Wednesday, February 1, 2012

AU yashindwa kuchagua mwenyekiti wa Tume

AU yashindwa kuchagua mwenyekiti wa Tume

 30 Januari, 2012 - Saa 19:19 GMT
Jean Ping
Jean Ping ataendelea kuwa mwenyekiti kwa miezi sita
Umoja wa Afrika umeshindwa kuchagua mwenyekiti mpya wa tume ya umoja huo licha ya duru tatu za upigaji kura mjini Adis Ababa.
Baada ya kupiga kura mara tatu, hakupatikana mshindi wa moja kwa moja kati ya wagombea wawili, mwenyekiti wa sasa Jean Ping kutoka Gabon na waziri wa mambo ya ndani wa Afrika Kusini Nkosazana Dlamini Zuma.
Sasa uchaguzi wa mweneykiti mpya wa Tume ya AU umeahirishwa hadi mkutano unaofuata, utakaofanyika nchini Malawi mwezi Julai.
Baada ya kushindwa kupata mshindi, viongozi wa Afrika waliafikiana Bwana Ping aendelee kama mwenyekiti hadi wakati hio.
Awali taarifa zilielezea kwamba naibu mwenyekiti Erastus Mwencha kutoka Kenya ndiye angeshikilia wadhifa huo hadi uchaguzi utakapofanyika.
Bi Zuma ambaye ni mke wa zamani wa Rais Jacob Zuma, na mmoja wa mawaziri waliohudumu kwa muda mrefu zaidi nchini Afrika Kusini aligombea kuwa mwanamke wa kwanza kuongoza kamati hiyo kuu ya Umoja wa Afrika, ambao una wanachama 54.
Bw Ping ambaye amekuwa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika tangu 2008 alikuwa anagombea kwa muhula wa pili.
Mwandishi wa BBC Noel Mwakugu anasema Bw Ping alikabiliwa na upinzani baada ya kushtumiwa na viongozi wa Afrika kwa kushirikiana na Ufaransa katika kumng'atua madarakani Rais wa Libya Muammar Gaddaffi.
Mwandishi huyo anasema kulikuwa na malalamiko kwamba Bw Ping hakuunga mkono mpango wa Umoja wa Afrika wa kukomesha ghasia nchini Libya, na pia ujumbe wa mapatanisho ulioongozwa na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma.
Shirika la Nato na waliokuwa waasi nchini Libya walikataa mpango huo wa AU, kwa kuwa haukumtaka Rais Gaddaffi kuondoka madarakani.

Nchi 25 zatia saini mkataba wa Euro

Nchi 25 zatia saini mkataba wa Euro

 31 Januari, 2012 - Saa 03:33 GMT
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron
Nchi 25 kati ya 27 wanachama wa jumuiya ya ulaya zimetia saini mkataba ambao utachunguza zaidi matumaizi ya bajeti. Lakini jamhuri ya Czech na Uingereza hajizatia saini mkataba huo.
Mkataba huo mpya utasainiwa na nchi 25 mwezi Machi na baadaye lazima uidhinishwe.
Mkataba huo utaziwekea vikwazo nchi ambazo zitavunja sheria za matumizi ya fedha za jumuiya ya ulaya.
Nchi zilizotia saini mkataba huo pia zitahitajika kuongeza sheria kuhusu bajeti katika katiba zao.
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amesema kwamba angependa uchumi katika nchi za jumuiya ya ulaya kuimarika haraka iwezekanavyo lakini ameeleza wazi kwamba atachukua hatua ikiwa mkataba huo mpya wa kifedha utadhuru Uingereza.
Waziri mkuu huyo ameshtumiwa kwa kurudi nyuma katika utekelezaji wa ahadi ya kuzuia taasisi za jumuiya ya ulaya kutumika katika kufuatilia mkataba huo mpya.
Cameron amesema Uingereza itakuwa macho kuona kwamba mambo kama kuendesha shughuli za soko moja haziathiriwi.
Lakini amesema kwamba itakuwa vyema ikiwa nchi ambazo zinatumia sarafu ya Euro zitaweza kukumbana na madeni na ikiwa mkataba huu mpya utazisaidia kufanya hivyo.
Ujerumani inataka nchi zote zinazotumia sarafu ya Euro zitie saini mkataba huo, ambao utakua na sheria kali zaidi za bajeti, kabla iamue kama itatumia fedha zaidi kusaidia nchi hizo kupambana na mdororo wa uchumi.

Polisi watawanywa Senegal

Polisi watawanywa Senegal

 31 Januari, 2012 - Saa 14:24 GMT
Wade
Rais Wade anataka kuwania muhula wa tatu
Idadi kubwa ya polisi nchini Senegal wamepelekwa katikati ya mji mkuu wa Dakar kuzuia mkutano mkubwa ulioitishwa na upande wa upinzani.
Kundi la vyama vya upinzani liitwalo M23, linapinga mipango ya Abdoulaye Wade ya kuwania muhula wa tatu wa urais.
Watu wawili walipigwa risasi siku ya Jumatatu mjini Podor wakati wa maadamano baada ya mahakama kusema hatua ya Bw Wade ni halali.
Kundi la M23 linasema linadhamiria kuandamana hadi katika jumba la rais.
Uchaguzi katika taifa hilo la magharibi mwa Afrika unatarajiwa kufanyika Februari 26.
Waandishi wa habari wanasema polisi wanawazuia waandamanaji kufika katika eneo la mkutano, liitwalo Place de l'Obelisque katikati ya jiji, ambapo viongozi wa M23 wamewataka waandamanaji wakusanyike hapo.
Mapema, mwanaharakati Alione Tune ambaye pia ni mjumbe wa M23 aliachiliwa huru na polisi bila mashataka yoyote baada ya kuzuiliwa kwa siku mbili.
Baada ya kuachiliwa huru, aliliambia shirika la habari la AFP kuwa polisi walimuuliza "maswali mengi kuhusu maandamano" yaliyopangwa na M23.
Mwandishi wa BBC Abdourahmane Dia mjini Dakar amesema kuna wasiwasi maandamano ya Jumanne yanaweza yakasababisha ghasia kwa sababu hayajaruhusiwa kufanyika.
Lakini upande wa upinzani umesema una haki ya kikatiba kuandaa mikutano ya hadhara nchini kote.
Mwandishi wetu anasema miili ya waandamanaji wawili waliouawa mjini Podor siku ya Jumatatu imepelekwa Dakar kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi.
Katiba ya Senegal inaruhusu rais kuwania mihula miwili, lakini mahakama ya kikatiba ilisema sheria hiyo haimgusi Bw wade ambaye aliingia madarakani kabla haijawekwa.
Wakati Bw Wade ameruhusiwa kuwania urais, mahakama ya katiba iliwakatalia mwimbaji Youssou N'Dour na wagombea wengine wawili wa upinzani kugombea urais.

ICTR yawaombea hifadhi walioachiwa huru

ICTR yawaombea hifadhi walioachiwa huru

 31 Januari, 2012 - Saa 18:46 GMT
ICTR
Majaji katika mahakama ya ICTR
Mahakama inayoendesha kesi za mauaji ya kimbari yaliyotokea Rwanda mwaka 1994 imetoa wito kwa mataifa kutoa hifadhi kwa wale walioondolewa mashtaka.
Watu 5 kati ya watu 10 walioondolewa lawama za kuhusishwa katika mauaji hayo wanasema hawawezi kurejea nchini Rwanda.
Wanaishi chini ya ulinzi wa Polisi katika nyumba moja mjini Arusha, Tanzania, ambako ndiko makao ya mahakama hiyo ya ICTR.
Mahakama hiyo ya ICTR inatarajiwa kufunga mwishoni mwa mwaka huu.
Watu 800,000 kutoka jamii ya waTutsis na waHutus wenye msimamo wa kadiri waliuwawa katika kipindi cha siku 100 nchini Rwanda mwaka 1994.
Msemaji wa ICTR Roland Amoussouga ameambia BBC kupatikana nchi za kuwahifadhi wale ambao hawakupatikana na hatia ndio changamoto kuu inayokabili mahakama.
"Ni mzigo mkubwa kwetu kuendelea kuwahifadhi watu hawa walioachiwa huru kwa muda wa miaka mingi hivi, na tumeshirikiana nao, pamoja na mawakili wao kutafuta nchi ambako wanaweza kupelekwa. Hadi sasa hatujafanikiwa," alisema.
Wote 5 walioko mjini Arusha ni kutoka kabila la waHutu na miongoni mwao ni afisa wa zamani wa jeshi wa cheo cha Brigadier generali, mawaziri wa zamani na mfanya biashara mmoja.
Wanaishi pamoja katika nyumba inayolindwa, wanaweza kwenda mjini na kanisani, lakini hawawezi kuondoka huko.
Waziri wa zamani wa uchukuzi Andre Ntagerura amekuwa akisubiri kupata hifadhi kwa kipindi cha miaka 6 tangu mashtaka dhidi yake yalipoondolewa.
Wengine wawili wameshatumika vifungo vyao lakini hawana pa kwenda.
Wote wana familia nchini Ubelgiji, Canada na Ufaransa lakini hadi sasa hawawezi kupewa vibali kujiunga na familia zao, licha ya maombi kutoka baraza la usalama la umoja wa mataifa.

Mitt Romney easily clinches Florida primary

Mitt Romney easily clinches Florida primary

Former Massachusetts Gov. Mitt Romney coasted to a first-place finish in Florida's primary Tuesday, laying claim to all of the state's 50 delegates in the significant winner-take-all contest.