Monday, May 4, 2015

Floyd Mayweather amshinda Pacquiao

Floyd Mayweather amshinda Pacquiao

  • 3 Mei 2015
Pacquiao na Mayweather
Bondia wa Marekani Floyd Mayweather ameshinda pigano lililosubiri kwa wingi katika miongo kadhaa.
Mayweather amshinda Pacquiao
Bondia huyo ambaye hajashindwa alimshinda mpinzani wake raia wa Ufilipino Manny Pacquiao kwa wingi wa pointi.
Pacquiao akimpiga makonde mayweather
Mashabiki wengi waliojaa katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena mjini Las Vegas walimzoma mara kwa mara Mayweather.
Mayweather ashinda kwa wingi wa pointi
Kote duniani wateja millioni 3 walilipa kuliona pigano hilo ambalo ndio pigano lililovutia kitita kikubwa cha fedha katika historia ya ndondi.
Mayweather
Tiketi nyingi za pigano hilo ziliuzwa katika bei ya makumi ya maelfu ya dola.

Mkuu wa majeshi Burundi akemea wanasiasa

Mkuu wa majeshi Burundi akemea wanasiasa

  • 3 Mei 2015
Mkuu wa majeshi ya Burundi Meja Jenerali Prime Niyongabo
Mkuu wa majeshi nchini Burundi Meja Jenerali Prime Niyongabo ametoa wito kwa wanasiasa kutotumia jeshi la taifa kwa manufaa yao ya kisiasa.
Jenerali Niyongabo amekariri tangazo lililotolewa na waziri wa ulinzi Jumamosi kuwa jeshi la nchi hiyo litahakikisha kuwa mkataba wa Arusha umetekelezwa kikamilifu na kuwa jeshi hilo halitumiwi na mtu au chama chochote cha kisiasa.
Kuhusiana na maandamano yanayoendelea, mkuu huyo wa jeshi amesema kuwa maandamano hayo sio halali na wanaichi wanapaswa kutumia mbinu za sheria zilizopo kutatua mizozo yao.
Polisi wa kuzuia ghasia wakikabiliana na waandamanaji katika mitaa ya Bujumbura nchini Burundi
Wakati huo huo Meja Jenerali Niyongabo amesema jeshi hilo litasalia kuwa lenye nidhamu ya hali ya juu na tiifu kwa taifa la Burundi na wala sio kwa mwanasiasa yeyote.
Ameongeza kusema kufikia sasa jeshi limefanya kazi nzuri kuhakikisha kuwepo kwa usalama nchini Burundi na katika mataifa mengine wanakohudumu katika vikosi vya Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika.
Mkuu huyo wa majeshi amesema wanajeshi wataendelea kushirikiana na polisi kushika doria ili kuhakikisha amani na utulivu vinakuwepo nchini Burundi.
Huku hayo yakijitokeza muungano wa upinzani umesema kuwa maandamano yataendelea siku ya Jumatatu baada ya mapunziko ya siku mbili.
Upinzani umepinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza ya kuwania muhula wa tatu kama rais.