Wednesday, June 24, 2015

Kondomu inayotambua maambukizi ya Zinaa

Kondomu inayotambua maambukizi ya Zinaa

 
Kondomu inayotambua maambukizi ya zinaa
Wanafunzi katika shule moja nchini Uingereza wameunda mipira ya kondomu inayowaonya watumiaji wanapojamiana na mtu aliyeambukizwa maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo inabadili rangi pindi inapokutana na majimaji ya mtu anayeugua maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
Kulingana na wanafunzi hao kondomu hiyo inabadili rangi tofauti kulingana na bakteria iliyopo.
Uvumbuzi huu ni wa Daanyaal Ali, 14, Muaz Nawaz, 13 na Chirag Shah, 14, ambao ni wanafunzi katika shule ya Isaac Newton Academy iliyoko Ilford, Essex, nchini Uingereza.
 null
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
''tuliazimia kumpa onyo mtumiaji wa mipira hii kuwa mpenzi wake yuko salama ama ni mgonjwa bila ya wasiwasi wa kupimwa hospitalini''.
Wanafunzi hao tayari wametunukiwa, tuzo la ubunifu la ''the TeenTech'' .
Daanyall alisema kuwa "Walizindua kondomu hiyo ilikuifaidi kizazi kijacho''
''Kwa hakika swala la usalama wa mpenzi wako ni swala la kibinafsi kwa hivyo ni swala linalopaswa kupewa kipaombele haswa ikifahamika kuwa tunawajibu wa kuchochea ngono salama bila ya kuwashurutisha wapenzi wetu kufika hospitalini bila wao wenyewe kukusudia''
 null
Wavumbuzi hao wanasema kuwa hiyo ni mojawepo ya njia salama ya kubaini usalama penzi lenyu
Wanafunzi hao waliwalitunukiwa pauni elfu moja pamoja na fursa ya kuzuru Kasri la Malkia wa Uingereza Buckingham Palace.
Muasisi wa kampuni ya ubunifu wa kiteknolojia, TeenTech, Bwana Maggie Philbin, alisema kuwa
"Ni wajibu wetu kama jamii kuchochea ubunifu unaopatikana madarasani kuchochewa na kupigwa msasa kwa minajili ya kuboresha maisha ya mwanadamu''

Facebook kukutambua bila picha ya uso Dakika 49 zilizopita Mshirikishe mwenzako Facebook Tayari mtandao huo wa kijamii wa Facebook unakusanya taarifa kutoka katika picha zako ili kubaini migao ya maoni kutoka kwa marafiki wako pale wanapoweka mtandaoni picha. Sasa inaonekana mitandao ya kijamii inachukua mkondo mwingine wa kuboreshwa zaidi. Watafiti kutoka katika idara ya upelelezi ya Facebook wamekuwa wakiifanyia kazi teknolojia hiyo mpya ambayo nia kuu ni kumtambua mtu hata kama uso wake hauonekani bayana kwenye picha. Teknolojia hiyo iitwayo 'algorithm', inaangazia zaidi ya viungo mia moja vya mwanadamu. Inatumika kwa pamoja katika kutambua uso wa mtu na pia mwili mzima wa binadamu. Watafiti hao walitumia njia hiyo kwa kuzifanyia majaribio picha elfu 37 za watu ambazo zilitolewa kutoka kwa 'Flickr Commons'. Wanasema kuwa njia hiyo ilitoa matokeo asilimia 83 ya watu 581 tofauti. Matokeo hayo yaliwasilishwa mapema mwezi huu wa Juni katika kongamano la wakfu wa Computer Vision.

Facebook kukutambua bila picha ya uso


 
Facebook
Tayari mtandao huo wa kijamii wa Facebook unakusanya taarifa kutoka katika picha zako ili kubaini migao ya maoni kutoka kwa marafiki wako pale wanapoweka mtandaoni picha.
Sasa inaonekana mitandao ya kijamii inachukua mkondo mwingine wa kuboreshwa zaidi.
Watafiti kutoka katika idara ya upelelezi ya Facebook wamekuwa wakiifanyia kazi teknolojia hiyo mpya ambayo nia kuu ni kumtambua mtu hata kama uso wake hauonekani bayana kwenye picha.
Teknolojia hiyo iitwayo 'algorithm', inaangazia zaidi ya viungo mia moja vya mwanadamu.
Inatumika kwa pamoja katika kutambua uso wa mtu na pia mwili mzima wa binadamu.
Watafiti hao walitumia njia hiyo kwa kuzifanyia majaribio picha elfu 37 za watu ambazo zilitolewa kutoka kwa 'Flickr Commons'.
Wanasema kuwa njia hiyo ilitoa matokeo asilimia 83 ya watu 581 tofauti.
Matokeo hayo yaliwasilishwa mapema mwezi huu wa Juni katika kongamano la wakfu wa Computer Vision.

US iliwachunguza marais wa Ufaransa

US iliwachunguza marais wa Ufaransa


 
Marais wa Ufaransa
Kitengo cha ujasusi nchini Marekani NSA kiliwachunguza marais wa Ufaransa akiwemo Jacques Chirac,Nicolas Sarkozy na Francois Hollande mwaka 2006-12,kulingana na mtandao wa wikileaks.
Mtandao huo ulipata habari hizo kutoka kwa ripoti za kiintelijensia na stakhabadhi nyengine za kiufundi za NSA.
Afisa mmoja wa Ufaransa amesema kuwa upelelezi wa washirika haufai.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande anatarajiwa kujadili swala hilo na maafisa wa usalama.
Marekani haijathibitisha ukweli wa stakhabadhi hizo
.null
Wikileaks
Mwaka 2013 shirika la ujasusi la Marekani NSA lilishtumiwa kwa kumpeleleza kansela wa Ujerumani Angela Merkel.
Siku ya jumanne,Wikileaks ilisema kuwa ilianza kuchapisha faili zilizo na kichwa ''Espionage Elysee'' ikiwa ni kumbukumbu za ikulu ya rais wa Ufaransa.
Imesema kuwa faili hizo za siri zilipatikana kupitia upelelezi wa moja kwa moja wa mawasiliano uliofanywa na shirika hilo kwa marais hao watatu wa Ufaransa pamoja na balozi wa Ufaransa nchini Marekani.
Moja ya faili hizo ilioandikwa mwaka 2012,ni kuhusu rais Hollande alivyokuwa akizungumza kuhusu kuondoka kwa Ugiriki katika muungano wa Ulaya.
Nyengine ya mwaka 2011 inadai kuwa bwana Sarkozy aliamua mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina bila kuhusisha Marekani.
 null
Mwanzilishi wa Wikileaks Julian Assange
Faili nyengine ilioandikwa mwaka 2010 inadai kwamba maafisa wa Ufaransa walijua kwamba Marekani ilikuwa ikiwapeleleza na kwamba walipanga kutoa malalamishi yao.
Kulingana na habari za mawasiliano yaliodukuliwa,balozi wa Ufaransa nchini Marekani na mshauri wa rais Sarkozy walijadiliana kuhusu mpango wa Sarkozy kutoa ghadhabu zake kuhusu kukataa kwa Marekani kutia saini makubaliano ya ushirikiano wa kijasusi,ikiwa lengo ni kwa Marekani kuendelea kuipeleleza Ufaransa.