi ni thabiti - kwamba hali ya hewa inabadilika; kwamba wanaadamu ndio wanayosababisha hayo.
Na kwamba ikiwa hatuchukui hatua sasa, basi totaona matokeo makubwa na hasara itakuwa kubwa kwa watu na dunia yenyewe."
Na Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Marekani, John Kerry, alisema wale wanaodharau sayansi kuhusu hali ya hewa iliomo kwenye ripoti hiyo, wanahatarisha maisha yetu, watoto na wajukuu wetu.

IS waua zaidi ya watu 300 Iraq


IS waua zaidi ya watu 300 Iraq

wapiganaji wa Islamic State
Maofisa wa serikali nchini Iraq wamesema wapiganaji wa Islamic State wameua watu zaidi ya 300 wa madhehebu ya Sunni ambao wamekuwa wakipigana na kundi hilo katika jimbo la Anbar.
Waziri wa Iraq wa masuala ya haki za binadamu amesema kuwa miili zaidi 50 ikiwemo ya wanawake na watoto ilikutwa ikielea katika visima.
Hata hivyo vyanzo kutoka jamii ya Al-Bu Nimr vimeerifu kuwa kumekuwa na mauaji kwa awamu tatu tangu alhamisi wiki iliyopita maeneo mbalimbali ya Iraq wakiwemo wale wanajitoa mhanga katika mabomu.
Mashambulizi zaidi yanatarajiwa kwa waumini wa dini ya Shia katika sherehe za za Ashura.

Thursday, October 30, 2014








Send Feedback

We appreciate your input!


  • Video does not load or slow to load
  • I'm having trouble sharing content
  • I see an error in content
  • I see an error in the content
  • Other
Please give an overall site rating: